Sunday, November 15, 2020

WATANZANIA TUMUUNGE MKONO JPM KULINDA HIFADHI ZA TAIFA: KIKWETE

Rais Mstaafu wa Tanzania awamu ya nne, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ametoa wito kwa Watanzania kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli katika ulinzi wa hifadhi za Taifa ni pamoja na kutoruhusu mifugo kuchungiwa kwenye hifadhi ili hifadhi hizo endelevu kwa manufaa ya Taifa na vizazi vijavyo. 

Dkt. Kikwete ameyasema hayo wakati akizungumza na wananchi wa mikoa ya Simiyu,  Mara pamoja na washiriki wa Mbio za Serengeti Safari Marathon kutoka mikoa mbalimbali nchini na wengine kutoka nje ya nchi na nje ya bara la Afrika zilizofanyika katika hifadhi ya Taifa ya Serengeti kupitia lango la Ndabaka.

“Mikoa miwili ya  Simiyu na Mara tu ina ng’ombe zaidi ya milioni tano, tukisema turuhusu mifugo ichungiwe kwenye hifadhi hakuna mnyama atakayebaki na hapo hakutakuwa na hifadhi tena hili siyo suala la kisiasa; sisi viongozi wa kisiasa tukilipigia siasa jambo hili hiyo sifa tunayoisema ya Serengeti kuwa  Hifadhi ya kwanza Duniani haitakuwepo baada ya kuruhusu ng’ombe kuingia kwenye hifadhi,” alisema Dkt. Kikwete.

Aidha, Dkt. Kikwete amewapongeza waandaaji wa Serengeti Safari Marathon kwa namna kwa kuanzisha mbio hizo ambazo zao jipya la utalii ambayo ikitangazwa vizuri itatangaza utalii nchini na kuweza kulifikia lengo la serikali la kufikisha watalii 5,000,000 ifikapo 2025 kutoka 1,300,000 wa sasa, huku akitoa wito kwa wadau wa utalii kujenga hoteli kwa ajili ya kuwapokea wageni/watalii.

Baadhi ya washiriki wa mbio za Serengeti Safari Marathon wakiwa katika eneo la kumalizia mbio hizo ambazo zimefanyika Novemba 14, 2020 kupitia lango la Ndabaka katika hifadhi ya Taifa ya Serengeti.

Baadhi ya washiriki wa mbio za Serengeti Safari Marathon wakiwa katika eneo la kumalizia mbio hizo ambazo zimefanyika Novemba 14, 2020 katika hifadhi ya Taifa ya Serengeti kupitia lango la Ndabaka.
Baadhi ya viongozi wa mikoa ya Simiyu na Mara pamoja na baadhi ya washiriki wakiwa katika mbio fupi za kilomita tano katika mashindano ya Serengeti Safari Marathon Novemba 14, 2020 katika hifadhi ya Taifa ya Serengeti kupitia lango la Ndabaka.
Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mhe. Adam Malima akimweleza jambo Rais mstaafu wa Tanzania wa awamu ya nne, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (wa pili kulia) wakati akitembea kuelekea lango la Ndabaka katika Hifadhi ya Tifa ya Serengeti  Novemba 14, 2020 kwa lengo la kufungua mashindano ya mbio za Serengeti Safari Marathon
Rais mstaafu wa Tanzania wa awamu ya nne, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi zawadi mmoja wa washindi wa Serengeti Safari Marathon, Bibi. Josien Vergroesien kutoka nchini Netherland, ambazo zimefanyika Novemba 14, 2020 katika hifadhi ya Taifa ya Serengeti kupitia lango la Ndabaka.

Rais mstaafu wa Tanzania wa awamu ya nne, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na mmoja wa wanafunzi wa shule ya sekondari Anthony Mtaka wilayani Busega aliyeshiriki  mashindano ya mbio za Serengeti Safari Marathon katika hifadhi ya Taifa ya Serengeti kupitia lango la Ndabaka.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (kulia) akifurahia jambo na Rais mstaafu wa Tanzania wa awamu ya nne, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete Novemba 14, 2020  mara baada ya kumpokea katika Hoteli ya Serenity On the Lake wilayani Busega kwa ajili ya kwenda kufungua mashindano ya mbio za Serengeti Safari Marathon.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(katikati) akimweleza jambo Rais mstaafu wa Tanzania wa awamu ya nne, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ( kulia) wakati akitembea kuelekea lango la Ndabaka katika Hifadhi ya Tifa ya Serengeti Novemba 14, 2020 kwa lengo la kufungua mashindano ya mbio za Serengeti Safari Marathon.

