Saturday, July 4, 2020

WALIMU WANAMAZINGIRA SIMIYU WATOA VIFAA VYA KUNAWIA MIKONO MASHULENI KWA AJILI YA TAHADHARI YA CORONA

Shirikisho la Walimu wanamazingira mkoa wa Simiyu wametoa msaada wa vifaa vya kunawia mikono ikiwa ni sehemu ya uungaji mkono juhudi za serikali mkoani hapa katika kuchukua tahadhari dhidi ya maambukizi ya Virusi vya Corona.

Vifaa hvyo ambavyo vyenye thamani ya shilingi 167,000/= vimepokelewa na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw.  Donatus Weginah katika viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu mjini Bariadi Julai 03, 2020.

Akikabidhi vifaa hivyo kwa naiaba ya walimu hao Mwenyekiti wa shirikisho hilo, Mwalimu Aron Kiunsi amesema wameguswa kutoa msaada huo kwa viongozi wa mkoa ili wao waweze kupelekea vifaa hivyo kwenye maeneo yenye uhitaji zaidi ikiwa ni pamoja na shule ambazo kwa sasa zimefunguliwa na wanafunzi wana uhitaji wa vifaa hivyo.

Akipokea vifaa hivyo Kaimu  katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Donatus Weginah amewashukuru walimu hao kwa kujitolea kuunga mkono nguvu ya mkoa  katika tahadhari dhidi ya Corona, huku akiendelea kutoa wito kwa wadau wengine kutoa msaada wa vifaa hivyo katika maeneo yenye uhitaji mkubwa ikiwa ni pamoja na shule.

“Ninawashukuru sana walimu kwa kutambua  mahitaji tuliyo nayo katika  kuchulua tahadhari ya Virusi vya Corona na kujitolea sehemu ya vipato vyao kununua vifaa hivi kuunga nguvu ya mkoa, sisi kama watumishi wa ofisi ya mkuu wa mkoa tutahakikisha kuwa vifaa hivi vitapelekwa katika baadhi ya shule za msingi na sekondari ambako kuna uhitaji mkubwa,” alisema Weginah.

Kwa upande wake Afisa Elimu wa Mkoa wa Simiyu, Mwl. Ernest Hinju amesema anawashukuru walimu kwa kuendela kuwa wadau muhimu katika sekta ya elimu kwanza kupitia ufundishaji na pili kupitia uchangiaji huku akieleza kuwa mchango wa vifaa hivyo ambavyo vitasaidia kuwakinga na maradhi mbalimbali ikiwemo maambukizi ya Corona na kusababisha wanafunzi kusoma wakiwa salama.

Naye Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dk. Khamis Kulemba amesema idara ya afya mkoa iko bega kwa began a walimu hao kuhakikisha kuwa wanafunzi wote wanakuwa salama  ambapo ameseitiziza kuwa itasimamia kuhakikisha tahadhari zote dhidi ya ugonjwa wa COVID 19 zinazingatiwa ikiwa ni pamoja na unawaji mikono kwa maji tiririka na sabuni.

“Walimu, viongozi na jamii yote kwa ujumla twendeni tukalinde afya za watoto wetu na kulinda haki hizo ni kuhakikisha zile tahadhari zote zinafuatwa wakati wote wanapokuwa shuleni; msaada mliotoa leo ni mfano wa kuigwa kwa mtu mmoja mmoja, mashirika na taasisi mbalimbali, niwahakikishie tu kuwa tuko pamoja nanyi kuhakikisha Corona ndani ya Simiyu inatokomezwa kabisa,” alisema Dkt. Kulemba.

Naye Katibu wa Itikadi na uenezi wa CCM Simiyu Bw.Mayunga George amewapongeza walimu hao kwa msaada walioutoa kwa ajili ya kuwasaidia watoto kusoma kwa usalama zaidi, huku akiwapongeza pia kwa kazi nzuri wanayoifanya katika kuwafundisha watoto na kuufanya mkoa kuwa katika nafasi nzuri katika ufaulu ambapo amebainisha kuwa ufudishaji wao unaifanya kazi inayofanywa na serikali ya awamu ya tano katika elimu kupitia elimu bila malipo ionekane.
MWISHO

