Thursday, May 24, 2018

RC MTAKA ASHAURI TFDA KUFUNGUA OFISI KATIKA MIKOA


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka ameishauri Mamlaka ya Chakula na Dawa hapa nchini (TFDA) kufungua Ofisi katika Mikoa ili kusogeza huduma karibu na wananchi na kuongeza ufanisi hususani katika kipindi hiki ambacho Serikali ya awamu ya Tano inahimiza utekelezaji wa ajenda ya Viwanda.

Mtaka ameyasema hayo Mei 23 wakati akifungua kikao kazi cha Wahariri na waandishi wa habari wa mikoa ya Simiyu na Mara kilicholenga kuhamasisha Sheria ya Chakula, dawa na vipodozi sura Na.219, ambacho kilifanyika Mjini Bariadi.

Amesema wakati huu ambao Sera ya Viwanda ni kipaumbele cha nchi ni vema Ofisi za TFDA zikawepo katika kila Makao Makuu ya  mkoa ili pale watu wanapotaka kujenga viwanda vitakavyozalishwa dawa, chakula na vipodozi waweze kupata huduma zinazotakiwa kwa wakati badala ya kufuata huduma katika ofisi za kanda.

“Mhe. Rais anapohimiza ajenda ya viwanda kwenye nchi TFDA inabidi ione umuhimu wa kuwa na Ofisi kwenye mikoa, ili mfano watu wa Simiyu wanapohitaji kufungua kiwanda cha bidhaa ambazo zinaihusu TFDA wasilazimike kwenda Mwanza kufauta huduma” alisema.

Aidha, Mtaka ameishauri Mamlaka ya Chakula na Dawa Nchini - TFDA  kutoa ufafanuzi wa mara kwa mara kuhusu dawa, chakula na vipodozi kupitia  vyombo vya habari,  ili jamii iweze kuwa na uelewa mpana wa madhara yatokanayo matumizi na bidhaa bandia na zenye madhara kwa binadamu.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa mkoa ametoa wito kwa waandishi wa habari baada ya kupata mafunzo kutoka TFDA kuwa mabalozi  wazuri wa TFDA katika kufafanua masuala yote yenye sintofahamu na kuandika habari za kiuchunguzi zilizofanyiwa utafiti kuhusu dawa, chakula na vipodozi.

Naye Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, Bi Agnes Sitta Kijo amewataka Waandishi wa habari kutoa taarifa pale wanapobaini uwepo bidhaa ambazo si salama kwa matumizi ya binadamu huku akiwasisitiza kujikita katika uandishi wa Habari za kiuchunguzi.

Baadhi ya washiriki wa kikao kazi hicho kutoka Mikoa ya Simiyu na Mara wamesema mafuzo waliyapata yamewasaidia kupata uelewa wa Sheria ya ya Chakula, dawa na vipodozi sura Na.219 na masuala mbalimbali yahusuyo chakula, dawa na vipodozi hivyo watakuwa mabalozi wazuri watakaowasaidia wananchi kupata uelewa juu ya masuala hayo.

“ Elimu niliyoipata imenisaidia na kupitia elimu hii kuhusu masuala ya chakula, dawa na vipodozi mimi kama mwandishi nitakuwa balozi mzuri ili kuwasaidia wananchi kujua madhara ya bidhaa zisizo salama kwa afya ya binadamu” alisema Shushu Joel kutoka Simiyu.

“Mafunzo haya yatatusaidia waandishi habari kujikita katika kuandika habari za kiuchunguzi zitakazowasaidia wananchi kujua madhara ya bidhaa zisizo salama kwa afya ya binadamu ” alisema Frankius Cleopas Mwandishi kutoka mkoani Mara.
MWISHO


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka akifungua kikao kazi cha Wahariri na waandishi wa habari wa mikoa ya Simiyu na Mara kilicholenga kuhamasisha wa sheria ya Chakula, dawa na vipodozi sura Na.219, ambacho kilifanyika Mjini Bariadi.




Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, Bi Agnes Sitta Kijo akizungumza na Wahariri na waandishi wa habari wa mikoa ya Simiyu na Mara katika kikao kazi kilicholenga kuhamasisha wa sheria ya Chakula, dawa na vipodozi sura Na.219, ambacho kilifanyika Mjini Bariadi
Baadhi ya Wahariri na waandishi wa habari wa mikoa ya Simiyu na Mara katika wakiwa katika kikao kazi kilicholenga kuhamasisha wa sheria ya Chakula, dawa na vipodozi sura Na.219, ambacho kilifanyika Mjini Bariadi.
Baadhi ya Wahariri na waandishi wa habari wa mikoa ya Simiyu na Mara katika wakiwa katika kikao kazi kilicholenga kuhamasisha wa sheria ya Chakula, dawa na vipodozi sura Na.219, ambacho kilifanyika Mjini Bariadi.
Kutoka kushoto Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, Bi Agnes Sitta Kijo, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka na Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe.Festo Kiswaga wakifuatilia kikao kazi cha wahariri na waandishi wa habari wa mikoa ya Simiyu na Mara kilicholenga kuhamasisha wa sheria ya Chakula, dawa na vipodozi sura Na.219, ambacho kilifanyika Mjini Bariadi.
Baadhi ya Maafisa kutoka Mamlaka ya Chakula na Dawa(TFDA) wakiteta jambo katika kikao kazi cha wahariri na waandishi wa habari wa mikoa ya Simiyu na Mara kilicholenga kuhamasisha wa sheria ya Chakula, dawa na vipodozi sura Na.219, ambacho kilifanyika Mjini Bariadi.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!