Sunday, July 19, 2020

SIMIYU YAJIPANGA KUONGEZA UPATIKANAJI WA HUDUMA ZA UGANI KUONGEZA TIJA KWENYE UZALISHAJI WA PAMBA


Katika kutekeleza mpango Mkakati wa Mapinduzi ya Kilimo cha Pamba wa miaka mitano (2019-2024) wa Mkoa wa Simiyu, mkoa unakusudia kuongeza hali ya upatikanaji wa huduma za ugani kwa lengo la kuongeza tija katika uzalishaji kutoka kilo 175 kufikia kilo 600 kwa ekari ifikapo mwaka 2024.

Hayo yamebainishwa na Katibu Tawala msaidizi sehemu ya mipango na uratibu Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Donatus Weginah wakati akitoa mada katika mafunzo ya maafisa ugani, maafisa ushirika na viongozi waandamizi wa wilaya na Halmashauri juu utekelezaji wa mpango mkakati huo yaliyofanyika Julai 18, 2020 Mjini Bariadi.

Weginah amesema kutokana na upungufu wa maafisa ugani wapatao 200 katika mkoa wa Simiyu, mkoa unatarajia kutoa mafunzo ya muda mfupi ya kilimo bora cha pamba kwa baadhi ya vijana ili waweze kuwasaidia wakulima kulima kilimo chenye tija hususani katika maeneo ambayo hakuna maafisa ugani.

“Tunataka kuongeza uzalishaji kutoka wastani wa kilo 175 zinazozalishwa sasa hivi mpaka kufikia kilo 600 kwa ekari ifikapo mwaka 2024, ili tuweze kufikia hapo ni lazima tuhakikishe huduma za ugani ambazo ni changamoto zinapatikana, tutatumia vijana ambao watapa mafunzo ya muda mfupi ili waweze kuwapatia elimu wakulima wetu huko vijijini,” alisema Weginah.

Aidha, Weginah amebainisha kuwa mafunzo yataanza kwa vijana wataohudumia Vyama vya Msingi vya Ushirika (AMCOS) 26 vilivyochaguliwa kuwa maeneo ya mfano ya kuanzia (pilot areas) kwa mwaka huu na baadaye kuanzia mwaka 2021 vijana hao watapelekwa katika mkoa mzima hususani katika maeneo yenye upungufu mkubwa wa maafisa ugani.

Afisa ugani wa kata ya Chinamili wilayani Itilima, Bw. Gaudence Mlay amesema vijana hao watakaopewa mafunzo pamoja na wakulima wawezeshaji watawasaidia maafisa ugani katika utoaji wa elimu kwa wakulima na watawafikia wakulima wengi zaidi kuliko ilivyo sasa ambapo katika baadhi ya maeneo afisa ugani mmoja anahudumia vijiji vitatu mpaka vinne.

Kwa upande wake Afisa Ushirika wa Halmashauri ya mji wa Bariadi, Bw. Billwater Mbilinyi amesema mkakati wa mapinduzi ya kilimo cha pamba umeanza kutekelezwa kwa kuwatambua wakulima, ukubwa wa maeneo wanayolima na mahitaji ya pembejeo jambo ambalo litasaidia wakulima kupata kiasi cha pembejeo kinachotakiwa  kwa wakati.

Wakati huo huo Mrajisi Msaidizi wa Vyama vya Ushirika mkoa wa Simiyu, Bw. Ibrahimu Kadudu amesema katika utekelezaji wa mkakati huo mkoa wa Simiyu utahakikisha unasimamia matumizi ya mizani za kidijitali ambazo zitatatua changamoto ya mizani kuchezewa hivyo mkulima atapata kile anachostahili kupata wakati anapouza pamba yake.

Awali akifungua mafunzo hayo Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga amesema mpango mkakati huo umekuja katika kipindi muafaka huku akitoa wito kwa wananchi, viongozi wa serikali, iongozi wa dini na wadau wengine wa pamba kuunga mkono utekelezaji wa mkakati huu kwa manufaa ya mkoa na Taifa kwa ujumla.

Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Mhandisi, Mashaka Luhamba akifunga mafunzo hayo amewataka washiriki wote wa mafunzo hayo kila mmoja akatimize wajibu wake katika kutekeleza mkakati huo kwa lengo la kufikia matokeo yaliyotarajiwa ikiwa ni pamoja na kuongeza tija ya kilimo cha pamba  kwa wakulima.

Mkakati wa Mapinduzi ya Kilimo cha Pamba wa miaka mitano (2019-2024) wa Mkoa wa Simiyu ulizinduliwa rasmi tarehe 05  Machi 2020 na Naibu Waziri wa kilimo, Mhe. Hussein Bashe, ambapo utekelezaji wake umeanza na Vyama vya msingi vya ushirika (AMCOS)  26 na baadaye utatekelezwa katika mkoa wote wa Simiyu.
MWISHO

Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Mipango na Uratibu katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Donatus Weginah akitoa mada katika mafunzo ya viongozi na wataalam juu ya utekelezaji wa mpango Mkakati wa Mapinduzi ya Kilimo cha Pamba wa miaka mitano (2019-2024) wa Mkoa wa Simiyu yaliyofanyika Julai 17, 2020 Mjini Bariadi.



