Thursday, November 26, 2020

ZAIDI YA WATU 300 KUSHIRIKI MASHINDANO YA BAISKELI, MBIO FUPI NA NGOMA ZA ASILI SIMIYU

 

Zaidi ya wanamichezo 300 kutoka mikoa mbalimbali hapa nchini wanatarajia kushiriki Tamasha la Simiyu Jambo Festival ambalo litahusisha mashindano ya mbio za baiskeli, ngoma za asili(wagika na wagalu), mbio fupi (kilometa kumi) pamoja na mashindano ya kitaaluma kwa wanafunzi wa shule za sekondari. 

Hayo yamebainishwa na Mratibu wa Tamasha la Simiyu Jambo Festival Bi. Zena Mchujuko wakati akizungumza na waandishi wa habari Mjini Bariadi  leo Novemba 26, 2020 juu ya tamasha hilo linalotarajiwa kufanyika Novemba 28, 2020 katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi. 

“Zawadi zitatolewa kwa mshindi wa kwanza mpaka wa kumi wanawake na wanaume (mbio za baiskeli), walemavu zitatolewa kwa mshindi wa kwanza mpaka wa tano; mbio fupi tutatoa kwa mshindi wa kwanza mpaka wa tatu,” alisema Bibi. Mchujuko.

Afisa Miradi kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu Duniani (UNFPA) ambalo ndiyo mdhamini Mkuu wa Simiyu Jambo Festival,  Bw. Dennis Swai amesema shirika hilo limeamua kudhamini tamasha hilo kwa kuwa ni fursa mojawapo ya kuiweza jamii kutambua haki za watoto wa kike na wanawake katika kufikia malengo yao,  huku akiahidi kuwa wataendelea kushirikiana na Serikali kama wadau wa maendeleo.

Kaimu Katibu wa Chama cha Riadha Mkoa wa Simiyu, Bw. Mbezi Ally amesema chama hicho kimeandaa washiriki ambao ni wazuri katika mbio,  ambapo amebainisha kuwa baadhi yao wameshiriki mbio ndefu (kilomita 21 na Kilomita 42) ikiwemo Serengeti Safari Marathon na kutoa wito kwa washiriki kutoka maeneo yote ndani na nje ya mkoa kushiriki mashindano haya.

Mwakilishi wa Mwenyekiti wa Mbio za Baiskeli Mkoa wa Simiyu, Bw. Buyaga George amesema pamoja na washiriki kutoka mkoa wa Simiyu, washiriki kutoka mikoa ya Shinyanga, Mwanza, Tabora na Arusha wamethibitisha kushiriki mashindano ya mbio za baiskeli kwa wanaume (Kilomita 140) ,wanawake (kilomita 80) na walemavu (kilomita tano).

Katibu Tawala wa mkoa wa Simiyu, Bibi. Miriam Mmbaga amesema mkoa wa Simiyu ni maarufu kwa kutumia baiskeli kama nyenzo ya usafiri hivyo mkoa umeona haja ya kuwaendeleza wana Simiyu kwa utamaduni wao wa kutumia baiskeli ili waitumie fursa hiyo kuingia katika mashindano yanayoweza kuwafanya wawe waendeshaji bora wa baiskeli.

Aidha, Mmbaga ametoa wito kwa wadau na wafanyabiashara mkoani hapa kushiriki katika tamasha hili kwa namna mbalimbali ikiwa ni pamoja na kulitumia kutangaza huduma na bidhaa zinazopatikana Simiyu.

Tamasha hili la Simiyu Festival linafanyika kwa mara ya tatu sasa likiwa na Kauli Mbiu, “WAWEZESHE WANAWAKE NA WATOTO WA KIKE ILI KUWA NA DUNIA BORA” chini ya udhamini wa UNFPA, Jambo Food Products, Alliance Ginnery Ltd, Busega Mazao na SweetDreams Hotel,  Mgeni rasmi akitarajiwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka.

MWISHO

Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bibi. Miriam Mmbaga( wa pili kulia) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani)  katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mjini Bariadi  leo Novemba 26, 2020 juu ya Tamasha la Simiyu Jambo Festival linalotarajiwa kufanyika Novemba 28, 2020 katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi.

Mratibu wa Tamasha la Simiyu Jambo Festival , Bibi Zena Mchujuko (wa tatu kushoto) akitoa taarifa ya hali ya maandalizi ya tamasha hilo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mjini Bariadi  leo Novemba 26, 2020  linalotarajiwa kufanyika Novemba 28, 2020 katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi.
Afisa Miradi kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu Duniani (UNFPA) mkoa wa Simiyu ambalo ndiyo mdhamini Mkuu wa Simiyu Jambo Festival,   Bw. Dennis Swai (wa pili kulia) akizungumza kwenye Mkutano na  waandishi wa habari katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mjini Bariadi  leo Novemba 26, 2020 juu ya Tamasha hilo linalotarajiwa kufanyika Novemba 28, 2020 katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi.

Mwakilishi wa Mwenyekiti wa Mbio za Baiskeli Mkoa wa Simiyu, Bw. Buyaga George(wa pili kushoto)  akizungumza kwenye Mkutano na  waandishi wa habari katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mjini Bariadi  leo Novemba 26, 2020 juu ya mashindano ya mbio za baiskeli katika Tamasha la Simiyu Jambo Festival linalotarajiwa kufanyika Novemba 28, 2020 katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi.

Mratibu wa Tamasha la Simiyu Jambo Festival , Bibi Zena Mchujuko (wa pili kushoto) akitoa taarifa ya hali ya maandalizi ya tamasha hilo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mjini Bariadi  leo Novemba 26, 2020  linalotarajiwa kufanyika Novemba 28, 2020 katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi.

Kaimu Katibu wa Chama cha Riadha Mkoa wa Simiyu, Bw. Mbezi Ally (wa pili kushoto) akizungumza kwenye Mkutano na  waandishi wa habari(hawapo pichani)  katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mjini Bariadi  leo Novemba 26, 2020 juu ya mashindano ya mbio fupi katika Tamasha la Simiyu Jambo Festival linalotarajiwa kufanyika Novemba 28, 2020 katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi.

Bango lenye taarifa muhimu za Tamasha la Simiyu Jambo Festival

 

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!