Wednesday, July 22, 2020

TACAIDS YAKABIDHI MASANDUKU 10 YA KUCHANGIA FEDHA ZA KUBORESHA HUDUMA ZA VVU NA UKIMWI SIMIYU

Tume ya Taifa ya Kudhibiti UKIMWI imekabidhi masanduku 10 kutoka Mfuko wa Udhamini wa Kudhibiti Ukimwi kwa Mkoa wa Simiyu ili yatumike kwa ajili ya kuhamasisha uchangiaji wa fedha kwa ajili ya kuboresha huduma za VVU na UKIMWI.

Akikabidhi masanduku hayo Mkurugenzi wa TACAIDS Dkt. Leonard Maboko amesema karibuni Wafadhili wamepunguza kwa kiasi kikubwa ufadhili katika masuala ya Ukimwi ni  vema zikatumika  fedha zetu wenyewe (wadau wa ndani)  badala ya kutegemea Wafadhili

“ Ili Kuchangia fedha hizo Mfuko  umebuni Masanduku ambayo Wanainchi wanaweza kutoa michango kwa Fedha taslim, tumeleta masanduku haya 10 ikiwa ni maagizo ya Waziri wa nchi ofisi ya Waziri  Mkuu Kazi, Vijana,Ajira na Wenye  Ulemavu Mhe.Jenista Mhagama ambaye alikuwa mgeni rasmi akimwakilisha  Mhe. Kassim Majaliwa  Waziri Mkuu,wakati wa maadhimisho ya siku ya ukimwi duniani yaliyofanyika kitaifa mkoani Mwanza 2019”

“ Katika maadhimisho hayo kila mkoa uliagizwa kuwa na   masanduku hayo na kuhamasisha wananchi kuchangia jitihada hizi, Siku ya Ukimwi Duniani 2020 kila mkoa utatakiwa kutoa taarifa kuwa umechangia Serikali kiasi gani kupitia Mfuko wa Udhamini wa  kudhibiti Ukimwi, alisema Dkt. Maboko.

Aidha, Dkt. Maboko amesema michango hiyo inaweza  kuwakilishwa kwa kuchangia Moja kwa moja au kupitia AIrtel Money +255 684 909090 au kwa Viongozi kuchukua masanduku na kuhamasisha wananchi kuchangia katika ziara na matukio mbalimbali ambayo wao wanayaongoza huku akibainisha kuwa mpaka sasa fuko umeshaipatia Serikali kiasi cha shilingi 660.

Katika hatua nyingine Dkt. Maboko amefafanua kuwa katika fedha zote zinazokusanywa  katika mfuko huu, asilimia 60 hutumika kwenye ununuzi wa dawa/vitendanishi,  asilimia 25 hutumika   kwenye kinga na asilimia 15 kwenye shughuli za bodi na Utawala.

Akipokea msaada huo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa Wa Simiyu, Mhandisi.Mashaka Luhamba ameshukuru TACAIDS kwa kutimiza ahadi ya kuleta masanduku hayo kama walivyoahidi kwa Mhe. Mkuu wa Mkoa huku akiwahakikishia TACAIDS kuwa mkoa utatumia kila fursa kuhakikisha kuwa unawahamasisha Wananchi wa  Simiyu kuchangia katika Mfuko huu.

Akieleza hali ya maambukizi ya VVU/UKIMWI katika Mkoa wa Simiyu, Mratibu wa Kudhibiti UKIMWI Simiyu, Dkt.Khamis  Kulemba amesema kutokana na utafiti wa Mwaka  2016-2017 ushamiri wa maambuziki ya VVU Mkoani Simiyu umefikia kiwango cha  3.9%  ambayo ni chini ya  4.7% ikiwa ni  kiwango cha  kitaifa

“ Tunaendelea na kazi ya kuzuia maambukizi mapya kwa kuwezesha asilimia 90 watu wanatambua hali za afya zao,  asilimia 90% ya  wagonjwa  wanatumia dawa na asilimia 90 nyingine kushusha kiwango cha virusi vya UKIMWI katika damu ya Mgonjwa ( Viral suppression)

Dkt. Kulemba ameongeza kuwa Mkoani Simiyu asilimia 91 ya watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI wanatumia dawa za kufubaza makali ya VVU na kiwango cha maambukizi katika damu zao kimeshuka, huku akitoa wito kwa wananchi kuchangia mfuko wa kudhibiti UKIMWI kwani vita dhidi ya VVU/UKIMWI ni ya kila mmoja katika jamii.

Mfuko wa Udhamini wa kudhibiti ukimwi  ulianzishwa Mwaka  2015, Kusudi la Mfuko huu ni  kuchangia fedha kwa ajili ya kuboresha huduma za VVU na UKIMWI.
MWISHO




Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti UKIMWI (TACAIDS),  Dkt. Leonard Maboko(kushoto) akimkabidhi moja ya sanduku Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu,  Mhandisi.Mashaka Luhamba yaliyotolewa na TACAIDS kwa ajili ya kuhamasisha uchangiaji wa fedha kwa ajili ya kuboresha huduma za VVU na UKIMWI.
 Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu,  Mhandisi.Mashaka Luhamba (kushoto) akimkabidhi Mratibu wa Kudhibiti UKIMWI Simiyu, Dkt.Khamis  Kulemba moja ya masanduku yaliyotolewa na TACAIDS kwa ajili ya kuhamasisha uchangiaji wa fedha kwa ajili ya kuboresha huduma za VVU na UKIMWI.
 Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu,  Mhandisi.Mashaka Luhamba (katikati) akimshukuru Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti UKIMWI (TACAIDS),  Dkt. Leonard Maboko baada ya makabidhiano ya masanduku 10 yaliyotolewa na TACAIDS kwa ajili ya kuhamasisha uchangiaji wa fedha kwa ajili ya kuboresha huduma za VVU na UKIMWI mkoani Simiyu.

 Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti UKIMWI (TACAIDS),  Dkt. Leonard Maboko (kushoto) akizungumza kabla ya kukabidhi kwa Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu,  Mhandisi. Mashaka Luhamba (wa tano kulia) masanduku 10 yaliyotolewa na TACAIDS kwa ajili ya kuhamasisha uchangiaji wa fedha kwa ajili ya kuboresha huduma za VVU na UKIMWI mkoani Simiyu.

Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu,  Mhandisi.Mashaka Luhamba  akizungumza kabla ya kupokea masanduku yaliyotolewa na TACAIDS kwa ajili ya kuhamasisha uchangiaji wa fedha kwa ajili ya kuboresha huduma za VVU na UKIMWI kutoka TACAIDS.


0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!