 Mwenyekiti wa shirikisho la walimu wanamazingira wa mkoa wa Simiyu, Mwl. Aron Kiunsi(kushoto) akikabidhi msaada wa vifaa vya kunawia mikono kwa wanafunzi  Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Donatus Weginah (wa pili kulia mbele) na Afisa Elimu wa Mkoa, Ernest Hinju( mwenye shati la kitenge kushoto) na Katibu wa Itikadi na uenezi wa CCM Simiyu Bw.Mayunga George(kulia) wakishuhudia makabidhiano hayo Julai 03, 2020 mjini Bariadi.
 Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Donatus Weginah (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa mkoani hapa na baadhi ya walimu wanamazingira mara baada ya makabidhiano ya vifaa vya kunawia mikono ili kuchukua tahadhari ya maambukizi ya Corona, yaliyofanyika Julai 03, 2020 Mjini Bariadi.
 Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na walimu wanamazingira ofisini kwake mara baada ya walimu hao kukabidhi  vifaa vya kunawia mikono ili kuchukua tahadhari ya maambukizi ya Corona hususani katika shule mbalimbali,  Julai 03, 2020 Mjini Bariadi.

 Mwenyekiti wa shirikisho la walimu wanamazingira wa mkoa wa Simiyu, Mwl. Aron Kiunsi(kushoto) akikabidhi msaada wa vifaa vya kunawia mikono kwa wanafunzi  kwa Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Donatus Weginah (wa pili kulia mbele) na Afisa Elimu wa Mkoa, Ernest Hinju (mwenye shati la kitenge kushoto) na Katibu wa Itikadi na uenezi wa CCM Simiyu Bw. Mayunga George (kulia) wakishuhudia makabidhiano hayo Julai 03, 2020 mjini Bariadi.
 Katibu wa Itikadi na Uenezi mkoa wa Simiyu, Bw. Mayunga George akizungumza jambo na walimu wanamazingira mkoa wa Simiyu kabla ya makabidhiano ya msaada wa vifaa vya kunawia mikono kwa wanafunzi uliotolewa na walimu hao  Julai 03, 2020 kuunga mkono juhudi za serikali katika kuchukua tahadhari dhidi ya maambukizi ya Corona.
                                                      
 Vifaa vilivyotolewa msaada na walimu wanamazingira mkoa wa Simiyu kwa wanafunzi uliotolewa na walimu hao  Julai 03, 2020 kuunga mkono juhudi za serikali katika kuchukua tahadhari dhidi ya maambukizi ya Corona.
 Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akifurahia jambo na walimu wanamazingira mkoa wa Simiyu ofisini kwake mara baada ya walimu hao kukabidhi  vifaa vya kunawia mikono ili kuchukua tahadhari ya maambukizi ya Corona hususani katika shule mbalimbali,  Julai 03, 2020 Mjini Bariadi.
 Mwenyekiti wa shirikisho la walimu wanamazingira wa mkoa wa Simiyu, Mwl. Aron Kiunsi(kushoto) akikabidhi msaada wa vifaa vya kunawia mikono kwa wanafunzi  Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Donatus Weginah (wa pili kulia mbele) na Afisa Elimu wa Mkoa, Ernest Hinju (mwenye shati la kitenge kushoto) na Katibu wa Itikadi na uenezi wa CCM Simiyu Bw. Mayunga George (kulia) wakishuhudia makabidhiano hayo Julai 03, 2020 mjini Bariadi.

 Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akifurahia jambo na walimu wanamazingira mkoa wa Simiyu ofisini kwake mara baada ya walimu hao kukabidhi  vifaa vya kunawia mikono ili kuchukua tahadhari ya maambukizi ya Corona hususani katika shule mbalimbali,  Julai 03, 2020 Mjini Bariadi.
 Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akifurahia jambo na walimu wanamazingira mkoa wa Simiyu ofisini kwake mara baada ya walimu hao kukabidhi  vifaa vya kunawia mikono ili kuchukua tahadhari ya maambukizi ya Corona hususani katika shule mbalimbali,  Julai 03, 2020 Mjini Bariadi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akifurahia jambo na walimu wanamazingira mkoa wa Simiyu ofisini kwake mara baada ya walimu hao kukabidhi  vifaa vya kunawia mikono ili kuchukua tahadhari ya maambukizi ya Corona hususani katika shule mbalimbali,  Julai 03, 2020 Mjini Bariadi.


0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!