Tuesday, February 20, 2018

MAKAMU WA RAIS APONGEZA VIONGOZI MKOANI SIMIYU KUTEKELEZA SERA YA VIWANDA KWA VITENDO


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan amewapongeza viongozi wa Mkoa wa Simiyu kwa kuunga mkono jitihada za Serikali  hususani katika utekelezaji wa Sera ya Tanzania ya Viwanda.


Mhe.Makamu wa Rais ametoa pongezi hizo wakati akizungumza na Wananchi wa Mji wa Bariadi kwenye Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa CCM Mkoa wa Simiyu.

Amesema amepokea taarifa kuwa Mkoa wa Simiyu una jumla ya viwanda 14 vya kuchakata pamba na viwanda vidogo vya kuongeza thamani ya mazao 1035,  jambo ambalo ni maendeleo makubwa kwa wananchi na akatoa wito kwa wananchi wa Simiyu kuendelea kuwekeza katika maeneo mbalimbali na kuwataka kuwapokea wawekezaji kutoka maeneo mengine ndani na nje ya nchi.

Aidha, amepongeza utekelezaji wa mkakati wa “Wilaya Moja Bidhaa Moja” ambao amesema ni mkakati mzuri unaoupambambanua Mkoa wa  Simiyu katika Sekta ya Viwanda.

“Nimeelezwa hapa na Mkuu wa Mkoa kuwa mmeanza kwa kila wilaya moja kuwa na bidhaa moja(kiwanda kimoja) lakini haikatazwi wilaya hiyo kuwa na viwanda vidogo, nimeelezwa kuwa Meatu mmeamua kusindika maziwa na Maswa kiwanda cha chaki, Bariadi kiwanda cha bidhaa za afya zitokanazo na pamba na hiki ni kiwanda changu ninacho kisimamia” alisema

“Nataka kuahidi kuwa kiwanda hiki kitajengwa na kitazalisha bidhaa za sekta ya Afya, Busega pia kitajengwa kiwanda cha maji tunayotundikiwa hospitali(IV Infussion/drip), Itilima nimeambiwa ni masuala ya asali na alizeti, lakini pia nimeambiwa kuna viwanda vya bidhaa za ngozi maeneo tofauti nawapongeza sana kwa mwamko mkubwa huu” alisisitiza Makamu wa Rais.

Wakati huo huo Mhe.Makamu wa Rais amewapongeza viongozi wa Mkoa na Halmashauri ya Mji Bariadi kwa kusimamia na kuhakikisha barabara za Mjini Bariadi zinajengwa kwa kiwango kinachoridhisha, hivyo amesisitiza usafi  uimarishwe katika barabara hizo hususani barabara iliyopewa jina lake  ili kupendezesha Mji.

Katika hatua nyingine Mhe.Makamu wa Rais amewahakikishia wananchi wa Mkoa wa Simiyu upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama ifikapo mwaka 2019/2020, kupitia Mradi mkubwa wa Maji kutoka Ziwa Victoria ambao unatekelezwa na Wizara iliyo chini ya Ofisi yake kwa kushrikiana na Wizara ya Maji.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka amesema tarehe 21/02/2017Mhe. Makamu wa Rais atakutana na timu ya wataalam wanaofanya upembuzi yakinifu wa ujenzi wa Kiwanda cha bidhaa za afya zitokanazo na pamba mkoani humo,  ambapo alibainisha kuwa mkoa umejipambanua kwenye sekta ya viwanda hasa katika kutekeleza maono na mtazamo wa Viongozi wakuu wa Kitaifa.

Mbunge wa Bariadi Andrew Chenge akawasilisha changamoto za wananchi kwa Makamu wa Rais amesema wananchi Bariadi wanakabiliwa  na uvamizi wa tembo katika mashamba yao ,  hivyo ni vema ikawekwa mipaka na zikatafutwa njia ya kuwazuia, jambo ambalo Mhe. Makamu alilitolea ufafanuzi kuwa Serikali italifanyia kazi kuhakikisha wanyama hao hawawadhuru watu na kuharibu mazao.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe.Samia Suluhu Hassan akiwa katika ziara yake wilayani Bariadi ameweka Jiwe la Msingi Ujenzi wa Nyumba za Viongozi wa Mkoa wa Simiyu, amekagua ujenzi wa barabara za Bariadi Mjini na kufungua barabara moja iliyopewa jina lake”BARABARA YA SAMIA SULUHU”.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , Mhe.Samia Suluhu Hassan(kulia) akifungua moja ya barabara za Mji wa Bariadi iliyopewa jina lake “SAMIA SULUHU AVENUE” wakati wa ziara yake katika Wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , Mhe.Samia Suluhu Hassan akifungua moja ya barabara za Mji wa Bariadi iliyopewa jina lake “SAMIA SULUHU AVENUE” wakati wa ziara yake katika Wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan akipanda mti wa kumbukumbu katika barabara iliyopewa jina lake “BARABARA YA SAMIA SULUHU” Mjini Bariadi, wakati wa ziara yake katika Wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan (katikati) na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe.Anthony Mtaka(mwenye suti kulia) wakifurahia jambo na baadhi ya wananchi waliofika kushuhudia akifungua barabara iliyopewa jina lake “BARABARA YA SAMIA SULUHU” Mjini Bariadi wakati wa ziara yake katika Wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu.
Mbunge wa Jimbo  la Bariadi, Mhe.Andrew Chenge akizungumza kwa niaba ya wananchi wa Bariadi katika Mkutano wa Hadhara uliofanyika Uwanja wa CCM Mkoa wa Simiyu, wakati wa ziara ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Samia Suluhu Hassan  mkoani humo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi wa Bariadi (hawapo pichani) katika Mkutano wa Hadhara uliofanyika Uwanja wa CCM Mkoa wa Simiyu, wakati wa ziara yake mkoani humo.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Samia Suluhu Hassan akiwaaga wananchi wa Bariadi Mjini mara baada ya kumaliza Mkutano wa Hadhara uliofanyika Uwanja wa CCM Mkoa wa Simiyu, wakati wa ziara yake mkoani humo.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka akipanda mti wa kumbukumbu katika  ya “BARABARA YA SAMIA SULUHU” Mjini Bariadi, ambayo imefunguliwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Samia Suluhu Hassan wakati wa ziara yake katika Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu.
Wabunge wa Viti Maalum kupitia CCM Mhe.  Esther Midimu(wa sita kulia) na Leah Komanya (anayefuata) wakicheza pamoja na  Kwaya ya Walimu Bariadi katika Mkutano wa Hadhara uliofanyika Uwanja wa CCM Mkoa wa Simiyu, wakati wa ziara ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Samia Suluhu Hassan mkoani humo.
Kwaya ya AICT Bariadi ikitoa burudani ya wimbo kwa wananchi na viongozi kabla ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Samia Suluhu Hassan kuzungumza na wananchi katika Mkutano wa Hadhara uliofanyika Uwanja wa CCM Mkoa wa Simiyu, wakati wa ziara yake mkoani humo


0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!