Thursday, April 4, 2019

RC MTAKA AZINDUA KAMBI YA KITAALUMA KWA KIDATO CHA SITA SIMIYU, AAGIZA TAA ZISIZIMWE WASOME


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka amezindua rasmi  kambi ya kitaaluma  kwa Wanafunzi wa  Kidato cha sita kwa mwaka 2019 yenye wanafunzi 1166 na kuagiza taa zisizimwe usiku ili wanafunzi waweze kupata nafasi ya kujisomea zaidi.

Mtaka ametoa agizo hilo , wakati akizindua  kambi hiyo kwa  wanafunzi 1166 wa kidato cha sita na walimu mahiri 34  kutoka shule 12 za mkoa wa Simiyu,  inayofanyika katika shule ya sekondari ya  wasichana ya Maswa.

 
Amesema ili mkoa wa SIMIYU uweze kushindana kiuchumi unapaswa kufanya  mageuzi makubwa ya kielimu, hivyo elimu ni kiupaumbele cha mkoa ambapo ameagiza katika kipindi chote cha kambi wanafunzi waruhusiwe kusoma  bila kuzimiwa taa darasani.

Katika hatua nyingine Mtaka amewahakikishia wanafunzi na walimu upatikanaji wa mahitaji yote muhimu wawapo kambini, ikiwa ni pamoja na ulinzi na usalama, upatikanaji wa chakula, maji, umeme, mahitaji mengine na kueleza kuwa tayari viti vipatavyo 1000 vimeshanunuliwa kwa ajili ya kambi hiyo.

Aidha, ameahidi kutoa zawadi mbalimbali kwa wanafunzi, walimu na shule itakayofanya vizuri katika mtihani wa kidato cha Sita mwaka 2019 “Ofisi yangu itatoa zawadi ya shilingi milioni tatu kwa mwanafunzi atakayepata ‘division one ya point tatu’ atakayepata ‘division one ya point 4 na 5’ atapata shilingi laki tano; shule itakayokuwa katika kumi bora Kitaifa itapata shilingi milioni tano” alisema.

Kuhusu walimu watakaofanya vizuri katika masomo yao, Mtaka amesema mwalimu atapata zawadi ya shilingi elfu 50 kwa kila alama A itakayopatikana kwenye somo lake, huku akiahidi pia kutoa shilingi milioni 12 kwa ajili ya posho ya walimu walio kambini.

Kwa upande wao  Afisa Elimu Mkoa wa Simiyu, Mwl. Ernest Hinju na Mwenyekiti wa wakuu wa shule mkoa wa Simiyu, Mwl. Amede Ndonje wamekiri  kuwa kambi za kitaaluma zimechangia kuongeza ufaulu katika mitihani ya  kidato cha sita kutoka nafasi ya 26 mwaka 2017 hadi nafasi ya 10 mwaka 2018 na kwa kidato cha nne kutoka nafasi ya 11 mwaka 2017, hadi kufikia nafasi ya tisa mwaka 2018.
Baadhi ya walimu mahiri na wanafunzi wa Kidato cha Sita wametoa maoni yao kuhusu kambi “Tuna malengo ya kufanya vizuri zaidi ya mwaka jana, kambi ya mwaka jana ilikuwa kwa siku chache tu sisi tumepewa siku 28 nina uhakikika tutazitumia vizuri na tutahakikisha mkoa wetu unakuwa wa kwanza” MkimaWarento kutoka Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa.

“ Kuanzisha kambi za kitaaluma ni wazo zuri na  napenda kuwahakikishia kuwa fedha zenu mlizowekeza hapa kambini si bure, tunawaahidi kuwa hatutawaangusha sisi tumejipanga kufanya mapinduzi ya kitaaluma na tutakuwa nambari moja mwaka huu” alisema  Kasto Nyakarungu mwanafunzi wa Kidato cha Sita Shule ya Sekondari Binza.

“Nikiwa miongoni mwa walimu wawezeshaji katika kambi hii ya Kitaaluma niwahakikishie kuwa tumejipanga ipasavyo kuhakikisha mkoa wetu unaingia katika tatu bora na matarajio yetu ni kuwa nafasi ya kwanza” alisema Mwalimu Mary Kavishe anayefundisha somo la Kiswahili.

