Saturday, April 25, 2020

UONGOZI MASWA WATAKIWA KUMSIMAMIA MKANDARASI UJENZI WA VIWANDA VIKAMILIKE KWA WAKATI

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhandisi Joseph Nyamhanga ameutaka uongozi wa Wilaya ya Maswa kumsimamia Mkandarasi SUMA JKT anayejenga kiwanda cha chaki  na kiwanda cha vifungashio wilayani humo ili akamilishe ujenzi wa viwanda hivyo kwa wakati ili vianze uzalishaji.


Nyamhanga ameyasema hayo wakati wa ziara yake alipotembelea kuona maendeleo ya ujenzi wa viwanda hivyo eneo la Ng’hami ambapo ameutaka uongozi wa Wilaya ya Maswa kufuatilia uagizaji wa mitambo ya kiwanda cha chaki huku akiahidi kuwa ofisi yake itafuatilia kibali cha kuagiza Mitambo kwa ajili ya kiwanda cha vifungashio. katika Ofisi ya HAZINA(Wizara ya Fedha)ili miradi yote iende sambamba.



0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!