Friday, March 15, 2019

RC MTAKA ATOA WITO KWA JAMII KUSHIRIKI VITA DHIDI YA MIMBA KWA WANAFUNZI

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ametoa wito kwa wazazi, walimu na watumishi wengine wa Serikali, wanafunzi wa kike wanaopata mimba na jamii yote kwa ujumla kushirikiana na Serikali kuhakikisha wale wote waliowapa mimba wanafunzi wanabainika na kuchukuliwa hatua za kisheria.


Mtaka ameyasema hayo wakati akifunga kikao kazi cha viongozi na watendaji wa idara ya elimu kilichofanyika Machi 12, 2019 Mjini Bariadi kwa lengo la kuweka mikakati ya kuimarisha taaluma mkoa wa Simiyu.

Amesema katika uchunguzi wa awali uliofanyika imebainika kuwa wazazi, walimu, Maafisa Watendaji wa Kata na watumishi wengine wa Serikali na wanafunzi wenyewe waliopewa mimba wamekuwa wakikwamisha juhudi za serikali katika vita hii kwa kuwa sehemu ya kuharibu ushahidi.

“Kuna mimba zaidi ya 300 zimripotiwa katika maeneo mbalimbali baadhi ya maeneo wazazi wanashiriki kuharibu na wakati mwingine wanafunzi waliopata mimba wanashirikina na wazazi kuharibu ushahidi wa kesi wasi za wanafunzi wajawazito, baadhi ya maeneo walimu wetu wamehisiwa, kwingine watendaji wetu, naomba tushirikiane kuwabaini watu wanaowapa wanafunzi mimba kwenda  kwenye hatua” alisema Mtaka.

Ameongeza kuwa Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa imekaa na wameshakubaliana hatua za kuchukua kwa wanafunzi, watumishi, wazazi na watu wote waliokatisha ndoto za wanafunzi wa kike kwa kuwapa mimba.

Kwa  upande wake Mwalimu  Huruma Mjinja kutoka Shule ya Sekondari Kidinda, amesema katika kukabiliana na tatizo la mimba kwa wanafunzi ni vema walimu na wazazi wakashirikiana kuwalinda watoto wa kike na wapate muda wa kuzungumza nao.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe, Anthony Mtaka amesema Wanafuzi wa kidato cha sita mkoani hapa wanatarajia kuanza kambi za kitaaluma rasmi Machi 31, 2019 kwa ajili ya kujiandaa na mtihani wa Taifa.

Aidha, Mtaka amewataka Wakuu wa shule za sekondari zenye wanafunzi wa kidato cha nne chini ya 25 kukutana na wazazi ili wakae na kukubaliana baadaye  kuwakusanya wanafunzi hao kwa pamoja katika Shule ya sekondari Simiyu kwa ajili ya kufanya kambi za kitaaluma.

“Tunamaliza kujenga Simiyu Sekondari tukiwa na ziada ya vyumba vya madarasa 20 hivyo wakikaa watu 40 kwa kila chumba ni wanafunzi 800 tunajenga mabweni manne; shule zote za sekondari zenye wanafunzi wa kidato cha nne chini ya 25, bodi zao na viongozi wa Serikali wakae pamoja shuleni hapo kwa ajili ya kambi za kitaaluma baada ya likizo ya MweziAprili, 2019” alisema Mtaka.

Nao Baadhi ya Wakuu waShule wameahidi kufanya kazi kwa bidii na kuhakikisha wanafanya vizuri ili mkoa uweze kufanya vizuri pia kitaaluma huku akiomba viongozi wa mkoa waendelee kutoa motisha kwa walimu na wanafunzi wanaofanya vvizuri ili waweze kufanya vizuri zaidi kila mwaka.

“ Tutafanya jitihada kuhakikisha tunafanya vizuri lakini tunaomba viongozi wetu waendelee kuona haja ya kutoa motisha kwa wanaofanya vizuri kwa sababu mkiendelea kufanya hivyo mtatupa nguvu ya kufanya vizuri zaidi” Mwalimu Enelico Mwandibila kutoka wilaya ya Itilima.

Kwa upande wake Afisa Elimu Mkoa wa Simiyu, Mwl. Ernest Hinju amesema mkoa huo umejiweka mkakati kabambe wa kuimarisha ufuatiliaji na ufundishaji na tathmini itafanyika kila mwezi kujua vipindi vilivyofundishwa na ambavyo havijafundishwa vitafidiwa.

Kikao hiki kimehudhuriwa na Maafisa Elimu na Taaluma wa Mkoa na Wilaya, baadhi ya Waratibu Elimu Kata, Wakuu wa Shule za Sekondari za Kidato cha Nne, wadhibiti ubora na baadhi ya wadau wa elimu mkoani Simiyu.
MWISHO.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka(mwenye suti katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi wa kike wa Shule ya Sekondari Bariadi, mara baada ya kufunga kikao kazi cha viongozi na watendaji wa idara ya elimu kilichofanyika shuleni hapo Machi 12, 2019 kwa lengo la kuweka mikakati ya kuimarisha taaluma mkoani Simiyu.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka akizungumza na viongozi na watendaji wa idara ya elimu katika kikao kazi kilichofanyika Machi 12, 2019 Mjini Bariadi kwa lengo la kuweka mikakati ya kuimarisha taaluma mkoani Simiyu.
Baadhi ya viongozi na watendaji wa idara ya elimu mkoa wa Simiyu wakiwa katika kikao kazi kilichofanyika Machi 12, 2019 Mjini Bariadi kwa lengo la kuweka mikakati ya kuimarisha taaluma mkoani Simiyu.
Mmoja wa Viongozi wa Elimu mkoani Simiyu akichangia hoja katika kikao kazi cha viongozi na watendaji wa idara ya elimu kilichofanyika Machi 12, 2019 Mjini Bariadi kwa lengo la kuweka mikakati ya kuimarisha taaluma mkoani Simiyu.
Ibrahimu Buyungumya mwanafunzi bora wa Mkoa wa Simiyu katika Mtihani wa Kidato cha Nne mwaka 2018 kutoka Shule ya Sekondari Nkololo wilayani Bariadi, akionesha kiasi cha fedha alichopewa na baadhi ya wadau wa elimu mkoani Simiyu kama pongezi, katika kikao kazi cha viongozi na watendaji wa idara ya elimu kilichofanyika Machi 12, 2019 Mjini Bariadi kwa lengo la kuweka mikakati ya kuimarisha taaluma mkoani Simiyu.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka akizungumza na viongozi na watendaji wa idara ya elimu katika kikao kazi kilichofanyika Machi 12, 2019 Mjini Bariadi kwa lengo la kuweka mikakati ya kuimarisha taaluma mkoani Simiyu, (kushoto) Afisa Elimu Mkoa, Mwl Ernest Hinju.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka(mwenye suti katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi wa kike wa Shule ya Sekondari Bariadi, mara baada ya kufunga kikao kazi cha viongozi na watendaji wa idara ya elimu kilichofanyika shuleni hapo Machi 12, 2019 kwa lengo la kuweka mikakati ya kuimarisha taaluma mkoani Simiyu.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka(mwenye suti katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi wa kike wa Shule ya Sekondari Bariadi, mara baada ya kufunga kikao kazi cha viongozi na watendaji wa idara ya elimu kilichofanyika shuleni hapo Machi 12, 2019 kwa lengo la kuweka mikakati ya kuimarisha taaluma mkoani Simiyu.



0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!