Tuesday, November 24, 2020

SERIKALI YAWAHAKIKISHIA WACHIMBAJI WADOGO WA DHAHABU BARIADI KUPEWA LESENI

Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Prof. Simon Msanjila amewahakikishia wachimbaji wadogo katika mgodi wa dhahabu wa Bulumbaka uliopo katika kijijj cha Gasuma wilayani Bariadi mkoani hapa kuwa watapata leseni za uchimbaji na kusisitiza kuwa kamwe hawataondolewa katika mgodi huo. 


Prof. Msanjila ameyasema hayo jana Novemba 23, 2020 wakati akizungumza katika kikao chake na baadhi ya viongozi wa Wilaya ya Bariadi, Mkoa wa Simiyu, baadhi ya wamiliki wa mashamba katika eneo la mgodi na baadhi ya wachimbaji wadogo, katika Kijiji cha Gasuma wilayani Bariadi. 


"Muombe leseni mtapewa, leseni haiwezi kutolewa kwa mtu kutoka huko aliko halafu hawa vijana ambao wanachimba sasa hivi wakaondolewa hapana; najua kuna maombi nayaonaona kwenye mitandao lakini msiwe na wasiwasi hayawezi kutoka," alisema Prof. Msanjila. 


Aidha, Prof. Msanjila ameeleza utaratibu wa fidia kwa wenye mashamba "tusiichukulie kwamba kwa kuwa na shamba unakuwa na haki ya kuchimba, hapana; ila ni kwamba wale wanaochimba hawana fedha ya kukufidia, sasa  tumeweka utaratibu kwamba fidia yako uipate taratibu kwenye mgao na naamini huwa ni nyingi kuliko fidia nyingine.”

 

Katika hatua nyingine Prof. Msanjila amemtaka Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga kuanzisha upya mchakato wa kumpata msimamizi wa mgodi wa Bulambaka ambaye atahakikisha ulinzi unaimarishwa, mazingira yanaboreshwa ikiwa ni pamoja na uchimbaji wa vyoo pamoja na kuimarisha uhusiano mzuri miongoni mwa wachimbaji.


Awali baadhi ya wachimbaji wadogo na wamiliki wa mashamba walisilisha changamoto mbalimbali zinazowakabili katika mgodi huo ikiwa ni pamoja na kuomba uboreshaji wa miundombinu na upatikanaji wa huduma muhimu, ambapo Msanjila amebainisha kwamba Serikali inazifanyia kazi na baadhi zitatatuliwa na msimamizi wa mgodi huo baada ya kukamilika kwa mchakato wa kumpata ambao utaanzishwa Mkuu wa Wilaya. 


“Wachimbaji tumewekeza gharama kubwa sana, tunaomba serikali isaidie kuimarisha ulinzi na usimamizi wa mali tunazochimba na kuendelea kuboresha miundombinu ili tuweze kusafirisha mali tunazochimba hapa kwa urahisi,” alisema mchimbaji mdogo Wibelo Kihalata. 


“Wenye Maeneo tuliomba leseni ili na sisi tuweze kufanya kazi na Watanzania wenzetu, tunashukuru kwa kuwa mmetueleza kuwa hata sisi tukijiunga tunaweza kupata leseni tukachimba na siyo wenye hela peke yao tu,” alisema Masuke Sahani Mwenyekiti wa Kikundi cha Umoja Bulumbaka Bariadi. 


Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga amesema  atahakikisha mchakato wa kumpata msimamizi wa mgodi linafanyika kwa uwazi na kusimamia uendeshaji wa mgodi huo kwa kufuata sheria, kanuni, taratibu na miongozo  kutoka wizara ya Madini.

 

Naye Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bibi. Miriam Mmbaga amesema Serikali ya mkoa wakati wowote itahakikisha inasimamia Serikali ya wilaya katika kuhakikisha shughuli zote zinazofanyika zinafuata sheria, kanuni na taratibu.

MWISHO 

Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Prof. Simon Msanjila akizungumza baadhi ya viongozi wa Wilaya ya Bariadi, Mkoa wa Simiyu, baadhi ya baadhi ya wachimbaji wadogo, wamiliki wa mashamba katika eneo la mgodi wa Bulumbaka  Novemba 23, 2020 katika Kijiji cha Gasuma wilayani Bariadi.
Baadhi ya wananchi wakimsikilza Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Prof. Simon Msanjila katika kikao chake na baadhi ya viongozi wa Wilaya ya Bariadi, Mkoa wa Simiyu, baadhi ya baadhi ya wachimbaji wadogo, wamiliki wa mashamba katika eneo la mgodi wa Bulumbaka  Novemba 23, 2020 katika Kijiji cha Gasuma wilayani Bariadi.
Mkuu wa Wilay ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga akizungumza katika kikao cha Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Prof. Simon Msanjila na baadhi ya viongozi wa Wilaya ya Bariadi, Mkoa wa Simiyu, baadhi ya wachimbaji wadogo, wamiliki wa mashamba katika eneo la mgodi wa Bulumbaka  Novemba 23, 2020 katika Kijiji cha Gasuma wilayani Bariadi.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bibi. Miriam Mmbaga akizungumza katika kikao cha Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Prof. Simon Msanjila na baadhi ya viongozi wa Wilaya ya Bariadi, Mkoa wa Simiyu, baadhi ya baadhi ya wachimbaji wadogo, wamiliki wa mashamba katika eneo la mgodi wa Bulumbaka  Novemba 23, 2020 katika Kijiji cha Gasuma wilayani Bariadi.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bibi. Miriam Mmbaga akizungumza katika kikao cha Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Prof. Simon Msanjila na baadhi ya viongozi wa Wilaya ya Bariadi, Mkoa wa Simiyu, baadhi ya baadhi ya wachimbaji wadogo, wamiliki wa mashamba katika eneo la mgodi wa Bulumbaka  Novemba 23, 2020 katika Kijiji cha Gasuma wilayani Bariadi.
Bw. Samwel Chegeni mmoja wa wamili wa mashamba akichangia hoja katika kikao cha Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Dkt. Simon Msanjila na baadhi ya viongozi wa Wilaya ya Bariadi, Mkoa wa Simiyu, baadhi ya wachimbaji wadogo, wamiliki wa mashamba katika eneo la mgodi wa Bulumbaka  Novemba 23, 2020 katika Kijiji cha Gasuma wilayani Bariadi.

