Monday, April 6, 2020

UMOJA WA MAKANISA LAMADI WATOA VIFAA VYA UJENZI SHULE YA SEKONDARI ANTHONY MTAKA BUSEGA


Umoja wa makanisa kata ya Lamadi Wilayani Busega umetoa mchango wa vifaa vya ujenzi vikiwemo mchanga na saruji  kwa awamu ya kwanza kwa.ajili ya kuunga mkono juhudi za Serikali katika ujenzi wa vyumba vya madarasa katika Shule ya Sekondari ya Anthony Mtaka iliyopo katika Kijiji cha Lukungu kata ya Lamadi. 
Akipokea vifaa hivyo Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amewashukuru viongozi hao kwa kuona umuhimu wa kuchangia katika maendeleo ya elimu na kuahidi kuendelea kushirikiana na madhehebu ya dini wakati wote. 
Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Busega Tano Mwera aliushukuru Umoja wa Makanisa ya Kikristo Lamadi kwa mchango wao walioutoa kwa kutambua umuhimu wa kuchangia miundombinu ya elimu na huku akiyataka madhehebu mengine na jamii kwa ujumla kuona umuhimu wa jambo hilo. 
Naye mwenyekiti wa makanisa ya kikristo Lamadi, Mchungaji Michael Zacharia Kaburimoja amesema kuwa waliona umuhimu wa kuchangia miundombinu ya elimu ambapo wamechangia mchanga tripu 10 na mifuko mitano ya saruji yenye thamani ya shilingi laki saba. 
"Umoja wetu una jumla ya makanisa 30 ila yaliyoridhia kuchanga ni 21 na kila kanisa linamchango wake na kila tunapopokea michango tunaiwasilisha na hatujaishia hapa bado makanisa yanaendelea kuchanga," alisema Mchungaji kaburimoja 
Awali akisoma taarifa kwa niaba ya wachungaji wa makanisa hayo yaliyotoa mchango Mchungaji Emmanuel Edward Fyita kutoka Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG) ameiomba serikali kuona uwezekano wa kuipandisha hadhi ya shule ya sekondari Lamadi kutoka kidato cha nne hadi cha sita kutokana na ongezeko la wanafunzi wa kidato kwanza hadi cha nne kwenye kata hiyo.
Aidha, wameiomba serikali kuanzisha shule nyingine ya sekondari katika eneo la shule ya msingi lamadi ambapo bado kuna eneo kubwa lengo likiwa kuwapunguzia wanafunzi kutembea umbali mrefu. 
"Kuna wanafunzi wanaotoka vijiji vya mbali kama mwabasabi na Mwabulugu kwenda Lukungu waishie hapa lamadi badala ya kutembea mwendo mrefu na ujenzi huu utasaidia kukabiliana na ongezeko kubwa la wanafunzi katika shule zetu zilizo ndani ya kata ya Lamadi kwa sasa" alisema mchungaji Fyita. 
"Wachungaji tulio katika umoja huu tunakuahidi kuonesha njia kwa kujenga angalau chumba kimoja cha darasa," aliongeza mchungaji Fyita.
MWISHO
 Mwenyekiti wa makanisa Lamadi, Mchungaji Michael Zacharia Kaburimoja (kushoto) akitoa maelezo kwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka mara baada ya kuwasili katika Shule ya Sekondari Anthony Mtaka, wakati wa makabidhiano ya  msaada wa vifaa vya ujenzi wa madarasa katika shule hiyo uliotolewa na Umoja wa Makanisa Lamadi Machi 31, 2020.


 Mmoja wa Wachungaji akitoa sala wmara baada ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka na Viongozi wa Wilaya ya Busega mara baada ya kuwasili katika Shule ya Sekondari Anthony Mtaka wakati wa wakati wa makabidhiano ya  msaada wa vifaa vya ujenzi wa madarasa katika shule hiyo uliotolewa na Umoja wa Makanisa Lamadi Machi 31, 2020.


 Mwenyekiti wa makanisa Lamadi, Mchungaji Michael Zacharia Kaburimoja (kushoto) akimuongoza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka mara baada ya kuwasili katika Shule ya Sekondari Anthony Mtaka wakati wa makabidhiano ya msaada wa vifaa vya ujenzi wa madarasa katika shule hiyo uliotolewa na Umoja wa Makanisa Lamadi Machi 31, 2020.


 Mwenyekiti wa makanisa Lamadi, Mchungaji Michael Zacharia Kaburimoja (kushoto) akitoa maelezo kwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka mara baada ya kuwasili katika Shule ya Sekondari Anthony Mtaka wakati wa makabidhiano ya  msaada wa vifaa vya ujenzi wa madarasa katika shule hiyo uliotolewa na Umoja wa Makanisa Lamadi Machi 31, 2020.


 Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akieleza jambo mara baada ya kuwasili katika Shule ya Sekondari Anthony Mtaka wakati wa makabidhiano ya  msaada wa vifaa vya ujenzi wa madarasa katika shule hiyo uliotolewa na Umoja wa Makanisa Lamadi Machi 31, 2020.


Mwenyekiti wa makanisa Lamadi, Mchungaji Michael Zacharia Kaburimoja (kushoto) akitoa maelezo kwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka mara baada ya kuwasili katika Shule ya Sekondari Anthony Mtaka, wakati wa makabidhiano ya  msaada wa vifaa vya ujenzi wa madarasa katika shule hiyo uliotolewa na Umoja wa Makanisa Lamadi Machi 31, 2020.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!