Thursday, November 18, 2021

WAZIRI MKUU MSTAAFU NA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CCM ATEMBELEA OFISI YA MKUU WA MKOA SIMIYU

Waziri Mkuu Mstaafu na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa Mhe.Mizengo K.Pinda , jumatatu tarehe 15/11/2021,alitembelea Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu kusaini Kitabu cha Wageni ambapo Mhe.Mkuu wa Mkoa wa Simiyu.Mhe David Z.Kafulila aliwasilisha kwake taarifa fupi katika Sekta mbalimbali za Miradi ya Maendeleo.


Mhe.Pinda alisisitiza miradi ya utekelezaji kwa fedha za covid 19 usimamiwe kikamilifu na Mkoa na kusiwepo na ubadhirifu wowote. Aidha alisisitiza viongozi wa CCM wasihusike kwa vyovyote vile katika utekelezaji wa miradi hiyo kuepusha mgongano  wa maslahi.  

Mhe.Waziri Mkuu mstaafu na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa alisisitiza suala la Udumavu(Malnutrition), lisimamiwe kikamilifu ili takwimu za Mkoa kwenye udumavu lishuke au liishe kabisa.

Mwisho.*

Waziri Mkuu Mstaafu na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa Mhe.Mizengo K.Pinda atembelea ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa, Katibu Tawala, Mkuu wa Wilaya Bariadi

Waziri Mkuu Mstaafu na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa Mhe.Mizengo K.Pinda akisaini kitabu cha wageni Ofisini kwa Mkuu wa Mkoa Simiyu

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!