Saturday, May 25, 2019

MWENGE WA UHURU KUPITIA MIRADI 34 YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI 8.8 MKOANI SIMIYU


Mwenge wa Uhuru mwaka 2019 umeanza mbio zake Mei 22, 2019 Mkoani Simiyu ambapo unatarajia kupitia miradi 34 kutoka katika sekta binafsi, maji, elimu, afya, viwanda, kilimo, barabara, maendeleo ya jamii na hifadhi ya mazingira ambayo ina thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 8.8.

Akizungumza mara baada ya kupokea Mwenge wa Uhuru kutoka Mwanza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema katika thamani hiyo ya miradi ambayo ni shilingi 8, 878,598,412.25 shilingi 904,170,725.00 ni nguvu za wananchi, Halmashauri shilingi 428, 403,532.63, Serikali Kuu ni shilingi 5, 992,582,072.37, wahisani shilingi 1,256,475,082.25 na sekta Binafsi shilingi 296,967,000.00

Akizungumzia Ujumbe wa Mwenge wa Uhuru mwaka 2019 “MAJI NA HAKI YA KILA MTU TUTUNZE VYANZO VYAKE NA TUKUMBUKE KUSHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA” Mtaka amesema, wastani wa upatikanaji maji Simiyu ni asilimia 50.4 ambao unahudumia wakazi 817, 968  na kubainisha kuwa Serikali inaendelea kuhamasiha wananchi kulinda vyanzo vya maji ili kuwezesha upatikanaji wa huduma hiyo.

Aidha, amesema Mkoa wa Simiyu umejipanga na unaendelea kuandaa mazingira mazuri ya amani na utulivu, yatakayowezesha wananchi kutumia haki yao ya kidemokrasia kushiriki kikamilifu katika mchakato mzima wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2019.

Kwa upande wake Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2019, Ndg. Mzee Mkongea Ali  amewataka viongozi wa mkoa wa Simiyu na wilaya zote mkoani humo kuhakikisha taarifa zote za miradi ya maendeleobitakayopitiwa na Mwenge wa uhuru ziwepo eneo la mradi na wataalam wote wanaohusika na miradi hiyo wawepo.

Baada ya kupokelewa Mkoani Simiyu Mwenge wa Uhuru umeanza mbio zake wilayani Maswa ambapo umepitia mradi wa urasimishaji wa makazi Malampaka, ukaguzi wa ujenzi wa barabara za lami Mjini Maswa, mradi wa maji Nyashimba, Kiwanda cha viazi lishe Njiapanda, vyumba viwili vya madarasa na ofisi moja Kijiji cha Mwadila.

Aidha, Mwenge wa Uhuru ulitembelea na kuona shughuli za wajasiriamali na kutoa hundi za wajasiriamali, kuzindua klabu za kutokomeza rushwa na dawa za kulevya, kuzindua kampeni ya tokomeza malaria na kukagua shughuli za utoaji elimu ya kuhimiza upimaji wa VVU/UKIMWI.
Mwenge wa Uhuru takimbiza kwa mua wa siku sita mkoani Simiyu Mei 22 mpaka Mei 27, 2019 na Mei 28, 2019 utakabidhiwa mkoani Mara.
MWISHO
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(mwenye fulana nyeupe) akipokea Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. John Mongela katika kijiji cha Jihu wilayani Maswa, Mei 22, 2019.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(mwenye fulana nyeupe) akipokea hati ya makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. John Mongela katika kijiji cha Jihu wilayani Maswa, Mei 22, 2019.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(kulia) akimkabidhi  Mwenge wa Uhuru  Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe. Dkt. Seif Shekalaghe  katika kijiji cha Jihu wilayani Maswa, Mei 22, 2019 ikiwa ndiyo wilaya ya kwanza kuanza Mbio za Mwenge wa Uhuru mkoani Simiyu.
Mhandisi wa Maji wa Wilaya ya Maswa  akitoa maelezo kwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2019, Ndg. Mzee Mkongea Ali kabla ya kuweka jiwe la msingi mradi maji wa Nyashimba katika Kijiji cha Nyashimba wilayani Maswa, Mei 22, 2019.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2019, Ndg. Mzee Mkongea Ali akifungua vyumba viwili vya madarasa na ofisi moja ya mwalimu  Mkuu katika shule ya sekondari Mwadila Mei 22, 2019.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2019, Ndg. Mzee Mkongea Ali akiangali baadhi ya machapisho yanayotumika na wanachama wa Klabu yaMapambano dhidi ya Rushwa katika shule ya sekondari Lalago wilayani Maswa kutoa elimu ya vita dhidi ya rushwa kabla ya kuzindua klabu hiyo, Mei 22, 2019
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2019, Ndg. Mzee Mkongea Ali(wa nne kushoto)  na wakimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa wengine wakiangalia mbegu za  viazi lishe, kabla ya kuweka jiwe la msingi Kiwanda cha kusindika Viazilishe katika Kijiji cha Njiapanda wilayani Maswa, Mei 22, 2019.
Baadhi ya Askari wa Jeshi la Polisi na Vijana wa Skauti mkoani Simiyu wakipita na Mwenge wa uhuru katika moja ya barabara zinazojengwa  kwenye mtandao wa Kilomita 1.5 katika Mji wa Maswa, ambapo mradi huo ulikaguliwa na Mbio za mwenge wa Uhuru Mei 22, 2019.
Mbunge wa Maswa mashariki na Naibu Waziri wa Madini, Mhe. Stanslaus Nyongo akizungumza na wananchi, wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru wilayani Maswa, Mei 22, 2019.
Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Dkt. Seif Shekalaghe akizungumza na wananchi, wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru wilayani Maswa, Mei 22, 2019.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2019, Ndg. Mzee Mkongea Ali(wa pili kulia)  akiwasiliza wanawake wajasiriamali wa wilayani Maswa, wakati alipopita kukagua kazi zinazofanywa na wanawake hao baada ya kuwezeshwa na Halmashauri kuwezeshwa mikopo inayotoka na asilimia nne ya mapato ya ndani, wakati wa mbio za mwenge wa Uhuru wilayani humo Mei 22, 2019.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2019, Ndg. Mzee Mkongea Ali akimkabidhi hati ya kiwanja Mkazi wa Malampaka, Bw. Martini Kamuzora mara baada ya kuzindua zoezi la urasimishaji wa makazi ya wananchi katika Mji wa Malampaka, Mei 22, 2019.
Moja ya mabanda yaliyoandaliwa na Halmashauri ya Wilaya ya Maswa kutoa elimu kwa wananchi juu ya vita dhidi ya dawa za kulevya kupitia Klabu ya kupiga vita dawa za kulevya shule ya sekondari Lalago, wakati wa mbio za Mwenge wa Uhuru wilayani humo Mei 22, 2019.
Wanachama wa Klabu ya kupiga vita dawa za kulevya kutoka shule ya Sekondari Lalago wakitoa maelezo kwa Kiongozi wa mbio za mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2019, Ndg. Mzee Mkongea Ali, kabla ya kuzinduliwa kwa klabu hiyo wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru wilayani humo Mei 22, 2019.
Mkimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Ndg. Latifa Khamis Juwakali akitoa ujumbe wa Mwenge kwa wananchi wa Lalago wilayani Maswa(hawapo pichani), Mei 22, 2019.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2019, Ndg. Mzee Mkongea Ali akizungumza na wanawake wajasiriamali wanaojihusisha na kilimo cha pamba alipokuwa akikagua kazi wanazofanya wanawake hao, wakati wa mbio za Mwenge wa Uhuru wilayani Maswa, Mei 22, 2019.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!