Wednesday, July 18, 2018

WAZIRI WA MIFUGO AONGOZA WAOMBOLEZAJI MEATU MAZISHI YA DIWANI SHUKIA ALIYEFARIKI KWA AJALI

Waziri wa mifugo na Uvuvi, Mhe. Luhaga Mpina amewaongoza wakazi wa Wilaya ya Meatu na Mkoa wa Simiyu katika mazishi ya aliyekuwa Diwani wa Kata ya Mwanhuzi wilayani Meatu Elias Shukia aliyefariki katika ajali ya gari Mkoani Singida akitokea Dodoma na kusababisha kifo chake na dereva na kusababisha watu wengine watano kujeruhiwa.
Ajali hiyo imetokea Julai 14 eneo la Mkiwa Wilaya ya Ikungi Mkoa wa Singida ,baada ya gari walilokuwa wakisafiria aina Toyota landcluser DFPA 0148 la Halmashauri ya Meatu kupasuka tairi na kupinduka mara tatu na kusababisha vifo hivyo viwili,huku majeruhi wa ajali hiyo Mkurugenzi Mtendaji, Mwenyekiti wa Halmashauri na Maafisa wa Halmashauri hiyo walipata majeruhi.
Mpina ametoa pole kwa familia, wananchi, Chama Cha Mapinduzi na Halmashauri ya Wilaya ya Meatu na kuwataka kuwa wavumilivu katika kipindi hiki kigumu kwa kuondokewa na madiwani watatu na dereva katika matukio mawili tofauti ya ajali na akawaomba wasifikiri kitu kingine tofauti juu ya kutokea kwa ajali hizo badala yake wajue kuwa ni mapenzi ya Mungu.
“ Kuna watu wanaweza wasiamini kuwa ajali zinaweza zikatokea Meatu kwa muda fupi hivi kama ilivyotokea kwetu, naomba ndugu zangu wananchi, viongozi tusiingie kwenye mtego huo tujue tu kuwa haya ni mapenzi ya Mungu kama walivyosema viongozi wetu wa dini kuwa Mungu ndiye anayejua hatma ya maisha yetu” alisema Mpina.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ametoa pole kwa familia, chama na wananchi kwa msiba huo na  amewaagiza Viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu kuhakikisha stahili zote za marehemu zinalipwa kwa wakati kwa familia ya marehemu.
Aidha, amewaomba viongozi wa dini kufanya maombi kwa ajili ya  wilaya ya Meatu na Mkoa wa Simiyu kwa ujumla kuomba Mwenyezi Mungu kuwaepusha viongozi na wananchi na mitihani ya ajali iliyotokea mfululizo.
“Wakati tunawaaga madiwani wetu wale wawili waliofariki kwenye ajali ya kwanza,  Mwenyekiti wa Halmashauri na madiwani wengine walikuwa kwenye matibabu , leo tunamuaga
Mhe. Shukia Mkurugezi na Mwenyekiti wako kwenye matibabu kwa sababu ya majeraha waliyoyapata katika ajali, sisi kama wanadamu tunaamini kwenye ulimwengu wa roho tuna nafasi ya kuomba, niwaombe viongozi wa dini tumwombe Mungu atuepushe na mitihani hii” alisema
Mbunge wa Jimbo la Meatu Salum Khamis amesema kifo cha mhe. Shukia  ni pigo kubwa kwa kata ya Mwanhuzi na Meatu kwa ujumla kwa kuwa marehemu Shukia enzi za uhai wake alikuwa mtetezi ndani ya Chama Cha Mapinduzi na wananchi katika shughuli za maendeleo.
Akitoa mahubiri wakati wa ibada ya Mazishi, Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Dayosisi ya Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria, Dkt. Emmanuel Makala aliwakumbusha waombolezaji wote kuishi wakimtegemea Mungu, kwa kuwa kila mtu hapa duniani anaishi kwa neema ya Mwenyezi Mungu, hivyo wanapaswa kuishi maisha ya kumpendeza Mungu.
Marehemu Shukia ameacha mke na watoto wanne, BWANA ALITOA , BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE. AMINA!

