Thursday, July 4, 2019

MEATU YATAKIWA KUBUNI VYANZO VIPYA VYA MAPATO NA KUONGEZA VITUO VYA BIASHARA


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Meatu kubuni vyanzo vipya vya mapato na kuongeza vituo vingine vya biashara  ili iweze kuongeza hali ya ukusanyaji wa mapato.

Mkuu wa Mkoa huyo aliyasema hayo jana wakati akizungumza na madiwani na watendaji wa Halamshauri hiyo kwenye kikao cha Baraza maalumu la madiwani llililokuwa na agenda moja ya  kujadili hoja 21 za ukaguzi zilizoibuliwa na mkaguzi na mthibiti mkuu wa hesabu za serikali(CAG).

“ Anzisheni vyanzo vipya vya mapato lakini pia fungueni miji mipya ya kibiashara mfano kule Bukundi daraja limeshajengwa hatuwezi kujenga daraja la Sabaiti halafu kukaendelea kuwa pori, ni lazima Bukundi uwe mji mwingine wa kibiashara kama Mwandoya, Mwanhuzi na ‘centres’ nyingine na karibisheni sekta binafsi” alisema.

Katika hatua nyingine amewakaribisha wafanyabiashara wa mabasi kupeleka magari yao Meatu ili kuwarahisishia wananchi huduma za usafiri kwenda Makao makuu ya mkoa na kuondoa changamoto ya usafiri iliyopo ambapo ni kampuni moja tu inayofanya kazi wilayani humo na akawaasa polisi kutojihusisha na uonevu dhidi ya wafanyabiashara na wananchi.

Kuhusu hoja za ukaguzi zilizoibuliwa na wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka ameitaka Halmashauri ya wilaya ya Meatu kujibu hoja za ukaguzi zilizoibuliwa na mkaguzi na mthibiti mkuu wa hesabu za serikali (CAG)kuhakikisha zinajibiwa kwa wakati na kwa ufasaha huku akiwataka wataalam kutoa ushirikiano kwa mkaguzi wa ndani.

Mtaka pia amemtaka mkaguzi wa ndani wa Halmashauri hiyo kuwa jicho ili aisaidie halmashauri hiyo wakati wakitekeleza miradi mbalimbali huku akisisitiza hoja zijibiwe kwa wakati bila ubabaishaji zikienda sambamba na  viambatanisho vya  vielelezo vinavyojitosheleza.

Fabian Manoza ni mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo ameahidi kuyafanyia kazi maelekezo yaliyotolewa na mkuu wa mkoa huo na kuhalikisha wanatoa ushirikiano wa kutosha kwa mkaguzi wa ndani .

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Pius Machungwa alisema kwa mwaka 2016/2017 mkaguzi na mthibiti Mkuu  10 wa hesabu za serikali aliibua hoja za ukaguzi 91 ambapo walipata hati ya mashaka, hivyo kwa mwaka huu wametekeleza baadhi ya mapendekezo na kuwafanya kupata hati safi.

Alisema kwa mwaka huu (2017/18) mkaguzi ameibua hoja za ukaguzi 24 na kuifanya halmashauri hiyo kupata hati safi huku akiahidi kusimamia miradi ili waendelee kupata hati safi na pia kumtumia mkaguzi wa ndani katika usimamizi wa miradi

Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Fabian Manoza alisema hoja nyingi zilitokana na mambo ya ndani ambayo watendaji walitakiwa kuyadhibiti hasa yatokanayo na ukusanyaji wa mapato ambapo wameanza kukusanya mapato kwa mfumo wa kielektroniki (EFD).

Manoza alisema watamtumia mkaguzi wa ndani wanapotekeleza miradi ili endapo akibaini kuna mapungufu aweze kuwajulisha na wayafanyie kazi.
MWISHO


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na Madiwa wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu wakati wa Kikao maalum cha Baraza la Madiwani chenye lengo la kujadili hoja za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa mwaka 2017/2018 .
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu, Mhe. Pius Machungwa  akifungua Kikao maalum cha Baraza la Madiwani chenye lengo la kujadili hoja za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa mwaka 2017/2018 .
Mkurugenzi wa Mtendaji wa Halmashauri ya Meatu, bw. Fabian Manoza  akiwasilisha taarifa katika Kikao maalum cha Baraza la Madiwani chenye lengo la kujadili hoja za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa mwaka 2017/2018 .
Baadhi ya madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu wakimsikiliza Mkuu wa mkoa wa Simiyu, MHE. Anthony Mtaka (hayupo pichani) katika Kikao maalum cha Baraza la Madiwani chenye lengo la kujadili hoja za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa mwaka 2017/2018.
Baadhi ya madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu wakimsikiliza Mkuu wa mkoa wa Simiyu, MHE. Anthony Mtaka (hayupo pichani) katika Kikao maalum cha Baraza la Madiwani chenye lengo la kujadili hoja za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa mwaka 2017/2018.


Baadhi ya wakuu wa idara wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu wakimsikiliza Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (hayupo pichani) katika Kikao maalum cha Baraza la Madiwani chenye lengo la kujadili hoja za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa mwaka 2017/2018.
Baadhi ya viongozi wa Serikali(mbele) wakifuatilia kikao maalum cha Baraza la Madiwani katika Halmashauri ya Wilaya ya Meatu chenye lengo la kujadili hoja za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa mwaka 2017/2018.
Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu, mhe. Juma Mpina akichangia hoja katika Kikao maalum cha Baraza la Madiwani chenye lengo la kujadili hoja za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa mwaka 2017/2018.


0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!