Monday, August 20, 2018

WANANCHI SIMIYU WAHIMIZWA KUWEKEZA KWENYE UJENZI WA MIUNDOMBINU YA ELIMU

Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa mwaka 2018, Ndg. Charles Kabeho amewahimiza wananchi wa wilaya ya Maswa mkoani Simiyu kuwekeza katika miundombinu ya elimu ili kukabiliana na msongamano wa wanafunzi  unaotokana na utekelezaji wa Sera ya Elimu  bila malipo.

Kabeho ametoa wito huo katika kijiji cha Jija wakati akizindua mradi wa Maji  na vyumba  viwili vya madarasa katika Shule ya Sekondari Jija, wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru wilayani humo Agosti 19, 2018 .

Amesema kutokana na utekelezaji wa sera ya Elimu bila malipo kumekuwa na ongezeko kubwa la wanafunzi wanaoandikishwa darasa la awali, darasa la kwanza wanaojiunga na kidato cha kwanza, hivyo wananchi wawekeze katika ujenzi wa madarasa na  miundombinu mingine ya elimu ili wanafunzi waweze kusoma katika mazingira mazuri.

Katika hatua nyingine Kabeho amewataka Watumishi wa Umma kuacha kufanya kazi kwa mazoea badala yake wafanye kazi kwa kwa weledi na ufanisi mkubwa wakiizingatia sheria, kanuni na taratibu.

“Mhe. Rais anaposema HAPA KAZI TU anamaanisha fanya kazi kwa bidii,  zingatia sheria, taratibu na kanuni, wapo watumishi wanafanya kazi pale tu palipo na maslahi mahali ambapo hapana maslahi hamwajibiki, achaneni na kufanya kazi kwa mazoea fanyeni kazi kwa kujituma na kwa ufanisi” alisema

Mbunge wa Jimbo la Maswa Magharibi Mashimba Ndaki akizungumza kwa niaba wa wananchi ameishukuru Serikali kwa namna inavyoendelea kuwaletea wananchi maendeleo,  ambapo ameshukuru kwa kupelekea miradi hiyo ya maji na elimu katika Kijiji cha Jija ,huku akisisitiza wazazi kutowakatisha masomo watoto wao hususani wa kike
.
Mwenge wa Uhuru ukiwa Wilayani Maswa  umepitia miradi yenye thamani ya milioni 516, kutoka sekta ya Elimu, Afya, Maji, Maendeleo ya Jamii (Vikundi vya vijana na wanawake)

Mbio za mwenge mkoani SIMIYU zimehitimishwa Agosti 19  baada ya kuanza kukimbizwa Agosti 14 ukitokea mkoani Singida na unatarajiwa kukabidhiwa mkoani Shinyanga Agosti 2018.
MWISHO

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2018, Ndg. Charles Kabeho akifungua vyumba viwili vya madasa katika Shule ya Sekondari Jija wilayani Maswa, Agosti 19, 2018, wakati Mwenge wa Uhuru ukiwa katika mbio zake wilayani humo
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru  2018, Ndg. Charles Kabeho akishuhudia jiwe la Ufunguzi wa Madarasa mawili aliyofungua katika Shule ya Sekondari Jija wilayani Maswa, Agosti 19, 2018 likisomwa, wakati Mwenge wa Uhuru ukiwa katika mbio zake wilayani humo.
Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe. Dkt. Seif Shekalaghe akisalimiana na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru  2018, Ndg. Charles Kabeho mara baada ya kukabidhiwa rasmi na Mkuu wa Wilaya ya Busega, Mhe. Tano Mwera(hayupo pichani), Agosti 19, 2018. 
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2018, Ndg. Charles Kabeho akimtwisha ndoo mkazi wa Jija mara baada ya kuzindua mradi wa maji wa Jija wilayani Maswa Agosti 19, wakati Mwenge wa Uhuru ukiwa katika mbio zake wilayani humo.
Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe. Dkt. Seif Shekalaghe akipokea Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Mkimbiza Mwenge Kitaifa Dominik Rweyemamu Njunwa, mara baada ya makabidhiano kati ya Wilaya ya Busega na Maswa yaliyofanyika Kijiji cha Jija kukamilika, Agosti 19, 2018.
Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe. Dkt. Seif Shekalaghe(kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Busega, Mhe. Tano Mwera wakitakiana heri mara baada ya kukamilika kwa makabidhiano ya mwenge wa Uhuru baina yao, yaliyofanyika katik a Kijiji cha Jija Wilayani Maswa Agosti 19,2018.
Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe. Dkt. Seif Shekalaghe(kushoto) na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2018, Ndg. Charles Kabeho wakiteta jambo mara baada ya madarasa mawili katika Shule ya Sekondari Jija kufunguliwa na kiongozi huyo Agosti 19, 2018, wakati Mwenge wa Uhuru ukiwa katika mbio zake wilayani humo

