Wednesday, October 9, 2019

WANANCHI MKAJIANDIKISHE, MCHUKUE FOMU NA KUPIGA KURA UCHUGUZI SERIKALI ZA MITAA: RC MTAKA

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthnony Mtaka ametoa wito kwa wananchi wote wenye sifa mkoani hapa kwenda kujiandikisha katika daftari la orodha ya wapiga kura, kugombea nafasi mbalimbali na hatimaye kwenda kupiga kura katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika Novemba 24, 2019  ili wapate viongozi waadilifu.

Mtaka ametoa wito huo  wakati akizungumza na waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Petro Mwanhuzi wilayani Meatu, baada ya ibada ya misa takatifu Oktoba 06, 2019 ambapo alibainisha kuwa wananchi wanapaswa kuchagua viongozi waadilifu na wacahapakazi ambao watasimamia vizuri fedha za miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo yao.

“Kuanzia tarehe nane mwezi huu uandikishaji unaanza nendeni mkajiandikishe na wote wenye sifa chukueni fomu za kugombea nafasi mbalimbali  na kujitokeza kupiga kura siku ya tarehe 24 Novemba ili mpate viongozi bora, tumekuwa tunapata migogoro mingi ya ardhi, fedha za miradi kutotumika inavyotakiwa na moja ya sababu ni vongozi wasio waadilifu, kajitokezeni mchague waadilifu, “ alisema.

Katika hatua nyingine Mtaka ametoa wito kwa wananchi mkoani Simiyu kusomesha watoto wao  na kuona umuhimu wa kuchangia ujenzi wa miundombinu ya elimu ikiwemo vyumba vya madarasa na mabweni ambayo yatawapunguzia watoto wa kike kutembea mwendo mrefu.

Akitoa shukrani kwa niaba ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Petro Mwanhuzi wilayani Meatu, Paroko Robert Walwa amesemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kusisitiza umuhimu wa kupenda elimu jambo ambalo amesema hata Biblia Takatifu imesisitiza kuishika elimu maana ndiyo chimbuko la imani,  hivyo  ni vema wananchi wakazingatia elimu ili imani zao ziimarishwe.

Naye mmoja wa waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Petro Mwanhuzi aliyejitambulisha kwa jina moja la Jennifer amesema wananchi wanamshukuru Mkuu wa Mkoa kwa jitihada anazozifanya katika mkoa ambazo zimekusudia kuinua mkoa kielimu na akabainisha kuwa watashirikiana na Serikali katika kuhakikisha malengo ya kuinua sekta ya Elimu yanatimia ikiwemo kuongeza ufaulu.

Kuhusu Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Bi. Jeniffer amesema atahakikisha anajiandikisha na kupiga kura siku ikifika ili aweze kutumia vema haki yake ya msingi ya kuchagua kiongozi anayemtaka na si wa kuchaguliwa na watu wengine.
MWISHO
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Petro Mwanhuzi wilayani Meatu, baada ya ibada ya misa takatifu Oktoba 06, 2019.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(mwenye suti kulia) na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania(TRC), Bw. Masanja Kadogosa(wa pili  kulia) pamoja na baadhi ya viongozi na watumishi wa Serikali  wakiwa katika ibada ya misa takatifu Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Petro Mwanhuzi wilayani Meatu 06, 2019 pamoja na waumini wa kanisa hilo.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(mwenye suti kulia) na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania(TRC), Bw. Masanja Kadogosa(wa pili  kulia) pamoja na baadhi ya viongozi na watumishi wa Serikali  wakiwa katika ibada ya misa takatifu Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Petro Mwanhuzi wilayani Meatu 06, 2019 pamoja na waumini wa kanisa hilo.
Baadhi ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Petro Mwanhuzi wilayani Meatu wakifuatilia ibada ya misa takatifu hapo jana Oktoba 06, 2019 ibada ambayo pia ilihudhuriwa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania(TRC), Bw. Masanja Kadogosa(hawapo pichani).
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania(TRC), Bw. Masanja Kadogosa akizungumza na waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Petro Mwanhuzi wilayani Meatu, baada ya ibada ya misa takatifu Oktoba 06, 2019.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Komredi. Enock Yakobo akizungumza na waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Petro Mwanhuzi wilayani Meatu, baada ya ibada ya misa takatifu Oktoba 06, 2019 (kushoto) Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka .
Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Pertro Mjini Mwanhuzi Meatu, Robert Walwa na Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Yohana ya Mjini Bariadi, Kizito Victor  wakiongoza ibada ya misa takatifu katika Parokia ya Mtakatifu Pertro Mjini Mwanhuzi Meatu, jana Oktoba 06, 2019.
Baadhi ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Petro Mwanhuzi wilayani Meatu, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(mwenye suti kulia) na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania(TRC), Bw. Masanja Kadogosa(wa pili  kulia)wakifuatilia ibada ya misa takatifu hapo jana Oktoba 06, 2019 ibada ambayo pia ilihudhuriwa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania(TRC), Bw. Masanja Kadogosa(hawapo pichani).

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!