Friday, May 18, 2018

RC MTAKA: TUTAKUWA NA UWANJA WA NANENANE UTAKAOFANYA MAONESHO YA KILIMO BIASHARA

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema dhamira ya Kanda mpya ya  Maonesho ya Kilimo na Sherehe za Nane Nane ya Ziwa Mashariki inayojumuisha mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga ni kuwa na Uwanja wa Nanenane utakaofanya  Maonesho ya  Kilimo Biashara.


Mtaka amesema hayo wakati akifungua kikao cha  Maandalizi ya Maonesho ya Nanenane ya Kanda ya Ziwa Mashariki  yatakayofanyika katika viwanja vya Nyakabindi kilichowakutanisha Wakuu wa Mikoa mitatu  ,Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri  na Sekretarieti za Mikoa  hiyo, ambacho kilifanyika mjini Bariadi.

Amesema pamoja na kufanya maonesho ya Kilimo Nanenane ambayo huwa yanafanyika kuanzia Agosti Mosi hadi Agosti 08 kila mwaka,  kutafanyika Maonesho mengine mara nne kwa mwaka pamoja na matukio mengine yatakayofanyika katika uwanja huo ili kuwe na tija kwa  Halmashauri kuwekeza fedha katika uwanja huo.

“Haiwezekani Halmashauri zetu zikawekeza katika uwanja wa NaneNane halafu uwanja uwe unatumika kila tarehe 01 hadi 08 mwezi wa nane kila mwaka tu, ni lazima  tuwe na viwanja ambavyo vitafanya maonesho ya kilimo biashara lakini eneo lile ukiacha maonesho haya ya NaneNane tutafanya maonesho mara nne kwa mwaka” alisema.

Ameongeza kuwa ili kuendana na hali ilivyo sasa ni vema Halmashauri zikakubaliana kujenga jengo la maonesho (exhibition hall) na kuwa na maeneo ya nje kwa ajili ya vipando na mifugo kama ilivyopendekezwa katika vikao vya awali,  badala ya kutumia vibanda na mahema kama ilivyozoeleka, ili kuifanya Nane Nane ya Kanda Mpya ya Ziwa Mashariki kuwa ya tofauti.

Katika kikao hicho, Halmashauri 21 za Mikoa ya Mara, Shinyanga na Simiyu zimeagizwa kuwasilisha mchango wa  kiasi cha shilingi milioni 20 ndani ya siku saba kwa ajili ya malipo ya awali ya ujenzi wa jengo la maonesho, huku Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mhe. Adam Malima akiwataka Wakurugenzi kutelekeleza agizo hilo.

“.....tumekubaliana kuwa kila Halmashauri itatoa shilingi milioni 20 na hili si jambo la masihara...  ndani ya siku saba tukitoka hapa kila Mkurugenzi atakuja na hundi yake ya shilingi milioni 20, ili itakapofika Juni Mosi haya mambo yakamilike” alisema Malima.  

Naye Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Mhe. Glorius Luoga ametoa wito kwa Wakurugenzi wa Halmashauri zote katika mikoa hiyo kuwa wabunifu katika kuhakikisha fedha za kuwezesha ujenzi wa jengo hilo linalotarajiwa kugharimu jumla ya shilingi bilioni 2.1 zinapatikana.

Hivi karibuni Wizara ya kilimo imetangaza Kanda Mpya ya Maonesho ya Nanenane ijulikanayo kama Kanda ya Ziwa Mashariki, ambayo inajumuisha mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga na Uwanja utakaotumika kwa ajili ya Maonesho hayo uko Eneo la Nyakabindi Mjini Bariadi Mkoani Simiyu, ambapo mwaka 2018 Kanda hiyo itakuwa mwenyeji wa maonesho hayo kitaifa.
MWISHO

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka  akifungua kikao cha viongozi na wataalam wa mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga  katika kikao maalum cha Maandalizi ya Maonesho ya Nanenane Kanda ya  Ziwa Mashariki, kilichofanyika Mjini Bariadi.
 Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mhe.Adam Malima akizugumza na viongozi  na wataalam kutoka mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga  katika kikao maalum cha Maandalizi ya Maonesho ya Nanenane Kanda ya  Ziwa Mashariki, kilichofanyika Mjini Bariadi Mkoani Simiyu.
Mkuu wa Wilaya ya Musoma mkoani , Mhe.Dkt. Vicent Naane akichangia hoja katika kikao cha viongozi na wataalam wa mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga  katika kikao maalum cha Maandalizi ya Maonesho ya Nanenane Kanda ya  Ziwa Mashariki,  kilichofanyika Mjini Bariadi.
Baadhi ya Wakuu wa Wilaya  na viongozi wengine wakifuatilia kikao cha viongozi na wataalam wa mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga  katika kikao maalum cha Maandalizi ya Maonesho ya Nanenane Kanda ya  Ziwa Mashariki , kilichofanyika Mjini Bariadi.
Mkuu wa Wilaya ya Itilima Mkoani Simiyu,  Mhe. Benson Kilangi akichangia hoja katika kikao cha viongozi na wataalam wa mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga  katika kikao maalum cha Maandalizi ya Maonesho ya Nanenane Kanda ya  Ziwa Mashariki , kilichofanyika i Mjini Bariadi.
Baadhi ya Wakurugenzi wa Halmashauri na Maafisa wakifuatilia kikao cha viongozi na wataalam wa mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga  katika kikao maalum cha Maandalizi ya Maonesho ya Nanenane Kanda ya  Ziwa Mashariki  inayohusisha mikoa kilichofanyika Mjini Bariadi.
Mkuu wa Wilaya ya Tarime mkoani Mara, Mhe.Glorius Luoga akichangia hoja katika kikao cha viongozi na wataalam wa mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga  katika kikao maalum cha Maandalizi ya Maonesho ya Nanenane Kanda ya  Ziwa Mashariki  inayohusisha mikoa hiyo kilichofanyika Mjini Bariadi.
Baadhi ya Viongozi wa Sekretarieti ya Mkoa na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya   Mkoa wa Simiyu wakifuatilia kikao cha viongozi na wataalam wa mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga  katika kikao maalum cha Maandalizi ya Maonesho ya Nanenane Kanda ya  Ziwa Mashariki  inayohusisha mikoa hiyo kilichofanyika Mjini Bariadi.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!