Thursday, July 30, 2020

NMB YATOA MILIONI 42.5 KUCHANGIA MAONESHO YA NANENANE SIMIYU



Benki ya NMB imetoa shilingi milioni 42.5 kwa ajili ya kudhamini Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2020 yatakayofanyika katika kanda ya Ziwa Mashariki  Viwanja vya Nyakabindi Bariadi mkoani Simiyu kuanzia Agosti 01 hadi Agosti 08, 2020.

Akikabidhi mfano wa hundi ya fedha hizo Julai 27, 20202  kwa Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga, Meneja wa NMB Kanda ya Magharibi, Bw. Sospeter Magese amesema pamoja na mchango huo, NMB imetoa fulana 300 ambazo zitatumika katika maonesho hayo.

Bw. Magese amesema NMB imekuwa ikidhamini maonesho haya tangu mwaka wa 2018 yalipoadhimishwa kwa mara kwanza mkoani Simiyu ambapo mpaka sasa benki hiyo  imeshatoa shilingi 100.

“Pamoja na kudhamini maonesho ya nanenane Benki ya NMB imekuwa ifanya kazi na katika maeneo mengi katika sekta ya elimu pamoja na kilimo; katika kilimo ndani ya miaka miwili tumeweza kufungua akaunti 500,000 lakini kati ya hizo akaunti 86,000 ni za wakulima wa pamba wa mkoa wa Simiyu,” alisema Magese.

Akipokea msaada huo kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Mkuu wa mkoa wilaya ya Bariadi, Mku wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga ameishukuru Benki ya NMB kwa namna inavyojitoa kusaidia mambo mbalimbali katika mkoa wa Simiyu ikiwemo katika sekta ya elimu pamoja na kilimo huku akiwahakikishia kuwa serikali iko tayari kushirikiana na benki hiyo kila itakapohitaji.

Katika hatua nyingine Kiswaga ametoa wito kwa wananchi wa mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga na maeneo yote nchini kujitokeza kwa wingi kujionea maonesho ya kilimo nanenaneyanayofanyika Kitaifa katika kanda ya ziwa Mashariki ili kuona fursa mbalimbali pamoja na teknolojia rahisi zinazotumika katika sekta ya kilimo.
MWISHO

 Meneja wa NMB kanda ya magharibi, Bw. Sospeter Magese (kushoto) akikabimkabidhi Mwakilishi wa mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga mfano wa hundi ya shilingi milioni 42.5 kama ikiwa ni mchango wa wa benki hiyo kwa ajili ya maonesho ya Nanenane Kitaifa yatakayofanyika Viwanja vya vya Nyakabindi mkoani hapa. Katikati ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga na Meneja wa NMB Tawi la Bariadi, Bw. Gabriel Paul.
 Meneja wa NMB kanda ya magharibi, Bw. Sospeter Magese (kushoto) akikabimkabidhi Mwakilishi wa mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga mfano wa hundi ya shilingi milioni 42.5 kama ikiwa ni mchango wa wa benki hiyo kwa ajili ya maonesho ya Nanenane Kitaifa yatakayofanyika Viwanja vya vya Nyakabindi mkoani hapa. Katikati ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga na Meneja wa NMB Tawi la Bariadi, Bw. Gabriel Paul.
 Meneja wa NMB kanda ya magharibi, Bw. Sospeter Magese (kushoto) akimkabikabidhi Mwakilishi wa mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga moja ya fulana kama ikiwa ni mchango wa wa benki hiyo kwa ajili ya maonesho ya Nanenane Kitaifa yatakayofanyika Viwanja vya vya Nyakabindi mkoani hapa. Katikati ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga na Meneja wa NMB Tawi la Bariadi, Bw. Gabriel Paul.
 Meneja wa NMB Tawi la Bariadi, Bw. Gabriel Paul akitoa taarifa ya utangulizi kabla ya makabidhiano ya fulana 300 na mfano wa hundi ya shilingi milioni 42.5  kati ya Meneja wa NMB kanda ya magharibi, Bw. Sospeter Magese ( wa pili kushoto)  na Mwakilishi wa mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga(wa tatu kushoto) ikiwa ni mchango wa benki hiyo kwa ajili ya maonesho ya Nanenane Kitaifa yatakayofanyika Viwanja vya vya Nyakabindi mkoani hapa.


Baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Simiyu na viongozi wa NMB baada ya makabidhiano ya fulana 300 na mfano wa hundi ya shilingi milioni 42.5  kati ya Meneja wa NMB kanda ya magharibi, Bw. Sospeter Magese ( wa nne kushoto)  na Mwakilishi wa mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga(wa tano kushoto) ikiwa ni mchango wa benki hiyo kwa ajili ya maonesho ya Nanenane Kitaifa yatakayofanyika Viwanja vya vya Nyakabindi mkoani hapa.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!