Tuesday, August 21, 2018

SIMIYU YAJIPANGA KUUFANYA MRADI WA UMWAGILIAJI MWASUBUYA KUWA WA MFANO, KUBADILISHA MAISHA YA WANANCHI

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema Serikali mkoani humo imedhamiria kuutumia Mradi wa Uwagiliaji wa Mwasubuya kubadilisha maisha ya wananchi wilayani Bariadi, kupitia kilimo cha kisasa kinachotumia zana za kisasa na kuufanya kuwa mradi wa mfano ambao watu wateanda kujifunza.


Mtaka ameyasema hayo katika kikao cha tathmini ya Maonesho ya Nanenane mwaka 2018 yaliyofanyika Kitaifa mkoani Simiyu na kuwashukuru viongozi wa Chama na Serikali, Watendaji, Watumishi, wafanyabiashara na wadau wengine waliofanikisha maonesho hayo, kilichofanyika Mjini Bariadi.

Amesema mradi huo wenye ekari 514 zitakazolimwa kupitia Kilimo cha Umwagiliaji kwa kutumia maji ya Bwawa la Mwasubuya lililoigharimu Serikali shilingi bilioni 1.24, utahusisha kilimo cha kisasa chenye kutumia zana za kisasa katika hatua zote kuanzia kuandaa shamba, kupanda, palizi na kuvuna badala ya kuhusisha zana za kilimo za mikono.

“ Nimewaambia watu wa Bariadi tunahitaji Kijiji kimoja ambacho tutabadilisha maisha ya wananchi na watu wataenda kujifunza na kuangalia transformation(mabadiliko) ya kile kijiji, lakini pia tunahitaji lile shamba lote la ekari 514 lilimwe pasipo kutumia mikono ya wanadamu kuanzia hatua za kuandaa shamba, kupanda, palizi hadi kuvuna” alisema

Ameongeza kuwa dhamira ya Mkoa ni kuona wananchi wanalima kisasa kwa kutumia zana bora za kilimo ambazo baada ya mazungumzo na Kampuni ya Agricom Africa  imekubali kuikopesha Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi zana zote muhimu ili kuwawezesha wakulima katika mradi wa Mwasubuya kuongeza tija katika uzalishaji.

Aidha, Mtaka amesema Bwawa la Mwasubuya lililopo katika Mradi huu wa Umwagiliaji wa  Mwasubuya wilayani Bariadi litawekewa vifaranga vya samaki vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni kumi.

"Huu ni mradi ambao tungehitaji watu wote ndani ya mkoa waende wakaangalie transformation(mabadiliko) ya kile kijiji, lile bwawa tutaliwekea vifaranga vya samaki vya zaidi ya shilingi milioni kumi na tutalifunga mpaka mwezi Agosti 2019, uongozi utakaokuja mwakani kwenye Nanenane moja ya eneo watakalotembelea ni bwawa la Mwasubuya na tutafanya shughuli ya uvuaji wa hao samaki" alisema Mtaka.

Ameongeza kuwa Watumishi na wananchi wa Bariadi watahamasishwa kwenda kutengeneza vizimba katika Bwawa hilo, lengo likiwa ni kutafsiri namna maji yanavyoweza kuinufaisha jamii kwa namna nyingine zaidi ya kilimo cha Umwagiliaji.

Kwa upande wake Mratibu wa Matawi ya Agricom Africa hapa nchini Bw. Zuberi Lujina amesema kampuni hiyo iko tayari kufanya kazi na mkoa wa Simiyu katika kuhakikisha wakulima wanaondokana na kilimo cha mazoea kwenda kwenye kilimo chenye tija na kilimo biashara wakitumia zana bora za kilimo.

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, Mhandisi. Wilbert Siogopi amesema wameshazungumza na Viongozi wa Kampuni ya Agricom Africa ambapo wameahidi kufikisha vifaa na zana hizo katika Halamshauri ya Wilaya ya Bariadi katika juma la tarehe 20 hadi 27 mwezi huu.

MWISHO
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka akizungumza katika Kikao cha Tathmini  Maonesho ya Nanenane yaliyofanyika Kitaifa mwaka 2018 mkoani Simiyu na kuwashukuru  Viongozi  na watendaji wa Chama na Serikali, wafanyabiashara na wadau wengine walioshiriki katika kufanikisha  maonesho hayo,  kilichofanyika Mjini Bariadi.


Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu akizungumza katika Kikao cha Tathmini  Maonesho ya Nanenane yaliyofanyika Kitaifa mwaka 2018 mkoani Simiyu na kuwashukuru  Viongozi  na watendaji wa Chama na Serikali, wafanyabiashara na wadau wengine walioshiriki katika kufanikisha  maonesho hayo,  kilichofanyika Mjini Bariadi.


Mratibu wa Matawi ya Kampuni ya Agricom Africa inayohusika na uuzaji wa zana bora za kisasa za kilimo, Bw. Zuberi Lujina akiztoa maelezo ya namna kampuni yake inavyofanya kazi,  katika Kikao cha Tathmini  ya Maonesho ya Nanenane yaliyofanyika Kitaifa mwaka 2018 mkoani Simiyu na kuwashukuru  Viongozi  na watendaji wa Chama na Serikali, wafanyabiashara na wadau wengine walioshiriki katika kufanikisha  maonesho hayo,  kilichofanyika Mjini Bariadi.



Mkuu wa Mkoa wa Wilaya ya Maswa, Dkt. Seif Shekalaghe akizungumza katika Kikao cha Tathmini  Maonesho ya Nanenane yaliyofanyika Kitaifa mwaka2018 mkoani Simiyu na kuwashukuru  Viongozi  na watendaji wa Chama na Serikali, wafanyabiashara na wadau wengine walioshiriki katika kufanikisha  maonesho hayo,  kilichofanyika Mjini Bariadi.

Baadhi ya Viongozi  na Watendaji wa Chama na Serikali, Wafanyabiashara na wadau wengine wakiwa katika kikao cha tathmini ya  Maonesho ya Nanenane yaliyofanyika Kitaifa mwaka 2018 mkoani Simiyu,  kilichofanyika Mjini Bariadi.
Baadhi ya Viongozi  na Watendaji wa Chama na Serikali, Wafanyabiashara na wadau wengine wakiwa katika kikao cha tathmini ya  Maonesho ya Nanenane yaliyofanyika Kitaifa mwaka 2018 mkoani Simiyu,  kilichofanyika Mjini Bariadi.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!