Thursday, May 31, 2018

MASWA WARIDHIA KAYA KUCHANGIA SHILINGI ELFU 50 KWA MWAKA KWA AJILI YA MAENDELEO

Viongozi wa wananchi, wenyeviti wa vitongoji na vijiji 120 vya wilaya ya Maswa mkoani Simiyu wameridhia mchango wa shilingi elfu hamsini kila kaya kwa ajili ya shughuli za maendeleo ambao utatolewa kwa mwaka, ambapo baada ya kaya kutoa mchango huo hazitachangia mchango mwingine wowote.

Hayo wameyasema katika mkutano uliofanyika katika Uwanja wa Nguzo nane Mjini  Maswa baina ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka na viongozi wa vitongoji ,vijiji na  wadau mbalimbali wa maendeleo  ,wakiwemo viongozi wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa, viongozi wa dini  na  wananchi, lengo likiwa ni kujadili azimio lililopitishwa na Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Maswa la Uchangiaji shughuli za maendeleo hususani ujenzi wa miundombinu ya elimu na afya.

“Kwanza ni  vizuri ikafahamika kwamba viongozi wa wananchi wameridhia mchango, hii habari ya nani kasema hapana ni lazima tutoe uhuru wa kutoa maoni, sidhani kama ingekuwa sahihi  tuje hapa tuamue kuwa haya ni maelekezo; lakini pili hatujasema adhabu kuwa asiyetoa mchango huu atafanywa nini waandishi wa habari saidieni kuondoa uzushi huu kwenye mitandao” amesema Mtaka.

Mtaka amesema ni vema  ikafahamika wazi kuwa baada ya kaya kutoa  mchango huu wananchi hawatachangiswa mchango wowote, huku akisisitiza kuwa mchngo huu hautazihusu zilizo chini ya Mpango wa Kunusuru kaya Maskini TASAF III pamoja na kaya za wananchi walio katika misamaha mbalimbali ya Serikali.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka wakati akihitimisha mkutano huo amesema uamuzi wa kuwa na mchango huo umetokana na kuona wananchi wamekuwa wakichangishwa michango mingi ya rejareja ambayo ilikuwa ikizidi kiasi cha shilingi elfu 50,  hivyo Halmashauri ikaona ipo haja ya kuwa na mchango mmoja ambao utakuwa na unafuu.

“Huu mchango ni sawa na michango mingine ambayo Wananchi wamekuwa wakichangia siku zote kwa ajili ya shughuli za maendeleo, lakini sasa hivi Halmashauri baada ya kuona wananchi wakichangia rejareja wanachangia fedha nyingi, iliona ni vema kukawa na mchango mmoja kwa mwaka wa shilingi elfu 50” alifafanua Mtaka.
Awali akitoa ufafanuzi kuhusu mchango huo Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe. Dkt. Seif Shekalaghe amesema wilaya hiyo ilifikia uamuzi wa kuwa na mchango mmoja kutokana na michango iliyokuwa ikitolewa rejareja kutokuwa na matokeo yaliyokusudiwa, ikiwa ni pamoja na miradi iliyokusudiwa kujengwa na fedha za michango hiyo hususani miundombinu yal elimu na Afya kutokamilika kwa wakati.
Kwa upande wake Erasto Mbigili Mwenyekiti wa Kijiji cha Mbalagane amesema  anaunga mkono wazo la kuwa na mchango mmoja kwa mwaka ambao utawarahisishia Wenyeviti wa Vijiji na vitongoji na kuwaondolea kero ya kwenda kila mara kuwasumbua wananchi kuomba michango.

Naye John Dalawida Mwenyekiti Kitongoji cha Matale amesema anaunga mkono wazo hilo ambalo limeanzia kwa madiwani ambao ni wawakilishi wao na anaamini litasaidia ukamilishaji wa maboma ya vyumba vya madarasa na zahanati waliyoanza kujenga ili kuboresha miundombinu ya sekta ya elimu na afya wilayani Maswa.

Jeremia Shigala Diwani wa kata ya Zanzui amesema Baraza la madiwani lilizimia kuja na mchango huo baada ya wataalam wa Halmashauri kuonesha mchanganuo kuwa wananchi wilayani humo wamekuwa wakichangia wastani wa shilingi elfu 70 kwa mwaka,  hivyo alilipokea na kuahidi kwenda kuwaelimisha wananchi  juu ya umuhimu wa mchango huo wa mara moja.

Katika Mkutano huo viongozi wa Chama na Serikali walitoa michango yao ya fedha taslimu, ahadi na vifaa vya ujenzi ili kuuunga mkono wazo la ujenzi wa miundombinu ya elimu na afya katika wilaya ya Maswa, ambapo Mkuu wa Mkoa wa Simiyu aliahidi kutoa shilingi 1,000,000/=, Mkuu wa wilaya hiyo aliahidi kutoa shilingi 500,000/= Mkurugenzi wa Halmashauri aliahidi kutoa shilingi 500,000/= na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC) akaahidi kutoa jumla ya mabati 500 kama mchango wake.
MWISHO
Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe.Dkt. Seif Shekalaghe akizungumza na Viongozi wa Vitongoji, Vijiji, Kata, Wilaya na Mkoani Simiyu katika Mkutano uliofanyika katika Uwanja wa Nguzo Nane Mjini Maswa.
Baadhi ya Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa wakifuatilia mkutano baina ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka   na viongozi wa vitongoji ,vijiji na  wadau mbalimbali wa maendeleo  ,wakiwemo viongozi wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa na   wananchi, lengo likiwa ni kujadili azimio lililopitishwa na Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Maswa la Uchangiaji shughuli za maendeleo. 


