Wednesday, May 29, 2019

KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE WA UHURU MWAKA 2019 AWEKA JIWE LA MSINGI SHULE YA DKT. BALELE MAJAHIDA



Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2019,  Ndg. Mzee Mkongea Ali akiweka jiwe la msingi katika Madarasa sita ya Shule ya Sekondari tarajiwa ya Dkt. Yohana Balele iliyopo Majahida Mjini Bariadi,wakati wa mbio za mwenge wa uhuru mjini Bariadi Mei 25, 2019.



Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2019,  Ndg. Mzee Mkongea Ali ameweka Jiwe la Msingi katika Madarasa sita ya Shule ya Sekondari tarajiwa ya Dkt. Yohana Balele iliyopo Majahida Mjini Bariadi, ambayo kikamilika kwake kutawapunguzia wanafunzi wa Kata ya Isanga kutembea Mwendo mrefu ambapo sasa wanasoma katika Shule za Sekondari Biashara Kata ya Sima na Kidinda Kata ya Bariadi.


Awali akitoa taarifa kwa kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru, Ndg. Mzee Mkongea Ali, Mwenyekiti wa Mtaa wa Majahida, Ndimi Silanga amesema vyumba hivyo vimejengwa kwa gahrama ya shilingi milioni 97 ikiwa ni michango ya wananchi, wadau mbalimbali wa elimu pamoja na Mbunge wa Jimbo la Bariadi, Mhe. Andrew Chenge.  

Kwa upannde wake Elizabeth Jailo ambaye ni mkazi wa Majahida na mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Biashara amesema kujengwa kwa shule hiyo kutasaidia kupunguza changamoto ya upungufu wa madarasa katika shule anayosoma maana wanafunzi wa shule hiyo wanaotoka karibu na Shule mpya watasoma hapo na kupunguziwa adha ya kutembea takribani kilometa 15 kwa siku.

Pamoja na kuweka Jiwe la Msingi Madarasa hayo, Mwenge wa Uhuru umepitia miradi mbalimbali ikiwepo kufungua Nyumba ya Kulala wageni Nghunde Classic Lodge, kuona mradi wa Uhifadhi wa Mazingira wa Msitu wa Kanisa Katoliki Old Maswa Sesele.

Aidha,umefungua jengo la Wodi ya Wazazi Zahanati ya Mwakibuga na kuona shughuli za wanawake Wajasiriamali pamoja na kuzindua klabu ya kupinga rushwa na klabu ya kupinga matumizi ya dawa za kulevya shule ya Sekondari Kusekwa.
MWISHO


Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2019,  Ndg. Mzee Mkongea Ali akiweka jiwe la msingi katika Madarasa sita ya Shule ya Sekondari tarajiwa ya Dkt. Yohana Balele iliyopo Majahida Mjini Bariadi,wakati wa mbio za mwenge wa uhuru mjini Bariadi Mei 25, 2019.


Baadhi ya wananchi wa Kata ya Isanga wakishuhidia uwekaji wa jiwe la msingi katika Madarasa sita ya Shule ya Sekondari tarajiwa ya Dkt. Yohana Balele iliyopo Majahida Mjini Bariadi,wakati wa mbio za mwenge wa uhuru mjini Bariadi Mei 25, 2019.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2019,  Ndg. Mzee Mkongea Ali akikagua moja ya vyumba sita vya madarasa Shule ya Sekondari tarajiwa ya Dkt. Yohana Balele iliyopo Majahida Mjini Bariadi,wakati wa mbio za mwenge wa uhuru mjini Bariadi Mei 25, 2019.
Wakimbiza Mwenge wa Uhuru na askari wa FFU wakiondoka baada ya kufungua Nyumba ya Kulala wageni Nghunde Classic Lodge wakati wa mbio za mwenge wa uhuru mjini Bariadi Mei 25, 2019.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2019,  Ndg. Mzee Mkongea Ali akizindua Jengo la Wodi ya wazazi katika Zahanati ya Mwakibuga, wakati wa mbio za mwenge wa uhuru mjini Bariadi Mei 25, 2019.

Jengo la Wodi ya wazazi katika Zahanati ya Mwakibuga lililozinduliwa wakati wa mbio za mwenge wa uhuru mjini Bariadi Mei 25, 2019.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2019,  Ndg. Mzee Mkongea Ali akipewa maelezo kuhusu namna hifadhiya msitu wa Sesele inavyotunzwa, wakati wa mbio za mwenge wa uhuru mjini Bariadi Mei 25, 2019.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2019,  Ndg. Mzee Mkongea Ali akipewa maelezo na mwenyekiti wa Klabu ya wapinga rushwa katika Shule ya Sekondari Kusekwa, wakati wa mbio za mwenge wa uhuru mjini Bariadi Mei 25, 2019.


0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!