Thursday, May 17, 2018

MHIFADHI MKUU SERENGETI: UJENZI WA UWANJA WA NDEGE SIMIYU UTAONGEZA HUDUMA ZA UTALII

Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti (SENAPA), William Mwakilema amesema Uwanja wa Ndege Simiyu unaotarajia kujengwa  Eneo la Igegu wilayani Bariadi utakapokamilika  utaongeza huduma za Utalii katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.

Mwakilema ameyasema hayo wakati  ziara ya Balozi wa Indonesia  hapa nchini , Prof.Dkt. Ratlan Pardede na Viongozi wa Mkoa wa Simiyu katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti Mei 16  ili kujionea wanyama na vivutio mbalimbali vya utalii katika hifadhi hiyo.

Amesema Hifadhi ya Serengeti ina uwanja ambao unaowezesha ndege ndogo kutua hivyo, ujenzi wa uwanja wa Simiyu utakaowezesha  ndege kubwa kutua itakuwa ni nyongeza ya huduma, ambapo  ndege kubwa zitakapotua Simiyu watalii ambao hawawezi kutembea mwendo mrefu kwa kutumia magari, watachukuliwa na ndege ndogo kutoka Simiyu na  kupelekwa  Seronera(Serengeti).

Ameongeza kuwa,  kuwepo kwa uwanja huo kutasaidia kwa kiasi kikubwa kuboresha huduma za Utalii, ambapo wafanyabiashara wengi  wa huduma za Utalii watavutiwa kuwekeza mkoani Simiyu kwa ajili kutoa huduma kwa wageni watakaotua uwanjani hapo na wanaoenda kufanya utalii Serengeti.

Aidha, Mwakilema amesema Mamlaka ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti inaendelea kushirikiana na Mkoa wa Simiyu kuhakikisha kuwa rasilimali zote ndani ya hifadhi ziko salama na zinaendelea kutunzwa ili  Taifa liweze kunufaika kiuchumi kupitia utalii.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema Mpango wa Mkoa huo ni kufikisha kwa wepesi huduma za Utalii katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti hivyo mkoa umepanga kujenga uwanja huo wa ndege katika Eneo la Igegu wilayani Bariadi ambalo liko karibu kabisa na Hifadhi hiyo.

“Tumepanga kujenga Uwanja wa Ndege pale Igegu ili kufikisha huduma za utalii kwa wepesi katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na mwaka huu wa fedha 208/2019  tumetengewa fedha kwa ajili ya ujenzi wa uwanja huo  utakaokuwa na ukubwa wa kilometa 2.5,  pia sisi kama mkoa tutahakikisha tunafungua malango yote ya watalii kuja kwenye vivutio vyetu” alisema Mtaka

“Tunapokamilisha miundombinu ya barabara ya Lamadi-Bariadi-Maswa-Mwigumbi ni pamoja na kuona namna tutakavyounganisha  ufunguaji wa barabara zitakazowezesha watu kwenda kwenye hoteli zote za kitalii zilizojengwa ndani ya hifadhi hasa zilizo katika eneo letu, ili huduma za utalii zirahisishwe” alisisitiza.

Kwa upande wake Balozi wa Indonesia nchini Tanzania, Prof. Dkt. Ratlan Pardede  baada ya kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Serengeti amesema atazungumza na Wafanyabiashara wa Indonesia na kuwaalika kuwekeza katika Sekta ya Utalii nchini Tanzania hususani Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, huku akisisitiza kutoa wito kwa wananchi wa Indonesia kutembelea Hifadhi ya Serengeti ili kuja kujionea vivutio mbalimbali vya utalii.

Balozi wa Indonesia, Prof. Dkt. Ratlan Pardede amehitimisha ziara yake kikazi mkoani Simiyu ambapo ameahidi kuimarisha ushirikiano kati ya Indonesia na Tanzania na hasa Mkoa wa Simiyu katika masuala ya kilimo na biashara ya zao la pamba, uwekezaji wa viwanda vya nguo, bidhaa za ngozi na mbolea pamoja na utalii.

MWISHO

Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti (SENAPA), William Mwakilema akizungumza na Balozi wa Indonesia nchini Tanzania, Prof. Dkt. Ratlan Pardede  na Viongozi wa Mkoa wa Simiyu wakati wa ziara yao katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti Mei 16  ili kujionea wanyama na vivutio mbalimbali vya utalii katika hifadhi hiyo
Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti (SENAPA), William Mwakilema(kulia) akitoa maelezo  juu ya uwanja mdogo wa ndege  wa hifadhi hiyo (Seronera) kwa  Balozi wa Indonesia nchini Tanzania, Prof. Dkt. Ratlan Pardede  na Viongozi wa Mkoa wa Simiyu wakati wa ziara yao katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti Mei 16  ili kujionea wanyama na vivutio mbalimbali vya utalii katika hifadhi hiyo.
Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti (SENAPA), William Mwakilema (kushoto) akiwaongoza Balozi wa Indonesia nchini Tanzania, Prof. Dkt. Ratlan Pardede (katikati) na Viongozi wa Mkoa wa Simiyu kuelekea eneo la kupokea taarifa wakati wa ziara yao katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti Mei 16  ili kujionea wanyama na vivutio mbalimbali vya utalii katika hifadhi hiyo.
Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti (SENAPA), William Mwakilema (katikati) akiwaongoza Balozi wa Indonesia nchini Tanzania, Prof. Dkt. Ratlan Pardede (wa pili kulia) kuelekea eneo la kupokea taarifa wakati wa ziara yao katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti Mei 16  ili kujionea wanyama na vivutio mbalimbali vya utalii katika hifadhi hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti (SENAPA)  na baadhi ya viongozi wa Mkoa wa huo wakati wa ziara ya Balozi wa Indonesia hapa nchini, Prof. Dkt. Ratlan Pardede   na Viongozi wa Mkoa wa Simiyu katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti Mei 16  ili kujionea wanyama na vivutio mbalimbali vya utalii katika hifadhi hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (kulia) akiteta jambo na Balozi wa Indonesia hapa nchini, Prof. Dkt. Ratlan Pardede   wakati wa ziara ya Balozi huyo katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti Mei 16  ili kujionea wanyama na vivutio mbalimbali vya utalii katika hifadhi hiyo.  
Balozi wa Indonesia hapa nchini, Prof. Dkt. Ratlan Pardede   akizungumza na Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti (SENAPA), William Mwakilema na viongozi wa Mkoa wa Simiyu wakati wa ziara yake katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti Mei 16  ili kujionea wanyama na vivutio mbalimbali vya utalii katika hifadhi hiyo.
Balozi wa Indonesia hapa nchini, Prof. Dkt. Ratlan Pardede (kushoto)  akiangalia  wanyama  Mamba na Viboko katika Mto Grumeti wakati wa ziara yake katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti Mei 16  ili kujionea wanyama na vivutio mbalimbali vya utalii katika hifadhi hiyo.
Balozi wa Indonesia hapa nchini, Prof. Dkt. Ratlan Pardede katika picha ya pamoja mata baada ya kumaliza ziara  yake katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti Mei 16  ili kujionea wanyama na vivutio mbalimbali vya utalii katika hifadhi hiyo.
Baadhi ya Tembo waliopo Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ambao ni moja ya vivutio vya utalii katika hifadhi hiyo.



0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!