Thursday, November 25, 2021

HALMASHAURI ZOTE IGENI MKOA WA SIMIYU-NAIBU WAZIRI (AFYA) TAMISEMI

Wito huo umetolewa leo na Mhe.Dkt.Festo Dungage NaibuWaziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serilkali za Mitaa (TAMISEMI-AFYA), mara baada ya kupokea taarifa ya utekelezaji wa mpango wa maendeleo kwa ustawi wa taifa na mapambano dhidi ya uviko 19 Mkoa wa Simiyu.

Mhe.Dugange,amepongeza Sekretarieti ya Mkoa, Mamlaka za Serikali za Mitaa na viongozi wote wa Mkoa wa Simiyu,kwa kazi nzuri wanayofanya.

"Hongera kwa kazi nzuri sana mnayofanya mkoa wa Simiyu. Hatua ya  ujenzi wa madarasa kufikia 85%, hiyo ni hatua kubwa sana. Lengo la Serikali ya awamu ya Sita ni kuhakikisha kwamba watoto wetu wanaoingia kidato cha kwanza 2022, wote wanaingia darasani kwa pamoja , hivyo hakutakuwa na uchaguzi wa kuingia kidato cha kwanza kwa mara ya pili yaani (second Selection).

Serikali ya Awamu ya sita imetoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 15000 kati ya hayo  madarsa 12000 ni kwa ajili ya shule za sekondari na  madarasa 3000  kwa ajili ya shule za msigi.Mkoa wa Simiyu umepatiwa shule 380.

Kuhusa sekta ya afya pongezi kwako Mkuu wa Mkoa, RHMT na RMO, kwani sekta hii ilikuwa na changamoto sana, mikataba ambayo inatoa viwango vya upimaji  utendaji kazi (Key Performance Indicator - KPI) na vikao vya kila robo mwaka ni ubunifu wa hali ya juu kwani inaleta uwajibikaji Kabla ya kuwa Naibu Waziri nilikuwa Mwanasimiyu/mganga Mkuu na hivyo namba yangu simu yangu ilitumika kupokea malamiko mbalimbali ya wanasimiyu.Kipindi cha nyuma kulikuwa na malalamiko  mengi sana ila ndani ya miezi 6 sijapata malalamiko yeyote.

"Asilimia 95 ya huduma za afya hutolewa na Mamlaka za Serikali za Mitaa ambzo zipo chini ya TAMISEMI. Niwapongeze sana Mkoa wa Simiyu kwani  kwa kipindi cha miezi sita  mlianza matumizi ya mfumo wa GoThomis, na   65% ya vituo vyenu vya afya vinatumia mfumo huo  kwa  ajili ya kukusanya mapato. Kama aliyoeleza mkuu wa Mkoa  mfumo huo umewasaidia kuongeza mapato kutoka Tsh.200mln–600mln. Makusanyo haya yanasaidia sana kuacha utegemezi toka Serikali kuu au wafadhili. Hivyo ni vyema Halmashauri zote ziige mkoa wa Simiyu" amesema Mhe. Dugange .


Akizungumza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. David Kafulila amemshukuru Mhe. Dugange kwa kutembelea mkoa wa Simiyu,na kumhakikishia kuwa ujenzi wa madarasa ambao umefikia  85% utamalizika kwa wakati. Kwa upande wa sekta ya afya Mhe. Kafulia amemfahamisha Naibu Waziri Tamisemi /afya kuwa mafanikio katika sekta ya afya yametokana na utendaji kazi mzuri wa Mganga mkuu wa mkoa pamoja na timu yake RMO,kwani kwa kipindi cha miezi sita mapato yameongezeka kwa asilimia 300. "Nimesaini mkataba wa utendaji kazi kati yangu na  Wakuu wa wilaya .Niwapongeze  wakuu wa Wilaya kuwa sasa tunasomana" amesema Kafulila.

 

Akiwasilisha taarifa ya hali ya utekelezaji mpango wa maendeleo kwa ustawi wa Taifa na mapambano dhidi ya UVIKO-19 mkoa wa Simiyu,Kaimu Katibu Tawala M,Injinia Mashaka Luhamba alieleza kuwa Mkoa wa Simiyu umetengewa jumla ya Tshs 20,476,951,633.30 kwa ajili ya kutekeleza miradi inayolenga kuimarisha miundombinu ya Sekta za Elimu na Afya na mapambano dhidi ya UVIKO 19. Fedha hizo zimetolewa kwa taasisi mbalimbali za Serikali zikiwemo Shule za Sekondari,Shule Shikizi,Hospitali za Wilaya katika ngazi za Halmashauri za Wilaya, Miji ,Manispaa na Majiji. Aidha, fedha zingine zimepelekwa kutekeleza miradi ya kipaumbele katika Hospitali ya Rufaa za Mkoa na Mamlaka za maji.

