Thursday, July 25, 2019

MAKAMU WA RAIS KUFUNGUA MAONESHO YA NANENANE KITAIFA 2019 MKOANI SIMIYU


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan anatarajia kuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019, yatakayofanyika Kanda ya Ziwa Mashariki katika Viwanja vya Nyakabindi Mjini Bariadi kuanzia tarehe 29/07/2019 hadi 08/08/2019.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka wakati akizungumza na waandishi wa habari  katika mkutano maalum wa kutoa taarifa kwa Umma uliofanyika  Mjini Bariadi, Julai 24, 2019.

Mtaka amesema Mhe Makamu wa Rais atafungua rasmi maonesho hayo Agosti Mosi, 2019 na waoneshaji mbalimbali zikiwemo Taasisi, Mashirika mbalimbali na wajasiriamali wataanza kuonesha teknolojia, huduma na bidhaa zao Julai 29, 2019 ikiwa ni maandalizi ya ufunguzi rasmi utakaofanywa na Mhe. Makamu wa Rais.

“Shughuli ya ufunguzi itafanywa tarehe 01/08/2019 na Mhe. Makamu wa Rai, haya ni maonesho ambayo yatakaribisha viongozi wa Kitaifa, Agosti 03, 2019 tutakuwa na Mhe. Waziri Mkuu, Agosti 06, 2019 tutakuwa na Waziri Mkuu Mstaafu, Mizengo Pinda na Kilele tunatarajia kuwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli” alisema.

Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Omary Mgumba amesema ameridhishwa na maandalizi ya Maonesho ya nanenane yanayoendelea mkoani Simiyu na kutoa wito kwa wakulima na wananchi wote kwa ujumla kujitokeza kwa wingi kushiriki katika maonesho haya ili kuja kujionea teknolojia mbalimbali zitakazojibu changamoto za wakulima, wafugaji na wavuvi.

Aidha, Mhe. Mgumba ametoa wito kwa waoneshaji kuwa wabunifu katika teknolojia, huduma na bidhaa watakazoonesha ili maonesho haya yawe  chachu ya kuwasaidia wakulima, wavuvi na wafugaji  kuongeza tija katika uzalishaji

Naye Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mhe. Adam Malima amesema matarajio ya mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga inayounda Kanda ya Ziwa Mashariki ni kuwa na maonesho ya tofauti na mwaka jana, lengo likiwa ni kuifanya kanda hiyo kuwa ni mahali pa kudumu pa wakulima, wafugaji na wavuvi kuwa na maonesho ya kilimo biashara.

Maonesho ya Nanenane Kitaifa yanafanyika kwa mara ya pili sasa mkoani Simiyu tangu Kanda ya Ziwa ilipogawanywa katika kanda mbili yaani, Kanda ya Ziwa Mashariki(Simiyu, Mara na Shinyanga) na Kanda ya Ziwa Magharibi(Mwanza, Geita na Kagera) ambapo mwaka huu yanaadhimishwa chini ya kauli Mbiu:-“KILIMO, MIFUGO NA UVUVI KATIKA UKUAJI WA UCHUMI WA NCHI”
MWISHO
Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Omary Mgumba (kulia) akikagua moja ya kitalu nyumba wakati wa ziara ya kukagua maandalizi ya Maonesho ya  Nanenane Kitaifa mwaka 2019 yatakayofanyika kuanzia Julai 28, 2019 Viwanja vya Nyakabindi Bariadi.
Mtaalam kutoka JKT (kulia) akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Omary Mgumba (katikati) wakati akikagua moja ya tanki la ufugaji wa samaki wakati wa ziara ya kukagua maandalizi ya Maonesho ya  Nanenane Kitaifa mwaka 2019 yatakayofanyika kuanzia Julai 28, 2019 Viwanja vya Nyakabindi Bariadi.
Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Omary Mgumba (kulia) akikagua baadhi ya vipando wakati wa ziara ya kukagua maandalizi ya Maonesho ya  Nanenane Kitaifa mwaka 2019 yatakayofanyika kuanzia Julai 28, 2019 Viwanja vya Nyakabindi Bariadi.
Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Omary Mgumba (kulia) akipokea maelezo kutoka kwa Afisa wa JKT akikagua baadhi ya vipando wakati wa ziara ya kukagua maandalizi ya Maonesho ya  Nanenane Kitaifa mwaka 2019 yatakayofanyika kuanzia Julai 28, 2019  Viwanja vya Nyakabindi Bariadi.
Baadhi ya vipando vilivyo katika Viwanja vya Maonesho ya  Nanenane Kanda ya Ziwa Mashariki vilivyopandwa kwa ajili ya maandalizi ya  Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 .
Mtaalam kutoka JKT (kulia) akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Omary Mgumba (katikati) wakati akikagua moja ya Bwawa la ufugaji wa samaki wakati wa ziara ya kukagua maandalizi ya Maonesho ya  Nanenane Kitaifa mwaka 2019 yatakayofanyika kuanzia Julai 28, 2019 Viwanja vya Nyakabindi Bariadi.
Mtaalam kutoka JKT (kulia) akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Omary Mgumba wakati akikagua moja ya tanki la ufugaji wa samaki wakati wa ziara ya kukagua maandalizi ya Maonesho ya  Nanenane Kitaifa mwaka 2019 yatakayofanyika kuanzia Julai 28, 2019 Viwanja vya Nyakabindi Bariadi.
Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mhe. Adam Kighoma Malima(kulia) akizungumza katika kikao cha Kamati ya maandalizi ya Maonesho ya Nanenane Kitaifa 2019 Kanda ya Ziwa Mashariki, kilichofanyika Julai 23, 2019 katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi, (kushoto) ni Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka.
Moja ya vipando vya mazao ya kilimo  katika viwanja vya Nanenane Nyakabindi 
Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Omary Mgumba (kushoto) akiwa ameambatana na viongozi wengine wa Mkoa wa Simiyu na Wizara ya Kilimo wakati akikagua ujenzi wa majego ya kudumu katika VIwanja wa Nananenane Nyakabindi Bariadi

Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Omary Mgumba akikagua vipando vya mazao ya iilimo katika viwanja vya Nanenane Nyakabindi, Julai 25, 2019.
Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Omary Mgumba akikagua vipando vya mazao ya iilimo katika viwanja vya Nanenane Nyakabindi, Julai 25, 2019.


0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!