Wednesday, November 24, 2021

Wilaya ya Bariadi, Yapongezwa kwa Kupata Leseni ya Kuchimba Madini

Washiriki wakimsikiliza kwa makini Mkuu wa Mkoa wakati wa kikao

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe.David Kafulila akizungumza na Washiriki wa kikao cha kuwapongeza Wanabariadi kwa kupata leseni ya Kuchimba Madini

Washiriki wakimsikiliza kwa makini Mkuu wa Mkoa 

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. David Kafulila amempongeza Mkuu wa wilaya ya Bariadi Mhe.Lupakisyo Kapange na Wakurugenzi Bw.Khalid Mwalami na Adrian Jungu kwa kazi kubwa ambayo wameendelea kuifanya katika sekta ya madini. 

Rc.Kafulila ametoa pongezi hizo kwenye kikao cha kukabidhi leseni ya kuchimba Madini kwa Mkurugenzi wa halmashauri ya Bariadi mji na Bariadi vijijini, hafla iliyofanyika hivi karibuni katika viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa wilaya Bariadi.

 " Nakupongeza Mkuu wa Wilaya, na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Bariadi mji na Bariadi vijijini , kwani Halmashauri ya Bariaji Vijijini ilikuwa dhoofu sana katika makusanyo kiasi cha kufikiria kuifuta. Lakini ndani ya miezi 6 imetoka nafasi za mkiani mpaka nafasi ya 15 kati ya halmashauri185 huku halmashauri ya mji ikishika nafasi ya 13".Amesema Kafulila.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!