MWISHO

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Luhaga Mpina akiweka shada la maua katika kaburi la aliyekuwa Diwani wa Kata ya Mwanhuzi wilayani Meatu, Mhe.Elias Shukia ambaye alifariki dunia katika ajali ya gari Julai 14, mkoani Singida akitokea Dodoma kikazi,  baada ya mazishi ya diwani huyo yaliyofanyika Julai 17, 2018 wilayani Meatu.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe.Enock Yakobo akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa aliyekuwa Diwani wa Kata ya Mwanhuzi wilayani Meatu, Mhe.Elias Shukia ambaye alifariki dunia katika ajali ya gari Julai 14, mkoani Singida akitokea Dodoma kikazi, kabla ya mazishi ya diwani huyo yaliyofanyika Julai 17, 2018 wilayani Meatu.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa aliyekuwa Diwani wa Kata ya Mwanhuzi wilayani Meatu, Mhe.Elias Shukia ambaye alifariki dunia katika ajali ya gari Julai 14, mkoani Singida akitokea Dodoma kikazi, kabla ya mazishi ya diwani huyo yaliyofanyika Julai 17, 2018 wilayani Meatu.
Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Dayosisi ya Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria, Dkt. Emmanuel Makala akitoa sala wakati wa ibada ya mazishi aliyekuwa Diwani wa Kata ya Mwanhuzi wilayani Meatu, Mhe.Elias Shukia ambaye alifariki dunia katika ajali ya gari Julai 14, mkoani Singida akitokea Dodoma kikazi,  kabla ya mazishi ya diwani huyo yaliyofanyika Julai 17, 2018 wilayani Meatu.

Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Dayosisi ya Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria, Dkt. Emmanuel Makala na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka wakiteta jambo kwenye msiba wa aliyekuwa Diwani wa Kata ya Mwanhuzi wilayani Meatu, Mhe.Elias Shukia ambaye alifariki dunia katika ajali ya gari Julai 14, mkoani Singida akitokea Dodoma kikazi ,kabla ya mazishi ya diwani huyo yaliyofanyika Julai 17, 2018 wilayani Meatu.
Mbunge wa Meatu, Mhe. Salum Khamis akitoa salamu za rambirambi katika msiba wa aliyekuwa Diwani wa Kata ya Mwanhuzi wilayani Meatu, Mhe.Elias Shukia ambaye alifariki dunia katika ajali ya gari Julai 14, mkoani Singida akitokea Dodoma kikazi, kabla ya mazishi ya diwani huyo  yaliyofanyika Julai 17, 2018 wilayani Meatu.
Kutoka kushoto Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza, Mhe. Anthony Diallo,  Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Luhaga Mpina na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Meatu, Mhe.Juma Mwiburi wakiteta jambo jambo kwenye msiba wa aliyekuwa Diwani wa Kata ya Mwanhuzi wilayani Meatu, Mhe.Elias Shukia ambaye alifariki dunia katika ajali ya gari Julai 14, mkoani Singida akitokea Dodoma kikazi, kabla ya mazishi ya diwani huyo yaliyofanyika Julai 17, 2018 wilayani Meatu.
Vijana wa CCM na Vijana wa KKKT Meatu wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa Diwani wa Kata ya Mwanhuzi wilayani Meatu, Mhe.Elias Shukia ambaye alifariki dunia katika ajali ya gari Julai 14, mkoani Singida akitokea Dodoma kikazi kuelekea kwenye mazishi yaliyofanyika Julai 17, 2018 wilayani Meatu.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe.Enock Yakobo (kulia) na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza, Mhe. Anthony Diallo wakiweka shada la maua katika kaburi la aliyekuwa Diwani wa Kata ya Mwanhuzi wilayani Meatu, Mhe.Elias Shukia ambaye alifariki dunia katika ajali ya gari Julai 14, mkoani Singida akitokea Dodoma kikazi baada ya mazishi ya diwani huyo yaliyofanyika Julai 17, 2018 wilayani Meatu.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza, Mhe. Anthony Diallo akitoa salamu za rambirambi katika msiba wa aliyekuwa Diwani wa Kata ya Mwanhuzi wilayani Meatu, Mhe.Elias Shukia ambaye alifariki dunia katika ajali ya gari Julai 14, mkoani Singida akitokea Dodoma kikazi, kabla ya mazishi ya diwani huyo yaliyofanyika Julai 17, 2018 wilayani Meatu.
Kutoka kushoto Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Meatu, Mhe.Juma Mwiburi, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Maswa, Mhe. Paul Jidayi na Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Mhe. Dkt. Joseph Chilongani,  wakiteta jambo jambo kwenye msiba wa aliyekuwa Diwani wa Kata ya Mwanhuzi wilayani Meatu, Mhe.Elias Shukia ambaye alifariki dunia katika ajali ya gari Julai 14, mkoani Singida akitokea Dodoma kikazi, kabla ya mazishi ya diwani huyo yaliyofanyika Julai 17, 2018 wilayani Meatu.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza, Mhe. Anthony Diallo na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka wakiteta jambo kwenye  msiba wa aliyekuwa Diwani wa Kata ya Mwanhuzi wilayani Meatu, Mhe.Elias Shukia ambaye alifariki dunia katika ajali ya gari Julai 14, mkoani Singida akitokea Dodoma kikazi,  kabla ya mazishi ya diwani huyo yaliyofanyika Julai 17, 2018 wilayani Meatu.
Mama mzazi wa aliyekuwa Diwani wa Kata ya Mwanhuzi wilayani Meatu, Mhe.Elias Shukia ambaye alifariki dunia katika ajali ya gari Julai 14, mkoani Singida akitokea Dodoma kikazi, kabla ya mazishi ya diwani huyo yaliyofanyika Julai 17, 2018 wilayani Meatu.
Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Dayosisi ya Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria, Dkt. Emmanuel Makala akiongoza maombi ya kuuombea Mkoa wa Simiyu, wakati wa ibada ya mazishi ya aliyekuwa Diwani wa Kata ya Mwanhuzi wilayani Meatu, Mhe.Elias Shukia ambaye alifariki dunia katika ajali ya gari Julai 14, mkoani Singida akitokea Dodoma kikazi, kabla ya mazishi ya diwani huyo yaliyofanyika Julai 17, 2018 wilayani Meatu.
Baadhi ya viongozi wa Chama na Serikali wakiwa katika ibada ya mazishi ya aliyekuwa Diwani wa Kata ya Mwanhuzi wilayani Meatu, Mhe.Elias Shukia ambaye alifariki dunia katika ajali ya gari Julai 14, mkoani Singida akitokea Dodoma kikazi, kabla ya mazishi ya diwani huyo yaliyofanyika Julai 17, 2018 wilayani Meatu, ibada hiyo ilifanyika . Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Usharika wa Baraka Meatu.

Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Dayosisi ya Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria, Dkt. Emmanuel Makala akiteta jambo na viongozi wengine wa Dayosisi hiyo kwenye ibada ya mazishi ya aliyekuwa Diwani wa Kata ya Mwanhuzi wilayani Meatu, Mhe.Elias Shukia ambaye alifariki dunia katika ajali ya gari Julai 14, mkoani Singida akitokea Dodoma kikazi,  kabla ya mazishi ya diwani huyo yaliyofanyika Julai 17, 2018 wilayani Meatu.
Baadhi ya waombolezaji wakiwa katika ibada ya mazishi ya aliyekuwa Diwani wa Kata ya Mwanhuzi wilayani Meatu, Mhe.Elias Shukia ambaye alifariki dunia katika ajali ya gari Julai 14, mkoani Singida akitokea Dodoma kikazi, kabla ya mazishi ya diwani huyo yaliyofanyika Julai 17, 2018 wilayani Meatu.
Baadhi ya viongozi wa Chama na Serikali wakiungana na viongozi wa dini mkoa wa Simiyu, kuuombea Mkoa huo kabla ya mazishi ya aliyekuwa Diwani wa Kata ya Mwanhuzi wilayani Meatu, Mhe.Elias Shukia ambaye alifariki dunia katika ajali ya gari Julai 14, mkoani Singida akitokea Dodoma kikazi,  kabla ya mazishi ya diwani huyo yaliyofanyika Julai 17, 2018 wilayani Meatu.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akiweka shada la maua katika kaburi la aliyekuwa Diwani wa Kata ya Mwanhuzi wilayani Meatu, Mhe.Elias Shukia ambaye alifariki dunia katika ajali ya gari Julai 14, mkoani Singida akitokea Dodoma kikazi, baada ya mazishi ya diwani huyo yaliyofanyika Julai 17, 2018 wilayani Meatu.
Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Mhe. Dkt. Joseph Chilongani  akiweka shada la maua katika kaburi la aliyekuwa Diwani wa Kata ya Mwanhuzi wilayani Meatu, Mhe.Elias Shukia ambaye alifariki dunia katika ajali ya gari Julai 14, mkoani Singida akitokea Dodoma kikazi, baada ya mazishi ya diwani huyo yaliyofanyika Julai 17, 2018 wilayani Meatu.
Mbunge wa Jimbo la Meatu Salum Khamis akiweka shada la maua katika kaburi la aliyekuwa Diwani wa Kata ya Mwanhuzi wilayani Meatu, Mhe.Elias Shukia ambaye alifariki dunia katika ajali ya gari Julai 14, mkoani Singida akitokea Dodoma kikazi, baada ya mazishi ya diwani huyo yaliyofanyika Julai 17, 2018 wilayani Meatu.
Baadhi ya Viongozi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania wakiwa katika ibada ya mazishi ya aliyekuwa Diwani wa Kata ya Mwanhuzi wilayani Meatu, Mhe.Elias Shukia ambaye alifariki dunia katika ajali ya gari Julai 14, mkoani Singida akitokea Dodoma kikazi, kabla ya mazishi ya diwani huyo yaliyofanyika Julai 17, 2018 wilayani Meatu.
Baadhi ya wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Kanisa la Kiinjili Kilutheri Tanzania  Dayosisi ya Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria wakiweka shada la maua katika kaburi la aliyekuwa Diwani wa Kata ya Mwanhuzi wilayani Meatu, Mhe.Elias Shukia ambaye alifariki dunia katika ajali ya gari Julai 14, mkoani Singida akitokea Dodoma kikazi,  kabla ya mazishi ya diwani huyo yaliyofanyika Julai 17, 2018 wilayani Meatu.
Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Dayosisi ya Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria, Dkt. Emmanuel Makala akiweka shada la maua katika kaburi la aliyekuwa Diwani wa Kata ya Mwanhuzi wilayani Meatu, Mhe.Elias Shukia ambaye alifariki dunia katika ajali ya gari Julai 14, mkoani Singida akitokea Dodoma kikazi,  baada ya mazishi ya diwani huyo yaliyofanyika Julai 17, 2018 wilayani Meatu.
Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Dayosisi ya Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria, Dkt. Emmanuel Makala akiongoza ibada ya mazishi ya aliyekuwa Diwani wa Kata ya Mwanhuzi wilayani Meatu, Mhe.Elias Shukia ambaye alifariki dunia katika ajali ya gari Julai 14, mkoani Singida akitokea Dodoma kikazi, wakati wa  mazishi ya diwani huyo  yaliyofanyika Julai 17, 2018 wilayani Meatu.

Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Dayosisi ya Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria, Dkt. Emmanuel Makala akizungumza na waombolezaji katika msiba wa aliyekuwa Diwani wa Kata ya Mwanhuzi wilayani Meatu, Mhe.Elias Shukia ambaye alifariki dunia katika ajali ya gari Julai 14, mkoani Singida akitokea Dodoma kikazi kabla ya mazishi ya diwani huyo yaliyofanyika Julai 17, 2018 wilayani Meatu.
Baadhi ya ndugu wa aliyekuwa Diwani wa Kata ya Mwanhuzi wilayani Meatu, Mhe.Elias Shukia ambaye alifariki dunia katika ajali ya gari Julai 14, mkoani Singida akitokea Dodoma kikazi, wakisikiliza mahubiri ya viongozi wa dini  kabla ya mazishi ya diwani huyo yaliyofanyika Julai 17, 2018 wilayani Meatu..
Baadhi ya waombolezaji na ndugu wa aliyekuwa Diwani wa Kata ya Mwanhuzi wilayani Meatu, Mhe.Elias Shukia ambaye alifariki dunia katika ajali ya gari Julai 14, mkoani Singida akitokea Dodoma kikazi, wakisikiliza mahubiri ya viongozi wa dini  kabla ya mazishi ya diwani huyo yaliyofanyika Julai 17, 2018 wilayani Meatu.
Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Dayosisi ya Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria, Dkt. Emmanuel Makala akiongoza ibada ya mazishi ya aliyekuwa Diwani wa Kata ya Mwanhuzi wilayani Meatu, Mhe.Elias Shukia ambaye alifariki dunia katika ajali ya gari Julai 14, mkoani Singida akitokea Dodoma kikazi, kabla ya  mazishi ya diwani huyo  yaliyofanyika Julai 17, 2018 wilayani Meatu.
Mjane wa aliyekuwa Diwani wa Kata ya Mwanhuzi wilayani Meatu, Mhe.Elias Shukia ambaye alifariki dunia katika ajali ya gari Julai 14, mkoani Singida akitokea Dodoma kikazi, akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa mume wake, kabla ya mazishi yaliyofanyika Julai 17, 2018 wilayani Meatu.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,mhe.Anthony Mtaka akitoa salamu za rambirambi katika msiba wa aliyekuwa Diwani wa Kata ya Mwanhuzi wilayani Meatu, Mhe.Elias Shukia ambaye alifariki dunia katika ajali ya gari Julai 14, mkoani Singida akitokea Dodoma kikazi, kabla ya  mazishi ya diwani huyo  yaliyofanyika Julai 17, 2018 wilayani Meatu.


0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!