Sunday, August 12, 2018

JKT KUJENGA MAJENGO YA KUDUMU UWANJA WA NANENANE SIMIYU MWISHONI MWA MWAKA 2018

Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) limewahakikishia viongozi wa Mkoa wa Simiyu kuwa litaanza kujenga majengo ya kudumu katika Uwanja wa Nanenane Nyakabindi Bariadi mkoani humo, mwishoni mwa mwaka 2018.

Haya yamesemwa na Mwakilishi wa Mkuu wa JKT, Meja Jenerali Martin Busungu, Luteni Kanali Respicious Kaiza wakati Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Simiyu na viongozi wa Wilaya ya Bariadi wakiagana na baadhi ya viongozi  na Maafisa wa JKT katika Uwanja wa Nanenane Nyakabindi mara baada ya kukamilisha siku tatu za nyongeza za maonesho ya nanenane  zilizotolewa na Waziri wa Kilimo, Dkt. Charles Tizeba, wakati akifungua maonesho hayo Kitaifa mwaka 2018, mkoani Simiyu.

Luteni Kanali Kaiza amesema viongozi wa JKT wameondoka Nyakabindi Uwanja wa Nanenane kwa lengo la kwenda kujipanga ili waondokane na majengo ya kuhamisha na kuanza ujenzi wa majengo ya kudumu katika uwanjauwanja huo katika maonesho yajayo. 

"Tutaka kwenda kujipanga baada ya muda kidogo tutarudi kuanza rasmi ujenzi wa majengo ya kudumu ili tusiwe na majengo haya ambayo ni ya kuhamisha, Mungu akijalia mwishoni mwa mwaka huu tunataka tuwe tumeshaanza kujenga"'alisema.

Aidha, Luteni Kanali Kaiza amesema pamoja na viongozi na Maafisa wa JKT kuondoka Uwanjani hapo, vijana wa JKT pamoja na viongozi wa JKT waliokuwepo katika Kambi ya Nyakabindi wakati wa Maonesho ya Nanenane watabaki katika Eneo hilo la Nyakabindi kuendeleza shughuli walizozianzisha katika Uwanja huo.

 Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema dhamira ya Mkoa huo ni kuwa na  Maonesho ya Nanenane ya Kimataifa hivyo amewaomba viongozi wa JKT kuona uwezekano wa kujenga majengo makubwa zaidi ya yaliyotumika mwaka huu kwa kuwa mwaka 2019 watu zaidi ya 100,000 wanatarajiwa kushiriki maonesho ya nanenane na akawaomba pia waone uwezekano wa kuanza kujenga majengo hayo mapema kuanzia mwezi Oktoba, 2018.

Mtaka ametoa wito kwa JKT pia kujenga hoteli, hosteli, kumbi za mikutano na miundombinu mingine muhimu katika eneo la Nykabindi kwa kuwa eneo hilo litatumika kwa maonesho ya nanenane, maonesho ya kilimo biashara kila baada ya miezi mitatu na Vyuo vingi vya Elimu ya Juu vitajengwa karibu na eneo hilo, hivyo majengo hayo yakijengwa yatasaidia na kurahisisha kutoa huduma katika eneo hilo.

Aidha, amesema Serikali imeandaa utaratibu wa kuliendeleza eneo la Uwanja wa Nyakabindi ambapo itatoa nafasi kwa vijana, watumishi wa Umma walio tayari kufanya shughuli zao katika kilimo na mifugo kwa usimamizi wa Wataalam wa Kilimo na mifugo ili liweze kutumika kwa manufaa.

Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini ameshauri kwa kuwa JKT  liwekeze katika ujenzi wa  hoteli na hosteli katika eneo la Nyakabindi  kwa kuwa ina nguvu kazi  ili watu wanapokuja kwenye maonesho wapate huduma ya malazi kwa urahisi ndani ya mkoa badala ya kutoka nje,  lakini pia JKT waweze  kufanya biashara kupitia uwekezaji huo.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Bw. Melckizedeck Humbe amesema uwepo wa JKT utachangia mji huo kukua kwa kasi, huku akibanisha kuwa Halmashauri inatarajia kupima viwanja katika eneo la Nyakabindi lengo ni kufanya JKT na wawekezaji mbalimbali kujenga miundombinu yote muhimu karibu na Uwanja wa Nanenane ikiwemo vituo vya mafuta, hoteli, kumbi na hosteli.
MWISHO



Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(kushoto) akiteta jambo na Mwakilishi wa Mkuu wa Jesho la Kujenga Taifa( JKT), Meja Jenerali Martin Busungu, Luteni Kanali P.M.Kaiza katika kikao kifupi kabla ya Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Simiyu,Viongozi wa Wilaya ya Bariadi na baadhi ya Viongozi na Maafisa wa JKT waliokuwepo Uwanja wa Nyakabindi Halmashauri ya Mji wa Bariadi kuagana hapo jana, baada ya kukamilisha siku tatu za nyongeza ya maonesho ya nanenane zilizomalizika Agosti 11.
Mwakilishi wa Mkuu wa JKT Meja Jenerali Martin Busungu, Luteni Kanali P.M. Kaiza akizungumza na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Simiyu, Viongozi wa Wilaya ya Bariadi, baadhi ya viongozi na Maafisa wa JKT waliokuwepo Uwanja wa Nyakabindi Halmashauri ya Mji wa Bariadi kuagana  hapo jana, baada ya kukamilisha siku tatu za nyongeza ya maonesho ya nanenane zilizomalizika Agosti 11. 
Katibu Tawala wa mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini (kushoto) akiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo  Kiswaga katika kikao kifupi kabla ya Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Simiyu, Viongozi wa Wilaya ya Bariadi na baadhi ya viongozi na Maafisa wa JKT waliokuwepo Uwanja wa Nyakabindi Halmashauri ya Mji wa Bariadi kuagana hapo jana, baada ya kukamilisha siku tatu za nyongeza ya maonesho ya nanenane zilizomalizika Agosti 11.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Bw. Melckizedeck Humbe akizungumza na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Simiyu, Viongozi wa Wilaya ya Bariadi, baadhi ya viongozi na Maafisa wa JKT waliokuwepo Uwanja wa NnaneNyakabindi Halmashauri ya Mji wa Bariadi kuagana  hapo jana, baada ya kukamilisha siku tatu za nyongeza ya maonesho ya nanenane zilizomalizika Agosti 11.

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, Mhandisi Wilbert Siogopi akizungumza na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Simiyu, Viongozi wa Wilaya ya Bariadi, baadhi ya viongozi na Maafisa wa JKT waliokuwepo Uwanja wa Nanenane Nyakabindi Halmashauri ya Mji wa Bariadi kuagana  hapo jana, baada ya kukamilisha siku tatu za nyongeza ya maonesho ya nanenane zilizomalizika Agosti 11.
Mwakilishi wa Mkuu wa Jesho la Kujenga Taifa( JKT), Meja Jenerali Martin Busungu, Luteni Kanali P.M.Kaiza( wa tano kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Simiyu,Viongozi wa Wilaya ya Bariadi katika Uwanja wa Nyakabindi Halmashauri ya Mji wa Bariadi baada ya kikao kifupi na kuagana hapo jana, baada ya kukamilisha siku tatu za nyongeza ya maonesho ya nanenane zilizomalizika Agosti 11.
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Simiyu, Kamishna Mwanamizi wa Polisi  Deusdedit Nsimeki  akizungumza katika kikao kifupi kati ya  Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Simiyu, Viongozi wa Wilaya ya Bariadi, baadhi ya viongozi na Maafisa wa JKT waliokuwepo Uwanja wa Nanenane Nyakabindi Halmashauri ya Mji wa Bariadi kabla ya kuagana  hapo jana, baada ya kukamilisha siku tatu za nyongeza ya maonesho ya nanenane zilizomalizika Agosti 11.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!