Friday, September 27, 2019

MAMIA YA WAOMBOLEZAJI WAJITOKEZA KUMZIKA MTOTO WA MKUU WA MAJESHI ALIYEFARIKI KWA AJALI YA NDEGE


Mamia ya wananchi kutoka mikoa ya Simiyu, Mara, Shinyanga, Mwanza na Dar es Salaam wameshiriki katika mazishi ya mtoto wa Mkuu wa Majeshi  marehemu Nelson Mabeyo aliyekuwa rubani wa ndege ya Shirika la Auric Air, ambaye alifariki Septemba 23, 2019 kwa ajali ya ndege iliyotokea katika Uwanja mdogo wa Seronera  uliopo katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti mkoani Mara.

Mazishi hayo yamefanyika Septemba 26, 2019 katika Kijiji cha Masanzakona wilaya ya Busega Mkoani Simiyu, ambapo yalitanguliwa na ibada ya mazishi iliyofanyika katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Yuda Tadei lililipo kijijini hapo ambapo ni nyumbani kwao na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Venance Mabeyo.

Akihubiri wakati wa ibada ya mazishi, Askofu Michael Msonganzila, Jimbo Katoliki Musoma amewasihi waombolezaji wote kuendelea kuifariji na kuiombea familia ya Mkuu wa Majeshi ili wapokee msiba huo kwa jicho la imani, masikio ya imani na kama mpango wa Mungu.

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi akitoa salamu za serikali  amesema “marehemu Nelson Mabeyo alikuwa  kijana mcheshi na mchapakazi leo hatuko naye tena nitoe pole kwa familia ya Jenerali Mabeyo, sisi ni wa Mwenyezi Mungu na kwake tutarejea niwaombe tuendelee kuwaombea katika kipindi hiki kigumu Mwenyezi Mungu awape ustahimilivu.”

Naye Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka akizungumza  kwa niaba ya wananchi wa mkoa wa Simiyu na wakuu wa mikoa ametoa pole kwa familia ya Mkuu wa Majeshi na kumshukuru kwa namna Mkuu  alivyowaunganisha watu wa Masanza, Busega na Simiyu katika masuala mbalimbali ya  ikiwemo Ujenzi wa Kanisa ambalo ibada ya mazishi ya marehemu Nelson imefanyika.

Kwa upande wake  Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenrali Venance Mabeyo amewashukuru watu wote walioshirikiana na familia yake tangu msiba wa mwanaye Nelson ulipotokea , ambapo amesema kama familia hawauchukulii msiba huo kama adhabu bali makusudi ya Mungu mwenyewe kwa mtoto wao .

Mazishi ya marehemu  Nelson Mabeyo yalihudhuriwa na  watu mbalimbali wakiwemo viongozi wa dini, viongozi na Maafisa wa JWTZ walioko kazini na wastaafu, mawaziri na manaibu waziri, makatibu wakuu, wakuu wa Taasisi, viongozi wa Vyombo vya Usalama, wabunge, Wakuu wa mikoa ya Simiyu, Mara, Shinyanga, Kagera, Kigoma, Mwanza na Dar es salaam , kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa wa Simiyu na wakuu wa wilaya.
MWISHO




Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Venance Mabeyo na mkewe Tina Mabeyo  wakiweka shada la maua katika kaburi la mtoto wao Rubani Nelson Mabeyo  ambaye alifariki katika ajali ya ndege Septemba 23, 2019 Seronera katika hifadhi ya Taifa ya Serengeti Mkoani Mara ; ambaye amezikwa Septemba 26, 2019 katika Kijiji cha Masanza wilayani Busega Mkoani Simiyu.


Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi akiweka shada la maua katika Kaburi la Rubani Nelson Mabeyo  mtoto wa Mkuu wa Majeshi  ambaye alifariki katika ajali ya ndege Septemba 23, 2019 Seronera katika hifadhi ya Taifa ya Serengeti Mkoani Mara ambaye amezikwa Septemba 26, 2019 katika Kijiji cha Masanza wilayani Busega Mkoani Simiyu.


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (wa pili kushoto) na wakuu wa mikoa ya Mwanza, Mara, Shinyanga, Kagera, Kigoma na Dar es Salaam wakiweka shada la maua katika Kaburi la Rubani Nelson Mabeyo  mtoto wa Mkuu wa Majeshi  ambaye alifariki katika ajali ya ndege iliyotokea Septemba 23, 2019 Seronera katika hifadhi ya Taifa ya Serengeti Mkoani Mara, ambaye amezikwa Septemba 26, 2019 katika Kijiji cha Masanza wilayani Busega Mkoani Simiyu.


Baadhi ya askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania wakiweka Jeneza lenye mwili wa mtoto wa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Venance Mabeyo, marehemu rubani Nelson Mabeyo aliyefariki kwa ajali ya ndege Septemba 23, 2019 Seronera Mkoani Mara ; ambaye amezikwa Septemba 26, 2019 katika Kijiji cha Masanza wilayani Busega Mkoani Simiyu.
 Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Venance Mabeyo na mkewe Tina Mabeyo  wakishuhudia jeneza lenye mwili wa  mtoto wao Nelson Mabeyo  ambaye alifariki katika ajali ya ndege Septemba 23, 2019 Seronera katika hifadhi ya Taifa ya Serengeti Mkoani Mara likishushwa kaburini wakati wa mazishi yake yaliyofanyika Septemba 26, 2019 Kijiji cha Masanza wilayani Busega Mkoani Simiyu.
 Viongozi mbalimbali wa Serikali wakitoa heshima za mwisho kwa mwili mtoto wa Mkuu wa majeshi Jenerali Venance Mabeyo, marehemu rubani Nelson Mabeyo  aliyefariki katika ajali ya ndege Septemba 23, 2019 Seronera katika hifadhi ya Taifa ya Serengeti Mkoani Mara, ambaye amezikwa Septemba 26, 2019 katika Kijiji cha Masanza wilayani Busega Mkoani Simiyu.


 Maaskofu wa Katoliki kutoka Majimbo ya Mara na Geita wakiweka shada la maua katika kaburi la mtoto wa Mkuu wa majeshi Jenerali katika hifadhi ya Taifa ya Serengeti Venance Mabeyo, marehemu rubani Nelson Mabeyo  aliyefariki katika ajali ya ndege Septemba 23, 2019 Seronera Mkoani Mara, ambaye amezikwa Septemba 26, 2019 katika Kijiji cha Masanza wilayani Busega Mkoani Simiyu.
Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Geita akiongoza ibada ya mazishi ya mtoto wa Mkuu wa majeshi Jenerali Venance Mabeyo, marehemu rubani Nelson Mabeyo  aliyefariki katika ajali ya ndege Septemba 23, 2019 Seronera katika hifadhi ya Taifa ya Serengeti Mkoani Mara, ambaye amezikwa Septemba 26, 2019 katika Kijiji cha Masanza wilayani Busega Mkoani Simiyu.
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi(mwenye miwani katikati) akizungumza jambo na baadhi ya viongozi wa Chama na Serikali mara baada ya ibada ya mazishi ya mtoto wa Mkuu wa majeshi Jenerali Venance Mabeyo, marehemu rubani Nelson Mabeyo  aliyefariki katika ajali ya ndege Septemba 23, 2019 Seronera katika hifadhi ya Taifa ya Serengeti Mkoani Mara, ambaye amezikwa Septemba 26, 2019 katika Kijiji cha Masanza wilayani Busega Mkoani Simiyu.








0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!