Katika uzinduzi huo wa kambi za kitaaluma wadau mbalimbali wakiwemo viongozi wa Chama na Serikali pamoja na watumishi wa Umma wameahidi kuchangia vyakula ambavyo ni mchele zaidi ya tani mbili, maharage kilo 200, ng’ombe wawili na fedha taslimu ili kufanikisha kambi hiyo kufanyika vizuri.

Wanafunzi wa Kidato cha Sita wako kambini kuanzia tarehe Mosi Aprili, 2019 na wanatarajia kukaa kambini kwa takribani siku 28 na baadaye kutawanyika kwenda kwenye shule zao kwa ajili ya maandalizi ya mwisho ya Mtihani wa Taifa utakaoanza Mei 06, 2019.
MWISHO
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(katikati) akifurahia  jambo na baadhi ya wanafunzi wa Kidato cha Sita katika Shule ya Sekondari Itilima, mara baada ya kuzindua rasmi kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi wa Kidato cha Sita mwaka 2019, uliofanyika katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Aprili 3, 2019.
 Kutoka kulia Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu,Bw. Jumanne Sagini, Katibu Tawala wa Wilaya ya Maswa, Bw. Godwin Chacha na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa(NEC), Mhe. Emmanuel Gungu Silanga  wakiteta jambo wakati wa uzinduzi rasmi wa kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi wa Kidato cha Sita mwaka 2019, uliofanyika katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Aprili 3, 2019. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa, Dkt. Fredrick Sagamiko akizungumza katika uzinduzi rasmi kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi wa Kidato cha Sita mwaka 2019, uliofanyika katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Aprili 3, 2019.
 Mkuu wa Shule ya Sekondari Binza akionesha fedha kiasi cha shilingi 500,000/= zilizotolewa na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa(NEC), Mhe. Emmanuel Gungu Silanga(wa tatu kushoto) kwa ajili ya walimu wanaofundisha wanafunzi wa Kidato cha Sita wakati wa uzinduzi rasmi kambi hiyo, uliofanyika katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Aprili 3, 2019. 



Afisa Elimu Mkoa wa Simiyu, Mwl. Ernest Hinju akizungumza katika uzinduzi rasmi kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi wa Kidato cha Sita mwaka 2019, uliofanyika katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Aprili 3, 2019. 

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(katikati)akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Viongozi wa Chama na Serikali (walioketi) na wanafunzi wa Kidato cha Sita mwaka 2019 Shule ya Sekondari Meatu, mara baaada ya uzinduzi rasmi kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi wa Kidato cha Sita mwaka 2019, uliofanyika katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Aprili 3, 2019.

Mwanafunzi wa Kidato cha Sita katika Shule ya Sekondari Maswa, Mkami Warento akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi wa Kidato cha Sita mwaka 2019, uliofanyika katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Aprili 3, 2019.

Kasto Nyakarungu Mwanafunzi Wa Kidato Cha Sita Shule Ya Sekondari Binza Warento akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi wa Kidato cha Sita mwaka 2019, uliofanyika katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Aprili 3, 2019.
 Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu,Bw. Jumanne Sagini, akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi wa Kidato cha Sita mwaka 2019, uliofanyika katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Aprili 3, 2019. 


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(katikati) akifurahi jambo na baadhi ya wanafunzi wa Kidato cha Sita katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa na Mkuu wao wa Shule, mara baada ya kuzindua rasmi kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi wa Kidato cha Sita mwaka 2019, uliofanyika katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Aprili 3, 2019.
Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Simiyu, Mhe. Mariam Manyangu akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi wa Kidato cha Sita mwaka 2019, uliofanyika katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Aprili 3, 2019. 
Katibu wa CWT Mkoa wa Simiyu, Mwl. Said Mselem akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi wa Kidato cha Sita mwaka 2019, uliofanyika katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Aprili 3, 2019.
 Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akimtambulisha mmoja wa wadau wa maendeleo ya Elimu ambaye ni Diwani wilayani Bariadi, wakati wa uzinduzi rasmi kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi wa Kidato cha Sita mwaka 2019, uliofanyika katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Aprili 3, 2019. 