 

Mchimbaji mdogo, Bw. Wibelo Kihalata akichangia hoja katika kikao cha Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Dkt. Simon Msanjila na baadhi ya viongozi wa Wilaya ya Bariadi, Mkoa wa Simiyu, baadhi ya wachimbaji wadogo, wamiliki wa mashamba katika eneo la mgodi wa Bulumbaka  Novemba 23, 2020 katika Kijiji cha Gasuma wilayani Bariadi.

Baadhi ya wananchi wakimsikilza Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Prof. Simon Msanjila katika kikao chake na baadhi ya viongozi wa Wilaya ya Bariadi, Mkoa wa Simiyu, baadhi ya wachimbaji wadogo, wamiliki wa mashamba katika eneo la mgodi wa Bulumbaka  Novemba 23, 2020 katika Kijiji cha Gasuma wilayani Bariadi.

Afisa Madini Mkazi wa mkoa wa Simiyu, akiwasilisha taarifa katika kikao cha ndani cha   Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Prof. Simon Msanjila na baadhi ya viongozi wa Wilaya ya Bariadi, Mkoa wa Simiyu, kwa lengo la kujadili uendeshaji wa machimbo madogo ya  Bulumbaka  Novemba 23, 2020 katika Kijiji cha Gasuma wilayani Bariadi.

 

Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bibi. Miriam Mmbaga akiagana na baadhi ya wananchi baada ya kikao cha Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Dkt. Simon Msanjila na baadhi ya viongozi wa Wilaya ya Bariadi, Mkoa wa Simiyu, baadhi ya wachimbaji wadogo, wamiliki wa mashamba katika eneo la mgodi wa Bulumbaka  Novemba 23, 2020 katika Kijiji cha Gasuma wilayani Bariadi

Baadhi ya wananchi wakimsikilza Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Prof. Simon Msanjila katika kikao chake na baadhi ya viongozi wa Wilaya ya Bariadi, Mkoa wa Simiyu, baadhi ya wachimbaji wadogo, wamiliki wa mashamba katika eneo la mgodi wa Bulumbaka  Novemba 23, 2020 katika Kijiji cha Gasuma wilayani Bariadi.

Afisa Madini Mkazi wa mkoa wa Simiyu, akiwasilisha taarifa katika kikao cha ndani cha   Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Prof. Simon Msanjila na baadhi ya viongozi wa Wilaya ya Bariadi, Mkoa wa Simiyu, kwa lengo la kujadili uendeshaji wa machimbo madogo ya  Bulumbaka  Novemba 23, 2020 katika Kijiji cha Gasuma wilayani Bariadi.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bibi. Miriam Mmbaga akiagana na baadhi ya wananchi baada ya kikao cha Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Dkt. Simon Msanjila na baadhi ya viongozi wa Wilaya ya Bariadi, Mkoa wa Simiyu, baadhi ya wachimbaji wadogo, wamiliki wa mashamba katika eneo la mgodi wa Bulumbaka  Novemba 23, 2020 katika Kijiji cha Gasuma wilayani Bariadi.

Baadhi ya wananchi wakimsikilza Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Prof. Simon Msanjila katika kikao chake na baadhi ya viongozi wa Wilaya ya Bariadi, Mkoa wa Simiyu, baadhi ya wachimbaji wadogo, wamiliki wa mashamba katika eneo la mgodi wa Bulumbaka  Novemba 23, 2020 katika Kijiji cha Gasuma wilayani Bariadi.

Baadhi ya viongozi wakifuatilia kikao  cha Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Dkt. Simon Msanjila na baadhi ya viongozi wa Wilaya ya Bariadi, Mkoa wa Simiyu, baadhi ya wachimbaji wadogo, wamiliki wa mashamba katika eneo la mgodi wa Bulumbaka  Novemba 23, 2020 katika Kijiji cha Gasuma wilayani Bariadi.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Prof. Simon Msanjila akizungumza na baadhi ya viongozi wa Wilaya ya Bariadi, Mkoa wa Simiyu katika kikao cha ndani kwa lengo la kujadili uendeshaji wa machimbo madogo ya  Bulumbaka  Novemba 23, 2020 katika Kijiji cha Gasuma wilayani Bariadi.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!