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa, Dkt. Fredrick Sagamiko (kulia) akifafanua jambo katika kikao cha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka   na viongozi wa vitongoji ,vijiji na  wadau mbalimbali wa maendeleo  ,wakiwemo viongozi wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa na   wananchi, lengo likiwa ni kujadili azimio lililopitishwa na Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Maswa la Uchangiaji shughuli za maendeleo. 
Diwani wa kata ya Zanzui Mhe. Jeremia Shigala akichangia hoja katika kikao cha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka na viongozi wa vitongoji ,vijiji na  wadau mbalimbali wa maendeleo  ,wakiwemo viongozi wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa na wananchi, lengo likiwa ni kujadili azimio lililopitishwa na Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Maswa la Uchangiaji shughuli za maendeleo. 

Baadhi ya Viongozi wa Mkoa wa Simiyu wakifurahia jambo katika Mkutano wa viongozi wa vitongoji ,vijiji na  wadau mbalimbali wa maendeleo  ,wakiwemo viongozi wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa na   wananchi, lengo likiwa ni kujadili azimio lililopitishwa na Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Maswa la Uchangiaji shughuli za maendeleo.

Baadhi ya Wenyeviti wa Vitongoji na Vijiji vya Wilaya ya Maswa, wakifuatilia mkutano baina yao na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka   na  wadau mbalimbali wa maendeleo  ,wakiwemo viongozi wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa na   wananchi, lengo likiwa ni kujadili azimio lililopitishwa na Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Maswa la Uchangiaji shughuli za maendeleo. 

Mkuu wa Wilaya ya Maswa , Mhe. Dkt. Shekalaghe akipokea mchango kwa Katibu wa CCM Mkoa, Bw. Donald Magesa mara baada ya kikao cha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka   na viongozi wa vitongoji ,vijiji na  wadau mbalimbali wa maendeleo  ,wakiwemo viongozi wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa na wananchi, lengo likiwa ni kujadili azimio lililopitishwa na Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Maswa la Uchangiaji shughuli za maendeleo.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa, Mhe. Enock Yakobo akifafanua jambo katika kikao cha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka na viongozi wa vitongoji ,vijiji na  wadau mbalimbali wa maendeleo  ,wakiwemo viongozi wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa na   wananchi, lengo likiwa ni kujadili azimio lililopitishwa na Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Maswa la Uchangiaji shughuli za maendeleo. 
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Maswa, Mhandisi. Paul Jidayi akifafanua jambo katika kikao cha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka na viongozi wa vitongoji ,vijiji na  wadau mbalimbali wa maendeleo  ,wakiwemo viongozi wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa na   wananchi, lengo likiwa ni kujadili azimio lililopitishwa na Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Maswa la Uchangiaji shughuli za maendeleo.
Diwani wa Viti Maalum CCM , Mhe. Leticia Lolela akichangia hoja katika kikao cha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka na viongozi wa vitongoji ,vijiji na  wadau mbalimbali wa maendeleo  ,wakiwemo viongozi wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa na wananchi, lengo likiwa ni kujadili azimio lililopitishwa na Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Maswa la Uchangiaji shughuli za maendeleo.
Kutoka kulia mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe. Enock Yakobo, Mkuu wa Mkoa huo, Mhe.Anthony Mtaka, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa, Dkt. Fredrick Sagamiko na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC)  Mhe. Gungu Silanga  wakiteta jambo wakati wa kikao maalum cha kujadili azimio lililopitishwa na Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Maswa la Uchangiaji shughuli za maendeleo katika Uwanja wa Nguzo Nane Mjini Maswa.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na na viongozi wa vitongoji ,vijiji na  wadau mbalimbali wa maendeleo  ,wakiwemo viongozi wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa na   wananchi, lengo likiwa ni kujadili azimio lililopitishwa na Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Maswa la Uchangiaji shughuli za maendeleo.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe. Enock Yakobo na Katibu Mkuu wa CCM mkoa, Bw. Donald Magesa wakiteta jambo wakati wa kikao maalum cha kujadili azimio lililopitishwa na Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Maswa la Uchangiaji shughuli za maendeleo katika Uwanja wa Nguzo Nane Mjini Maswa.
Kutoka kulia Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe. Enock Yakobo, Mkuu wa Mkoa, Mhe.Anthony Mtaka na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC)  Mhe. Gungu Silanga  wakiteta jambo wakati wa kikao maalum cha kujadili azimio lililopitishwa na Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Maswa la Uchangiaji shughuli za maendeleo katika Uwanja wa Nguzo Nane Mjini Maswa.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!