Monday, April 6, 2020

SIMIYU YAZINDUA KAMPENI YA ELIMU DHIDI YA MAAMBUKIZI YA CORONA


Mkoa wa Simiyu kwa kushirikiana na wadau wa afya umezindua rasmi kampeni ya kupambana na Maambukizi ya Ugonjwa wa Homa Kali ya mapafu unaosababishwa na virusi vya Corona kupitia utoaji wa elimu, ambapo Shirika la Msalaba Mwekundu limeanza kutoka elimu ya tahadhari ya ugonjwa huo katika Wilaya zote mkoani hapa hususani katika maeneo yenye muingiliano wa watu wengi kama vile stendi na masoko.

Akizindua kampeni hiyo Aprili 03,2020 Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amelishukuru Shirika la msalaba mwekundu kwa kujitoa kutoa elimu ya tahadhari ya maambukizi ya virusi vya Corona na kuwataka wataalam watakaotoa elimu hii kuendelea kuwahimiza wananchi kuzingatia maelekezo ya viongozi na wataalam wa afya ikiwa ni pamoja na kuepuka kupeana mikono, kuzuia mikusanyiko isiyo ya lazima, matumizi sahihi ya vitakasa mikono na kuhakikisha wananawa mikono kwa sabuni na maji tiririka.

“Sisi kama mkoa tunawashukuru sana Red Cross(Shirika la msalaba mwekundu) kwa kuanza kutoa elimu ya tahadhari dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona kwa wananchi, elimu hii ni vema ikaenda sambamba na kuwakumbusha wauzaji wa vitakasa mikono ili waweze kutengeneza vitakasa mikono kwa kuzingatia taratibu zilizowekwa na wauze kwa bei rafiki ya soko kwa wananchi,” alisema Mtaka.

Aidha, Mtaka amehimiza kuwa zoezi la utoaji elimu liende pamoja na kuwakumbusha wazazi na walezi kuwasimamia watoto wao kuhakikisha kuwa wanajisomea wakiwa majumbani katika kipindi hiki ambacho shule na vyuo vimefungwa ili wanafunzi hao waweze kufikia malengo yao hususani wanafunzi wa  madarasa ya mitihani.

Naye Mganga Mkuu wa Mkoa, Dkt. Festo Dugange amesema Mkoa wa Simiyu umewashirikisha wadau wote wa afya katika kuiandaa jamii kupambana na maambukizi ya Virusi vya Corona katika utoaji wa elimu ambayo ndiyo kinga, utoaji wa mafunzo kwa watoa huduma katika vituo vya kutolea huduma za afya na utoaji wa vifaa tiba na vifaa kinga lengo likiwa ni kuufanya mkoa wa Simiyu kutopata maambukizi ya virusi vya Corona.

Kwa upande wake Mratibu wa Mapambano dhidi ya Corona Mkoani Simiyu, Dkt. Khamis Kulemba amesema Mkoa wa Simiyu utashirtikiana na wadau katika kuhakikisha kuwa tahadhari na mapambano dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona yanafanikiwa.

Kwa upande wake mwakilishi wa Shirika la Msalaba Mwekundu Mkoa wa Simiyu,, Bw. Dismas Kiwale amesema Shirika hilo kwa kushirikianana watalam wa afya limekusudia kuwafikia wananchi hasa walio ndani zaidi(vijijini) na kupitia gari lao la matangazo wanatarajia kuzifikia kata zote na halmashauri zote sita za Mkoa wa Simiyu ambapo watakuwa wakitoa  elimu katika maeneo yenye muingiliano wa watu wengi na kugawa vipeperushi vyenye elimu juu ya tahadhari dhidi ya Corona.
MWISHO

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu. Mhe. Anthony Mtaka akikabidhi bendera ya Shirika la Msalaba mwekundu kama ishara ya uzinduzi wa kampeni ya mapambano dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona kupitia utoaji wa elimu kwa wananchi, uzinduzi huo ulifanyika Aprili 03, 2020 katika Viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mjini Bariadi.


 Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akibandika kipeperushi chenye ujumbe na elimu ya tahadhari dhidi ya Maambukizi ya Virusi vya Corona katika Ubao wa Matangazo katika Ofisi yake mara baada ya kuzindua kampeni ya mapambano dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona uzinduzi huo ulifanyika Aprili 03, 2020 katika Viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mjini Bariadi.


 Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt. Festo Dugange akifafanua jambo katika uzinduzi wa kampeni ya mapambano dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona kupitia utoaji wa elimu kwa wananchi, uzinduzi huo ulifanyika Aprili 03, 2020 katika Viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mjini Bariadi.


 Mwakilishi wa Shirika la Msalaba Mwekundu Bw. Dismas Kiwale akifafanua jambo katika uzinduzi wa kampeni ya mapambano dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona kupitia utoaji wa elimu kwa wananchi, uzinduzi huo ulifanyika Aprili 03, 2020 katika Viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mjini Bariadi.


 Mratibu wa Mapambano dhidi ya Corona Mkoani Simiyu, Dkt. Khamis Kulemba akifafanua jambo katika uzinduzi wa kampeni ya mapambano dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona kupitia utoaji wa elimu kwa wananchi, uzinduzi huo ulifanyika Aprili 03, 2020 katika Viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mjini Bariadi.


 Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akibandika kipeperushi chenye ujumbe na elimu ya tahadhari dhidi ya Maambukizi ya Virusi vya Corona katika Ubao wa Matangazo katika Ofisi yake mara baada ya kuzindua kampeni ya mapambano dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona uzinduzi huo ulifanyika Aprili 03, 2020 katika Viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mjini Bariadi.


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu. Mhe. Anthony Mtaka akikabidhi bendera ya Shirika la Msalaba mwekundu kama ishara ya uzinduzi wa kampeni ya mapambano dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona kupitia utoaji wa elimu kwa wananchi, uzinduzi huo ulifanyika Aprili 03, 2020 katika Viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mjini Bariadi. 

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!