Kuhusu miradi ya ujenzi wa shule mkoani Simiyu,Injinia Luhamba amesema, hadi sasa miradi iliyoanza kutekelezwa ni ya ujenzi wa vyumba vya madarasa 380 vya shule za Sekondari na vyumba vya madarasa 69 vya Shule Shikizi. Mpaka sasa ujenzi huo umefikia  85% ya utekelezaji wa ujenzi wa vyumba vya madarasa.Injinia Luhamba ameeleza kuwa pamoja na mafanikio haya katika ujenzi wa Madarasa Mkoa umekuwa ukikabiliwa na  changamoto mbalimbali hususani katika Wilaya ya Maswa na Itilima ambapo changamoto kubwa imekuwa upatikanaji wa vifaa. Vifaa vya viwandani kama vile bati na saruji kuchelewa kufika katika maeneo husika hasa kwa Halmashauri ambazo zilitumia mfumo wa manunuzi ya pamoja. Bei ya vifaa kupanda ghafla mara tu miradi ilipoanza na hivyo kusababisha gharama ya mradi kuongezeka.Shule ambazo ziliomba kibali cha kuhamisha fedha kwenda katika maeneo mengine kwa ajili ya ujenzi zilichelewa kupata kibali na hivyo kusababisha kuchelewa kuanza kwa mradi.

Kuhusu sekta ya afya,mganga Mkuu Mkoa wa Simiyu Dkt. Boniface Marwa, ameeleza kuwa kwa kipindi cha miezi tisa kumekuwa na mafanikio makubwa sana katika sekta ya afya Mkoani Simiyu.Awali kulikuwa na vituo vya afya 218 lakini sasa kuna vituo vya afya 221.Aidha upatikanaji wa dawa nao umeongezeka kufikia asilimia 91.

 Dkt. Marwa amesema mafanikio yote haya yamepatikana kutokana ushirikiano uliopo baina ya wafanyakazi wa Sekta ya Afya, uongozi bora toka kwa mkuu wa mkoa na menejimenti yake. DKt Marwa amemfahamisha Naibu Waziri kuwa moja ya siri kubwa ya mafanikio haya ni usainishaji wa mikataba ya ya utendaji kazi katika sekta ya afya kati ya Mkuu wa Mkoa na Wakuu wa Wilaya ambao nao walisainishana na maafisa tarafa, Katibu Tawala na Wakurugenzi wa Halmashauri zote ambao nao wamesainishana na waganga wakuu wa halmashauri.

"Lengo la kusaini mikataba hii ni kuhakikisha utendaji kazi katika sekta ya afya unafanyika kwa weledi zaidi. Aidha ripoti za utendaji kazi zimekuwa zikitolewa kila robo mwaka na kwa kweli kumekuwa na mafaniko makubwa sana.Lengo letu ni kutaka kuwe na usimamizi na utendaji wa pamoja katika mkoa"amesema.Dkt Marwa.

 

Akijibu hoja kuhusu changamoto ya uhaba wa watumishi sekya ya afya Mhe. Dugange amekiri kuwa mkoa wa Simiyu ni mmoja kati ya mikoa inayokabiliwa na changamoto  kubwa ya uhaba wa Watumishi wa  sekta ya afya.Serikali imeliona hilo na  inafanyia kazi kwa  kuendesha zoezi la kujua daktari na N esi ikilinganishwa na idadi ya wagonjwa wanaopaswa kuhudumiwa na dakkati /nesi mmoja ( Doctor/Nurse Patient ratio).Lengo la Serkali ni kuhakikisha kuwa kila mkoa uwe na watumishi angalau si chini ya  60% ya mahitaji yao .Akizungumzia 40% ya mapato ya ndani baada ya kutoa mapato lindwa, Mhe. Dugange amesema kuwa lazima fedha hizo ziende kwenye miradi ya maendeleo.

 Mhe. Festo Dugange yupo ziara Mkoani Simiyu kwa lengo la kupitia miradi ya ujenzi wa madarasa ya Uviko na vituo vya afya,ili kuona shughuli zinazoendelea na Changamoto mbalimbali wanazokalibiana nazo katika utekelezaji wa shughuli hizo. Mwisho


NAIBU WAZIRI TAMISEMI (AFYA) MHE. DKT. FESTO DUGANGE AKISALIMIANA NA BAADHI YA VIONGOZI WA MKOA WA SIMIYU MARA BAADA YA KUWASILI MKOANI HAPO

KAIMU RAS , INJINIA MASHAKA LUHAMBA AKISOMA TAARIFA YA MKOA

MGANGA MKUU OFISI YA MKUU WA MKOA SIMIYU DKT. BONIOFACE MARWA AKISOMA TAARIYA YA SEKYA YA AFYA

KULIA, ANAYEONGEA NI NAIBU WAZIRI TAMISEMI(AFYA),MHE,DKT.FESTO DUGANGE AKIZUNGUMZA, KUSHOTO ANAYESIKILIZA KWA MAKINI MKUU WA MKOA WA SIMIYU MHE. DAVID KAFULILA
WASHIRIKI KUANZIA KUSHOTO KUTOKA SEKTA YA AFYA, AAS-ELIMU,ASS-LGA, NA SEKTA YA AFYA WAKISIKILIZA KWA MAKINI






 


0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!