Wednesday, November 17, 2021

MKUU WA MKOA WA SIMIYU ATAKA KASI ZAIDI UJENZI WA MADARASA YA UVIKO/IMF

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. David Kafulila amefanya ukaguzi wa ujenzi madarasa 6 katika shule tatu za Sekondari ( Mwakaleka, Nyalikungu na Binza) zilizopo wilayani Maswa na kubainisha kuwa taratibu za ujenzi zinaonekana kwenda vema na kuzitaka Kamati za shule zinazosimamia ujenzi kuhakikisha mambo matatu; ubora, kasi na thamani kwa maana ya bei. Amezipongeza Kamati za shule zinazosimamia ujenzi na kuelekeza Halmashauri na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Maswa kuhakikisha Kamati hizo zinamiliki miradi hiyo kwa kufanya kila kitu ili kupunguza urasimu katika maeneo ambayo shule zimejipanga vizuri. Mkoa wa Simiyu umepokea zaidi ya TZS.11.6/-Bln, kwa ajili ya miradi na mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano ya Uviko-19, ambapo Wilaya zilipokea fedha zifuatazo: Maswa Tsh. 2.1 bln, Meatu Tsh.2.0 bln, Busega Tsh.bln na Bariadi vijijini Tsh. 2.05 bln. 

Mwisho.




Mkuu wa Mkoa Mhe David Kafulila akitembelea  miradi ya ujenzi wa shule za Uviko-19/IMF







Mhe. Kafulila akiwa pamoja na Mwenyekiti wa CCM  Mkoa wa Simiyu Bi. Shamsa Mohamed  na baadhi ya Viongozi wa Mkoa na Halmashauri ya Wilaya ya Maswa wakitembelea miradi ya Ujenzi ya Shule 6 za Sekondari





0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!