Friday, July 13, 2018

SERIKALI KUTOA SHILINGI BILIONI 1.5 UJENZI WA WODI YA MAMA NA MTOTO HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA SIMIYU


Serikali imetenga kiasi cha shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya ujenzi wa wodi ya mama na Mtoto katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa SIMIYU.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu Julai 12, 2018, mara baada ya kukagua ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje(OPD)  la Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu, ambapo ameridhishwa na ujenzi wa jengo hilo.

Waziri Ummy amewahakikishia viongozi wa mkoa wa Simiyu kuwa Serikali imetenga shilingi Bilioni 1.5 na wadau wengine wameahidi kutoa shilingi bilioni 1.1 kwa ajili ya kukamilisha wodi ya mama na mtoto.

“Simiyu katika bajeti ya Serikali imetengewa shilingi bilioni 1.5 lakini tumepata pia shilingi bilioni 1.1 kutoka kwa wafadhili kwa ajili ya ujenzi waWodi ya mama na mtoto katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu, lengo letu ni kukamilisha ujenzi haraka ili tuiwezeshe Halmashauri ya Mji wa Bariadi, kuchukua majengo ambayo yanatumika sasa hivi kama Hospitali Teule ya mkoa” alisema.

Katika hatua nyingine Waziri Ummy amesema baada ya kukamilisha ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa, Serikali ina mpango wa kujenga Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Ziwa Mashariki Mkoani Simiyu, itakayohudumia mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga  ili kuipunguzia mzigo Hospitali ya Rufaa ya Bugando ambayo inahudumia mikoa takribani minane.

Ameongeza kuwa pamoja na kuwa na mpango wa kujenga Hospitali ya hiyo Rufaa ya Kanda Simiyu, Serikali imekusudia kujenga Hospitali za Kanda tatu ambazo ni Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kusini ambayo imeanza kujengwa Mtwara, nyingine itajengwa Tabora Kanda ya Magharibi ili wananchi wapate matibabu ya kibingwa katika maeneo yao.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka ameishukuru Serikali kwa kutoa fedha za kujenga jengo hilo, ambazo zitasaidia kuboresha huduma za afya katika mkoa wa Simiyu .

Aidha, Mtaka amesema ardhi kwa ajili ya kujenga Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Ziwa Mashariki itatolewa bure na akamhakikishia Waziri Ummy ushirikiano wa asilimia 100 kila watakapokuwa wakihitajika kwa namna moja au nyingine ili kufanikisha ujenzi wa hospitali hiyo.

Pamoja na Serikali kuahidi kutoa shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya ujenzi wa wodi ya mama na Mtoto katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa SIMIYU,  pia Waziri Ummy amesema Serikali imetenga shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali yaWilaya ya Itilima.

MWISHO



Meneja wa Wakala wa Majengo nchini(TBA) Mkoa wa Simiyu.Mhandisi.Likimaitare Naunga (wa pili kulia) akimuonesha Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu(katikati) ramani ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa, mara baada ya Waziri Ummy kutembelea na kuona maendeleo ya Ujenzi wa Jengo la Wagonjwa wa Nje(OPD) la hospitali hiyo Mjini Bariadi, Julai12, 2018.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka akimuongoza  Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu , wakati alipotembelea  na kuona maendeleo ya Ujenzi wa Jengo la Wagonjwa wa Nje(OPD) la hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu Mjini Bariadi, Julai 12, 2018.
Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akisaini kitabu cha wageni  wakati alipotembelea  na kuona maendeleo ya Ujenzi wa Jengo la Wagonjwa wa Nje(OPD) la hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu Mjini Bariadi Julai 12, 2018.
Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akizungumza na viongozi wa Mkoa wa Simiyu wakati alipotembelea  na kuona maendeleo ya Ujenzi wa Jengo la Wagonjwa wa Nje(OPD) la hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu Mjini Bariadi Julai 12, 2018.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka (kulia) akitoa maelezo kwa Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati alipotembelea  na kuona maendeleo ya Ujenzi wa Jengo la Wagonjwa wa Nje(OPD) la hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu Mjini Bariadi, Julai 12, 2018.
Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu(wa nne kulia) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Mkoa wa Simiyu, mara baada ya kumaliza ziara yake ya kuona maendeleo ya Ujenzi wa Jengo la Wagonjwa wa Nje(OPD) la hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu Mjini Bariadi, Julai 12, 2018.
Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu(katikati) akifurahia jambo na viongozi wa Mkoa wa Simiyu wakati alipotembelea  na kuona maendeleo ya Ujenzi wa Jengo la Wagonjwa wa Nje(OPD) la hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu Mjini Bariadi, Julai 12, 2018.
Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu na viongozi wa Mkoa wa Simiyu wakitoka katika Jengo la Wagonjwa wa Nje(OPD) la Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu, mara baada Waziri Ummy  kutembelea na kuona maendeleo ya Ujenzi wa jengo hilo Mjini Bariadi, Julai 12, 2018.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka (kulia) akiteta jambo na Mkurugenzi wa Benjamin Mkapa Foundation, Dkt. Hellen Senkoro  wakati ziara ya Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu alipotembelea  na kuona maendeleo ya Ujenzi wa Jengo la Wagonjwa wa Nje(OPD) la Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu Mjini Bariadi Julai 12, 2018.
Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akizungumza na viongozi wa Mkoa wa Simiyu wakati alipotembelea  na kuona maendeleo ya Ujenzi wa Jengo la Wagonjwa wa Nje(OPD) la hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu Mjini Bariadi, Julai 12, 2018.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka akimuongoza  Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu , wakati alipotembelea  na kuona maendeleo ya Ujenzi wa Jengo la Wagonjwa wa Nje(OPD) la Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu Mjini Bariadi, Julai 12, 2018.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!