Wednesday, November 17, 2021

SIMIYU YASHIKA NAFASI YA 4 KUTOKA NAFASI YA 20 (2019) MIRADI YA MWENGE KITAIFA !

Mkuu wa Mkoa Simiyu, Mhe.David Kafulila, leo amewapongeza wakurugenzi wa wakuu wa wilaya 5 za Mkoa wa Simiyu kwa kuendelea kuboresha usimamizi wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kusisitiza kuwa ni juhudi hizo zilizofanikisha mkoa wa simiyu kushika nafasi ya 4 mwaka huu 2021 kutoka nafasi ya 20 mwaka 2019.

 " Mimi naona fahari kuwa na timu hii ya wakuu wa wilaya na wakurugenzi. Mbali ya kupaisha mkoa huu kutoka nafasi ya 2 kutoka mwisho mwaka 2020 mpaka nafasi ya 2 juu katika makusanyo ya halmashauri kimkoa, leo nimepata taarifa kuwa mkoa wetu umeshika nafasi ya 4 kitaifa katika miradi ya mwenge iliyokaguliwa kulinganisha na nafasi ya 20 mwaka 2019.

 Naamini mwakani tutashika nafasi ya 1." Angalia hapa Busega, taarifa ya makusanyo ya robo ya mwaka wa fedha 2020 ilikuwa asilimia 15% ya lengo, kulinganisha na asilimia 29% kwenye robo ya kwanza mwaka 2021. Hivyo inawezekana. Tuendelee kupambana kujenga mkoa wetu " alisisitiza Kafulila wakati wa kikao cha mabaraza la Madiwani Wilayani Busega.

 Mwisho.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu  Mhe.David Kafulika akipokea mwenge wa Uhuru June 28,2021 kutoka kwa aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Ally  Hapi
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. David Kafulia akimkabidhi Mwenge wa Uhuru, Mkuu wa Wilaya ya Busega Mhe. Gabriel Zakaria.



Wakuu wa Wilaya za Mkoa wa Simiyu wakikabidhiana Mwenge wa Uhuru



0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!