Thursday, November 12, 2020

RAIS MSTAAFU JAKAYA KIKWETE MGENI RASMI SERENGETI SAFARI MARATHON

 Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Awamu ya Nne, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika mashindano ya Serengeti Safari Marathoni yanayotarajiwa kufanyika tarehe 14 Novemba 2020 kuanzia lango la Ndabaka wilayani Busega mkoani Simiyu 

Akizungumza na waandishi wa habari leo Novemba 12, 2020 ofisini kwake Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema mbio hizo zitahusisha mikoa miwili ya Simiyu na Mara  na akatoa wito kwa wananchi wa mikoa ya hiyo kujitokeza kwa kushiriki katika mbio hizi ambazo zinalenga kutangaza hifadhi ya Taifa ya Serengeti ambayo asilimia 70 ipo mkoa wa Mara na asilimia 30 ipo mkoa wa Simiyu.

“Mhe. Rais Mstaafu Jakaya Kikwete atakuwepo hapa tarehe 13/11/2020, tarehe 14/11/2020 ataanzisha rasmi mbio hizo na atashiriki mbio za kilomita tano na baadaye ataongoza uvalishaji wa medali kwa wachezaji na washiriki watakaokuwepo kwenye mbio ndefu,” alisema Mtaka.

Kwa upande wake  Mkurungenzi wa Serengeti Safari Marathon Bw.Timothy Mdinka amesema lengo kubwa la Serengeti Safari Marathon ni kukuza utalii wa ndani na nje ya nchi ambapo amebainisha kuwa Mbio hizi zimeanza tarehe 12/11/20  na Kilele chake ni 14/11/2020. 

Kutakuwa na aina nne za mbio; ambazo ni kilomita  42 (Half Marathon),  Kilomita 21 (Half Marathon), Kilometa 10 (Executive Run)  na kilomita tano (Fun Run);  kwa washindi zinategemeana na aina ya Mbio, Zawadi zitaanzia Tsh. 100,000/= hadi Tsh.600,000/=, ,” alisema Mdinka. 

Mdinka ameongeza kuwa wanatarajia kuwa na washiriki takribani  800, kutoka mikoa yote nchini, ,Afrika Mashariki na Ulaya ya Mashariki ambapo pia amebainisha kuwa kutakuwa na mbio za watoto, lengo likiwa kuwahamasisha  watoto wawe wakimbiaji wazuri wa baadaye.

MWISHO

 

Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Awamu ya Nne, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(kulia) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) ofisini kwake Mjini Bariadi juu ya mbio za Serengeti Marathon zinazotarajiwa kufunguliwa rasmi na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Awamu ya Nne, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete Novemba 14, 2020 kuanzia lango la Ndabaka wilayani Busega.

Mkurungenzi wa Serengeti Safari Marathon Bw.Timothy Mdinka(kushoto) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu mjini Bariadi juu ya maandalizi ya mbio za Serengeti Marathon zinazotarajiwa kufunguliwa rasmi na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Awamu ya Nne, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete Novemba 14, 2020 kuanzia lango la Ndabaka wilayani Busega.

 


0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!