Baadhi ya viongozi na watalaam wa kilimo na ushirika wakifuatilia mada iliyowasilishwa katika mafunzo ya viongozi na wataalam juu ya utekelezaji wa mpango Mkakati wa Mapinduzi ya Kilimo cha Pamba wa miaka mitano (2019-2024) wa Mkoa wa Simiyu yaliyofanyika Julai 17, 2020 Mjini Bariadi.
 Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga (kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka) akifungua mafunzo ya viongozi na wataalam juu ya utekelezaji wa mpango Mkakati wa Mapinduzi ya Kilimo cha Pamba wa miaka mitano (2019-2024) wa Mkoa wa Simiyu yaliyofanyika Julai 17, 2020 Mjini Bariadi.


Kaimu katibu Tawala wa mkoa wa Simiyu, Mhandisi. Mashaka Luhamba akifunga mafunzo ya viongozi na wataalam juu ya utekelezaji wa mpango Mkakati wa Mapinduzi ya Kilimo cha Pamba wa miaka mitano (2019-2024) wa Mkoa wa Simiyu, yaliyofanyika Julai 17, 2020 Mjini Bariadi.

Mrajisi msaidizi wa Vyama vya Ushirika mkoa wa Simiyu, Bw. Ibrahimu Kadudu akiwasilisha mada  katika mafunzo ya viongozi na wataalam juu ya utekelezaji wa mpango Mkakati wa Mapinduzi ya Kilimo cha Pamba wa miaka mitano (2019-2024) wa Mkoa wa Simiyu, yaliyofanyika Julai 17, 2020 Mjini Bariadi.

Baadhi ya viongozi na watalaam wa kilimo na ushirika wakifuatilia mada iliyowasilishwa katika mafunzo ya viongozi na wataalam juu ya utekelezaji wa mpango Mkakati wa Mapinduzi ya Kilimo cha Pamba wa miaka mitano (2019-2024) wa Mkoa wa Simiyu, yaliyofanyika Julai 17, 2020 Mjini Bariadi.

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Bi. Suzy Sabuni akichangia hoja katika mafunzo ya viongozi na wataalam juu ya utekelezaji wa mpango Mkakati wa Mapinduzi ya Kilimo cha Pamba wa miaka mitano (2019-2024) wa Mkoa wa Simiyu, yaliyofanyika Julai 17, 2020 Mjini Bariadi.
 Afisa Tarafa kutoka  wilayani Maswa akichangia hoja katika mafunzo ya viongozi na wataalam juu ya utekelezaji wa mpango Mkakati wa Mapinduzi ya Kilimo cha Pamba wa miaka mitano (2019-2024) wa Mkoa wa Simiyu, yaliyofanyika Julai 17, 2020 Mjini Bariadi.

 Mkuu wa Jeshi la Zimamoto na uokoaji mkoa wa Simiyu, akichangia hoja katika mafunzo ya viongozi na wataalam juu ya utekelezaji wa mpango Mkakati wa Mapinduzi ya Kilimo cha Pamba wa miaka mitano (2019-2024) wa Mkoa wa Simiyu, yaliyofanyika Julai 17, 2020 Mjini Bariadi.


Afisa Kilimo wa Wilaya ya Meatu, akichangia hoja katika mafunzo ya viongozi na wataalam juu ya utekelezaji wa mpango Mkakati wa Mapinduzi ya Kilimo cha Pamba wa miaka mitano (2019-2024) wa Mkoa wa Simiyu yaliyofanyika Julai 17, 2020 Mjini Bariadi.
 Baadhi ya viongozi na watalaam wa kilimo na ushirika wakifuatilia mada iliyowasilishwa katika mafunzo ya viongozi na wataalam juu ya utekelezaji wa mpango Mkakati wa Mapinduzi ya Kilimo cha Pamba wa miaka mitano (2019-2024) wa Mkoa wa Simiyu yaliyofanyika Julai 17, 2020 Mjini Bariadi.


Baadhi ya viongozi na watalaam wa kilimo na ushirika wakifuatilia mada iliyowasilishwa katika mafunzo ya viongozi na wataalam juu ya utekelezaji wa mpango Mkakati wa Mapinduzi ya Kilimo cha Pamba wa miaka mitano (2019-2024) wa Mkoa wa Simiyu yaliyofanyika Julai 17, 2020 Mjini Bariadi.
 Baadhi ya viongozi na watalaam wa kilimo na ushirika wakifuatilia mada iliyowasilishwa katika mafunzo ya viongozi na wataalam juu ya utekelezaji wa mpango Mkakati wa Mapinduzi ya Kilimo cha Pamba wa miaka mitano (2019-2024) wa Mkoa wa Simiyu yaliyofanyika Julai 17, 2020 Mjini Bariadi.


Baadhi ya viongozi na watalaam wa kilimo na ushirika wakifuatilia mada iliyowasilishwa katika mafunzo ya viongozi na wataalam juu ya utekelezaji wa mpango Mkakati wa Mapinduzi ya Kilimo cha Pamba wa miaka mitano (2019-2024) wa Mkoa wa Simiyu yaliyofanyika Julai 17, 2020 Mjini Bariadi.





Baadhi ya viongozi na watalaam wa kilimo na ushirika wakifuatilia mada iliyowasilishwa katika mafunzo ya viongozi na wataalam juu ya utekelezaji wa mpango Mkakati wa Mapinduzi ya Kilimo cha Pamba wa miaka mitano (2019-2024) wa Mkoa wa Simiyu yaliyofanyika Julai 17, 2020 Mjini Bariadi. 

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!