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa, Dkt. Fredrick Sagamiko(kushoto)  akisalimiana na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru  2018, Ndg. Charles Kabeho mara baada ya kukabidhiwa rasmi na Mkuu wa Wilaya ya Busega, Mhe. Tano Mwera(hayupo pichani) kwa Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Dkt. Seif Shekalaghe, Agosti 19, 2018.
 Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru  2018, Ndg. Charles Kabeho na Viongozi wa Wilaya ya Maswa wakisikiliza taarifa ya ujenzi wa Nyumba ya Mtumishi katika Kituo cha Afya cha Malampaka, kabla ya Kiongoi huyo kukagua na kufungua jengo hilo Agosti 19, 2018,  wakati Mwenge wa Uhuru ukiwa katika mbio zake wilayani humo.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru  2018, Ndg. Charles Kabeho akifuatilia nyaraka mbalimbali zinazoonesha uthibitisho wa fedha za Halmashauri ya Wilaya ya Maswa zilizotolewa kama mkopo kwa vikundi vya Vijana na Wanawake, kabla ya kukagua kazi za Vikundi hivyo, wakati Mwenge wa Uhuru ukiwa katika mbio zake wilayani humo Agosti 19, 2018.


Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru  2018, Ndg. Charles Kabeho akizungumza na viongozi wa Wilaya ya Maswa, kabla ya kuzindua Mradi wa Maji wa Kijiji cha Jija wakati Mwenge wa Uhuru ukiwa katika mbio zake wilayani humo Agosti 19, 2018.



Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe. Dkt. Seif Shekalaghe(kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Busega, Mhe. Tano Mwera wakitakiana heri mara baada ya kukamilika kwa makabidhiano ya mwenge wa Uhuru baina yao, yaliyofanyika katik a Kijiji cha Jija Wilayani Maswa Agosti 19,2018.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru  2018, Ndg. Charles Kabeho akizungumza na viongozi wa Wilaya ya Maswa, wakati Mwenge wa Uhuru ulipopita katika Mradi wa Jengo la Bweni ukiwa katika mbio zake wilayani humo Agosti 19, 2018.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru  2018, Ndg. Charles Kabeho akisalimiana na Wajasiriamali kutoka katika Vikundi vya wakina mama na vijana, wakati alipopita na kuona kazi zao, wakati Mwenge wa Uhuru ukiwa katika mbio zake wilayani humo Agosti 19, 2018.
Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe. Dkt. Seif Shekalaghe(kulia), akikiri kupokea Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Busega, Mhe. Tano Mwera katika makabidhaiano yaliyofanyika katika Kijiji cha Jija wilayani Maswa, wakati Mwenge wa Uhuru ukiwa katika mbio zake wilayani humo Agosti 19, 2018.
Vijana wa Wilaya ya Maswa wakimvisha skafu Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru  2018, Ndg. Charles Kabeho mara baada ya kuwasili wilayani humo akitokea wilayani Busega, tayari kwa kuanza mbio za  Mwenge wa Uhuru wilayani humo Agosti 19, 2018.
Mkuu wa Wilaya ya Busega, Mhe. Tano Mwera akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe. Dkt. Seif Shekalaghe(kulia), Mwenge wa Uhuru tayari kwa kuanza kuukimbiza katika Wilaya ya Maswa, Agosti 19, 2018. 

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!