Wednesday, July 29, 2020

RC MALIMA: TUNAWAKARIBISHA WANANCHI KUJIONEA NANENANE KITAIFA 2020 YA KIWANGO


Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mhe. Adam Kighoma Malima ametoa wito wananchi wa mikoa ya Simiyu, Mara, Shinyanga na maeneo mengine nchini kafika katika maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2020 yatakayofanyika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Mkoani Simiyu katika Kanda ya Ziwa Mashariki inayoundwa na mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga  ili wajionee maonesho yenye kiwango.

Mhe. Malima ameyasema hayo Juni  27, 2020 katika kikao cha maandalizi ya Maonesho hayo ambayo yatafanyika kitaifa katika kanda hiyo kwa mara ya tatu mfululizo kilichofanyika katika Uwanja wa Maonesho wa nyakabindi Mjini Bariadi Mkoani Simiyu.

“Ingawa maandalizi yetu yaliathiriwa na changamoto ya Corona bado tuna uhakikia wa kufanya vizuri kwani tumepita kuangalia maendeleo ya vipando, vipando viko katika hali nzuri na tunaamini kuwa maonesho haya yatakwenda vizuri kama ilivyo kawaida yetu, hivyo tunawakaribisha wananchi wote kushiriki maonesho haya ambayo yatakuwa ya viwango,” alisema Malima.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Zainab Telack amesema Kanda ya Ziwa Mashariki itafanya vizuri katika maonesho ya kitaifa mwaka 2020 kuliko miaka miwili  ya mwanzo, kwa kuwa pamoja na changamoto zilizojitokeza katika maandalizi kumekuwa na mwamko mkubwa wa ushiriki wa wadau katika maonesho haya.

Katika hatua nyingine Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga amesema wadau mbalimbali zikiwemo taasisi binafsi na za Umma, wananchi wakiwemo wajasiriamali na wafanyabiashara wameonesha mwitikio mkubwa na wanaendelea na maandalizi ambapo alibainisha kuwa katika maonesho ya nanenane mwaka huu washiriki takribani 500 wanatarajiwa kushiriki.

Aidha Bi. Mmbaga ametoa wito kwa wananchi wote nchini hususani wa mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga kuitumia vizuri fursa ya kuwa maonesho haya ya Kitaifa kufanyika katika kanda ya ziwa Mashariki na wajitokeze kwa wingi katika maonesho haya ili waweze kupata kuona mambo mbalimbali yatakayosaidia kuongeza tija kwenye maeneo yao ya uzalishaji

Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2020 yanaongozwa na Kauli Mbiu inayosema “KWA MAENDELEO YA KILIMO MIFUGO NA UVUVI CHAGUA VIONGOZI BORA 2020.”
MWISHO
 Baadhi ya viongozi na wataalam wakitembelea vipando mbalimbali  vya mazao vilivyoandaliwa kwaa jili ya maonesho ya nanenane kabla ya kikao cha maandalizi ya maonesho ya nanenane Kitaifa ambayo yanafanyika katika kanda ya ziwa mashariki inayojumuisha mikoa hiyo mitatu ambayo yatafanyika kwa mara ya tatu mfululizo sasa  katika Uwanja wa NaneNane Nyakabindi jana uwanjani hapo.



 Baadhi ya viongozi na wataalam wakitembelea vipando mbalimbali  vya mazao vilivyoandaliwa kwaa jili ya maonesho ya nanenane kabla ya kikao cha maandalizi ya maonesho ya nanenane Kitaifa ambayo yanafanyika katika kanda ya ziwa mashariki inayojumuisha mikoa hiyo mitatu ambayo yatafanyika kwa mara ya tatu mfululizo sasa  katika Uwanja wa NaneNane Nyakabindi jana uwanjani hapo.



 Mkuu wa mkoa wa Mara, Mhe. Adam Malima akizungumza na viongozi na wataalam kutoka mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga katika kikao cha maandalizi ya maonesho ya nanenane Kitaifa ambayo yanafanyika katika kanda ya ziwa mashariki inayojumuisha mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga ambayo yatafanyika katika Uwanja wa NaneNane Nyakabindi jana uwanjani hapo.


 Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack akizungumza na viongozi na wataalam kutoka mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga katika kikao cha maandalizi ya maonesho ya nanenane Kitaifa ambayo yanafanyika katika kanda ya ziwa mashariki inayojumuisha mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga ambayo yatafanyika katika Uwanja wa NaneNane Nyakabindi jana uwanjani hapo.




AANGALIA BAADHI YA PICHA ZA VIONGOZI KATIKA KIKAO CHA MAANDALIZI YA NANENANE, PICHA ZAO WAKITEMBELEA VIPANDO, PICHA ZA VIPANDO, MAJENGO NA UJENZI WA MAHEMA












0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!