Friday, July 31, 2020

CRDB YAKABIDHI HUNDI YA SHILINGI MILIONI 60 UDHAMINI WA NANENANE KITAIFA 2020 SIMIYU

Benki ya CRDB imekabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni 60 kama mchango wa udhamini wa Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2020 yanayofanyika katika  Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Simiyu, Kanda ya Ziwa Mshariki inayoundwa na mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga kuanzia 01 Agosti, 2020 mpaka 08 Agosti, 2020 

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo Julai 30, 2020 Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Ziwa, Bw. Lusingi Sitta amesema benki hiyo imekuwa mstari wa mbele katika kusaidia wakulima ambapo amesema benki hiyo imejipanga katika kuhakikisha kuwa wakulima wote wa pamba wanapata malipo yao kupitia akaunti za benki ya CRDB.

“Tumehakikisha kuwa AMCOS zote tumefungua nao akaunti kama CRDB tutahakikisha kwamba kila mkulima anayeuza pamba yake atalipwa kupitia akaunti yake ya CRDB na tumejipanga kwamba kila alipo mkulima wa pamba nasi tupo hapo ,” alisema Lusingi.

Aidha, Lusingi amesema CRDB imefungua tawi lingine katika Wilaya ya Meatu ambapo amebainisha kuwa benki hiyo imepeleka gari ambalo lina mahitaji yote muhimu katika utoaji wa huduma na wateja(wananchi ) hivyo wanaweza kupata huduma zote katika gari hilo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga kwa niaba ya Wakuu wa Mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga ameishukuru benki ya CRDB kwa kukubali kuwa mdhamini Mkuu wa Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2020 na kwa namna ambavyo imekuwa ikiwajali wateja hususani wakulima ambapo imetoa zaidi ya asilimia 60 ya mikopo kwa wanunuzi wa pamba msimu wa mwaka 2019/2020 ili pamba ya wakulima inunuliwe.

“Kuna maana kubwa sana kwa CRDB kudhamini maonesho ya nanenane kwa sababu, lengo la maonesho haya ni kuwasaidia wakulima wa kawaida kwenda kwenye ukulima wa kisasa, hivyo inapotokea CRDB inajitokeza kusaidia maonesho kufana, inaenda sambamba na lengo la nchi la kuinua wakulima wadogo wadogo kwenda kwenye ukulima wenye tija,” alisema Kiswaga.

Wakati huo huo Kiswaga amewahakikishia viongozi wa benki ya CRDB kuwa serikali itaendelea kufanya kazi na benki hiyo katika matawi yote huku akitoa wito kwa viongozi hao kutosita kuwaeleza viongozi wa serikali kila wanapohitaji msaada katika maeneo mbalimbali.

Katika hatua nyingine Kiswaga ametoa wito kwa wananchi kutoka mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga inayounda Kanda ya Ziwa Mashariki ya Maonesho ya Nanenane pamoja na maeneo mengine ndani na nje ya nchi; kujitokeza kwa wingi kushiriki katika maonesho ya Nanenane Kitaifa huku akiwahakikishia kuwa maonesho hayo yatakuwa ya tofauti kuwataka watarajia kuona teknolojia mbalimbali zinazoleta mapinduzi katika kilimo.

Kauli Mbiu ya Maonesho ya Nanenane mwaka 2020 ni “KWA MAENDELEO YA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI CHAGUA VIONGOZI BORA 2020.”

MWISHO



Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Ziwa, Bw. Lusingi Sitta (kushoto) akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga (kulia) mfano wa hundi ya shilingi milioni 60, Julai 30, 2020  ikiwa ni udhamini wa Benki hiyo katika Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2020 yatakayofanyika  Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Mkoani Simiyu; Kiswaga amepokea kwa niaba ya Wakuu wa mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga inayounda Kanda ya Ziwa Mashariki ya Maonesho hayo.

:- Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Ziwa, Bw. Lusingi Sitta akizungumza na baadhi ya viongozi wa mkoa wa Simiyu kabla ya kukabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni 60, leo  Julai 30, 2020  ikiwa ni udhamini wa Benki hiyo katika Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2020 yatakayofanyika  Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Mkoani Simiyu.

Baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Simiyu wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Benki ya CRDB baada ya makabidhiano ya  mfano wa hundi ya shilingi milioni 60, leo  Julai 30, 2020  ikiwa ni udhamini wa Benki hiyo katika Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2020 yatakayofanyika  Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Mkoani Simiyu.

Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Mhe. Festo Kiswaga akizungumza mara baada ya kupokea mfano wa hundi ya shilingi milioni 60, leo  Julai 30, 2020 kitoka kwa Meneja wa CRDB Kanda ya Ziwa Bw. Lusingi Sitta ikiwa ni udhamini wa Benki hiyo katika Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2020 yatakayofanyika  Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Mkoani Simiyu; Kiswaga amepokea kwa niaba ya Wakuu wa mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga inayounda Kanda ya Ziwa Mashariki ya Maonesho hayo.

Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Ziwa, Bw. Lusingi Sitta (kushoto) akiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga baada ya makabidhiano ya  mfano wa hundi ya shilingi milioni 60, leo  Julai 30, 2020  ikiwa ni udhamini wa Benki hiyo katika Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2020 yatakayofanyika  Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Mkoani Simiyu

Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Ziwa, Bw. Lusingi Sitta (kushoto) akiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga baada ya makabidhiano ya  mfano wa hundi ya shilingi milioni 60, leo  Julai 30, 2020  ikiwa ni udhamini wa Benki hiyo katika Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2020 yatakayofanyika  Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Mkoani Simiyu.


0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!