Sunday, July 14, 2019

SIMIYU KUANZISHA KAMPENI YA TOHARA KWA WATOTO WACHANGA


Serikali mkoani Simiyu kwa kushirikiana na wadau Shirika liliso la kiserikali la InterHelath imeanzisha huduma ya tohara kinga kwa watoto wachanga na tayari zoezi hilo limekwishaanza wilaya ya Meatu ambapo wataalam wanaotoa huduma hiyo wamekwishapatiwa mafunzo.

Matarajio ya serikali ni kusambaza huduma hiyo ya tohara kinga kwa watoto wachanga kwenye wilaya zote mkoani hapo ili huduma hiyo ipatikane kiurahisi na kwa wakati na kulifanya zoezi hili kuwa utamaduni ili jamii ione umuhimu wake tangu mtoto akiwa mdogo .

Hayo yamesemwa na mratibu wa kudhibiti UKIMWI mkoa wa Simiyu Dkt Khamis Kulemba Julai 12, 2019  wakati akiongea na waandishi wa habari katika mahojiano maalum matra baada ya kuhitimishwa kwa kikao cha wadau wa AFya kilichofanyika Mjini Bariadi.

Ameongeza  kuwa awali zoezi la tohara lilikuwa la hiari kwa wanaume waliokuwa bado hawajafanyiwa huduma hiyo ambapo amesema lilipokelewa kwa mwititiko mkubwa  hivyo ikaonekana ipo haja na umuhimu wa kutoa huduma hiyo tangu mtoto akiwa mdogo ili kuwa na kizazi kijacho kilichopata huduma hiyo .

“kwa kipindi cha mwaka 2017/18 mpango wa tohara ya hiari kwa wanaume  ulijikita katika  halmashauri ya  Bariadi, halmashauri ya  Itilima na halmashauri ya  Meatu  kama mkoa tulikuwa tunataka tutoe tohara kinga kwa wanaume takribani 59,129 kuanzia Oktobar 2018  na kila halmashauri ina lengo lake kwa  kwa Bariadi lengo   lilikuwa kutahiri zaidi ya wanaume 20,440  lakini tulifanikiwa kutahiri wanaume 17,165 sawasawa na 84%,  alisema Dkt Kulemba na kuongeza kuwa:

“kwa wilaya ya Itilima lengo lilikuwa kuwafikia  kina baba wapatao 22,176  lakini mpaka tarehe 30 june tuliwafikia wanaume 16,621 sawasawa  na asilimia 75 , kwa wilaya ya Meatu tumekwenda mbali kidogo  lengo la lilikuwa kuwafikia wanaume  16,513  na mpaka mwisho wa mwezi wa sita  tarehe 30 tumewafikia wanaume 15,165 sawasawa na 92%  kwa mkoa mzima  tumeshawafikia wanaume 48,951  sawa na 82% aliongeza Dkt Kulemba”

Aidha Dkt Kulemba  ameongeza kuwa kwa  mujibu wa tafiti zilizofanyika nchini Kenya ,Uganda  na Afrika Kusini  maeneo mengi ambayo tohara kwa wanaume ni utamaduni wao maambukizi ya UKIMWI yapo chini ikilinganishwa na maeneo ambayo tohara ipo chini maambukizi yapo juu.

“maeneo ambayo tohara ni culture(utamaduni) yao maambukizi  ya virusi vya ukimwi yapo chini lakini kupitia wizara ya afya kwa kushirikiana na shirika la Interhealth hayo yote yameweza kufanyika na ndio maana tukapata matokeo haya ” alisema Dkt Kulemba .

MWISHO.




Mratibu wa Shughuli za Kudhiti na kupambana na UKIMWI, Dkt. Khamis Kulemba akiwasilisha mada katika kikao cha wadau wa afya, kilichofanyika kilichofanyika Mjini Bariadi JulaI 11 na 12, 2019.
Baadhi ya viongozi na wadau wa afya mkoani Simiyu wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga, katika kikao cha wadau hao, kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka kilichofanyika Mjini Bariadi JulaI 11 na 12, 2019.
Mkuu wa wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga akizungumza na wadau wa afya mkoani Simiyu wakati akifunga kikao cha wadau hao, kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka kilichofanyika Mjini Bariadi JulaI 11 na 12, 2019.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!