Rais mstaafu wa Tanzania wa awamu ya nne, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe. Enock Yakobo mara baada ya kuwasili katika Hoteli ya Serenity On the Lake wilayani Busega kwa ajili ya kwenda kufungua mashindano ya mbio za Serengeti Safari Marathon.
Kikundi cha ngoma kikitoa burudani wakati wa mashindano ya mbio za Serengeti Safari Marathon yaliyofanyika katika hifadhi ya Taifa ya Serengeti kupitia lango la Ndabaka.
Baadhi ya washiriki wa Mbio za Serengeti Safari Marathon wakiwa katika eneo la kumalizia mbio hizo ambazo  katika hifadhi ya Taifa ya Serengeti kupitia lango la Ndabaka.
Rais mstaafu wa Tanzania wa awamu ya nne, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (wa nane kulia) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi na watumishi wa mkoa wa Simiyu mara baada ya kufunga mashindano ya mbio za Serengeti Safari Marathon yaliyofanyika katika hifadhi ya Taifa ya Serengeti kupitia lango la Ndabaka.

Rais mstaafu wa Tanzania wa awamu ya nne, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (wa nne kulia) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa Simiyu mara baada ya kuwasili katika Hoteli ya Serenity On the Lake wilayani Busega kwa ajili ya kwenda kufungua mashindano ya mbio za Serengeti Safari Marathon.

Baadhi ya wananchi wakifuatilia hotuba ya Rais mstaafu wa Tanzania wa awamu ya nne, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete wakati wa kufunga mashindano ya Mbio za Serengeti Safari Marathon ambazo  zimefanyika katika hifadhi ya Taifa ya Serengeti kupitia lango la Ndabaka.
Rais mstaafu wa Tanzania wa awamu ya nne, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi zawadi mmoja wa washindi wa Serengeti Safari Marathon ambazo zimefanyika Novemba 14, 2020 katika hifadhi ya Taifa ya Serengeti kupitia lango la Ndabaka.
Rais mstaafu wa Tanzania wa awamu ya nne, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimvisha medali mmoja wa washindi wa Serengeti Safari Marathon ambazo zimefanyika Novemba 14, 2020 katika hifadhi ya Taifa ya Serengeti kupitia lango la Ndabaka.
Rais mstaafu wa Tanzania wa awamu ya nne, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimvisha medali mmoja wa washindi wa Serengeti Safari Marathon ambazo zimefanyika Novemba 14, 2020 katika hifadhi ya Taifa ya Serengeti kupitia lango la Ndabaka.
Rais mstaafu wa Tanzania wa awamu ya nne, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (wa nne kulia) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Kamati ya siasa ya mkoa wa Simiyu (CCM) mara baada ya kuwasili katika Hoteli ya Serenity On the Lake wilayani Busega, Novemba 14, 2020  kwa ajili ya kwenda kufungua mashindano ya mbio za Serengeti Safari Marathon.
Rais mstaafu wa Tanzania wa awamu ya nne, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (wa nne kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa mkoa wa Simiyu, Mkoa wa Mara, UNDP na waandaaji wa Serengeti Safari Marathon baada ya kufunga  mbio hizo Novemba 14, 2020 katika hifadhi ya Serengeti lango la Ndabaka.
Mmoja wa Wakurugenzi wa Serengeti Safari Marathon Henri Kimambo akiwasilisha taarifa ya mbio za Serengeti Safari  Marathon zilizofanyika Novemba 14, 2020 katika hifadhi ya Serengeti lango la Ndabaka.
Rais mstaafu wa Tanzania wa awamu ya nne, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (wa nne kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa mkoa wa Simiyu, Mkoa wa Mara, UNDP na waandaaji waSerengeti Safari Marathon baada ya kufunga  mbio hizo Novemba 14, 2020 katika hifadhi ya Serengeti lango la Ndabaka.
Baadhi ya viongozi wa mikoa ya Simiyu na Mara pamoja na baadhi ya washiriki wakiwa katika mbio fupi za kilomita tano katika mashindano ya Serengeti Safari Marathon Novemba 14, 2020 katika hifadhi ya Taifa ya Serengeti kupitia lango la Ndabaka.
Mjasiriamali kutoka Busega Mkoani Simiyu akimkabidhi zawadi Rais mstaafu wa Tanzania wa awamu ya nne, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete baada ya kufunga mashindano ya mbio hizo ambazo  zimefanyika katika hifadhi ya Taifa ya Serengeti kupitia lango la Ndabaka.
Rais mstaafu wa Tanzania wa awamu ya nne, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi zawadi mmoja wa washindi wa Serengeti Safari Marathon ambazo zimefanyika Novemba 14, 2020 katika hifadhi ya Taifa ya Serengeti kupitia lango la Ndabaka.
Kutoka kushoto Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mhe. Adam Malima, Rais mstaafu wa Tanzania wa awamu ya nne, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka wakifuatilia matukio mbalimbali katika ufungaji wa mbio za Serengeti Safari Marathon ambazo  zimefanyika Novemba 14, 2020 katika hifadhi ya Taifa ya Serengeti kupitia lango la Ndabaka.
Rais mstaafu wa Tanzania wa awamu ya nne, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na baadhi ya wananchi wa mikoa ya Simiyu na Mara, washiriki wa mbio za Serengeti Safari Marathon ambazo  zimefanyika Novemba 14, 2020 katika hifadhi ya Taifa ya Serengeti kupitia lango la Ndabaka.







0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!