Wednesday, November 24, 2021

RC. Kafulila - Ampongeza Mmiliki wa Kiwanda cha Kuchambua na Kusafisha dhahabu - ELIFRA INVESTMENT LIMITED.

Mhe.Kafulila,amempongeza mjasiliamali Frank Malima, ambaye ndiye mmiliki wa kiwanda cha kuchambua na kusafisha dhahabu cha ELIFRA INVESTMENT LIMITED.

Pongezi hizo zilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu akiwa ameambatana na Viongozi wengine wa Mkoa mara alipotembelea kiwanda cha kuchambua na kusafisha dhahabu cha ELIFRA INVESTMENT LIMITED kilichopo Mkoani Simiyu, hivi karibuni.

Akizungumzia Bw.Frank Malima, Mhe. Kafulila alieleza kuwa Bw. Malima  ni mubobezi wa masuala ya madini, maarifa ambayo ameyapata  nje ya nchi ikiwemo Afrika ya Kusini.

Akimshukuru, Mkuu wa Mkoa, Bw.Malima ameahidi kuwapatia kinamama mashine aina ya BALL MILL,mashine ambayo itaongeza uzalishaji kutoka wastani wa tani 5 kwa mwezi mpaka tani 100 kwa mwezi, hii ikiwa ni matumizi ya mashine moja.

Kiwanda cha kuchambua na kusafisha dhahabu cha ELIFRA INVESTMENT LIMITED kina uwezo wa kusafisha kilo 15-20 za dhahabu kwa siku. 




Ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Kafulila pamoja na viongozi wengine katika kiwanda cha kuchambua na kusafisha  dhahabu cha ELIFRA INVESTMENT LIMITED- Bariadi.


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe.David Kafulila wa kwanza Kulia, akiwa pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Mhe. Lupakisyo Kapange pamoja na Viongozi wengine wakipata maelezo wakati wa ziara ya kutembelea kiwanda cha Kuchambua dhahabu cha ELIFRA INVESTMENT LIMITED kilichopo Bariadi.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!