 Baadhi ya wakuu wa shule na wanafunzi wa kidato cha sita kutoka katika shule za mkoa wa Simiyu wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (hayupo pichani) , wakati wa uzinduzi rasmi kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi wa Kidato cha Sita mwaka 2019, uliofanyika katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Aprili 3, 2019. 
Baadhi ya walimu mahiri kutoka shue 12 za Kidato cha Tano na Sita mkoani Simiyu, wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (hayupo pichani) , wakati wa uzinduzi rasmi kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi wa Kidato cha Sita mwaka 2019, uliofanyika katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Aprili 3, 2019.
 Baadhi ya walimu mahiri kutoka shule 12 za Kidato cha Tano na Sita mkoani Simiyu, wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (hayupo pichani) , wakati wa uzinduzi rasmi kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi wa Kidato cha Sita mwaka 2019, uliofanyika katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Aprili 3, 2019.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akimkabidhi fedha Mwanafunzi mtarajiwa wa Kidato cha Tano, Silya Shiwa Jasamila(19) ambaye analelewa na Serikali katika Shule ya Sekondari Maswa Girls baada ya kukimbia nyumbani kwao baba yake alipotaka kumuozesha mara baada ya kumaliza kidato cha nne 2018 katika Shule ya Sekondari Kilabela Wilayani Bariadi na kupata ‘division two ya point 19’.
Baadhi ya wanafunzi wakiimba wimbo wa Tanzania kabla ya uzinduzi rasmi kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi wa Kidato cha Sita mwaka 2019, uliofanyika katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Aprili 3, 2019.
Afisa Elimu wa Mkoa wa Simiyu, Mwl. Ernest Hinju (wa pili kushoto) na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (wa pili kulia)  wakifurahia jambo na baadhi ya wanafunzi wa kidato cha Sita mara baada ya uzinduzi rasmi kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi wa Kidato cha Sita mwaka 2019, uliofanyika katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Aprili 3, 2019.
 Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (kushoto) akizungumza na baadhi wanafunzi  mara baada ya kuzindua rasmi kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi wa Kidato cha Sita mwaka 2019, uliofanyika katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Aprili 3, 2019. 
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza jambo na mwanafunzi wa Kidato cha Tano mtarajiwa, Silya Shiwa Jasamila(19) ambaye analelewa na Serikali katika Shule ya Sekondari Maswa Girls baada ya kukimbia nyumbani kwao baba yake alipotaka kumuozesha mara baada ya kumaliza kidato cha nne 2018 katika Shule ya Sekondari Kilabela Wilayani Bariadi na kupata ‘division two ya point 19’.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na walimu na wanafunzi katika uzinduzi  rasmi kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi wa Kidato cha Sita mwaka 2019, uliofanyika katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Aprili 3, 2019.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(katikati)akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Viongozi wa Chama na Serikali, mara baaada ya uzinduzi rasmi kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi wa Kidato cha Sita mwaka 2019, uliofanyika katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Aprili 3, 2019.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na baadhi wanafunzi  mara baada ya kuzindua rasmi kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi wa Kidato cha Sita mwaka 2019, uliofanyika katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Aprili 3, 2019.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na walimu na wanafunzi katika uzinduzi  rasmi kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi wa Kidato cha Sita mwaka 2019, uliofanyika katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Aprili 3, 2019.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na baadhi wanafunzi  mara baada ya kuzindua rasmi kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi wa Kidato cha Sita mwaka 2019, uliofanyika katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Aprili 3, 2019.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na baadhi wanafunzi  mara baada ya kuzindua rasmi kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi wa Kidato cha Sita mwaka 2019, uliofanyika katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Aprili 3, 2019.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari Itilima, mara baada ya uzinduzi rasmi wa kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi wa Kidato cha Sita mwaka 2019, uliofanyika katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Aprili 3, 2019.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!