Friday, August 10, 2018

TAASISI YA FRIEDKIN CONSERVATION FUND YATOA SHILINGI MILIONI 110 KUSAIDIA UJENZI WA SHULE MAALUM SIMIYU

Taasisi ya Uhifadhi na Utalii ya Friedkin Conservation Fund, imetoa msaada ya shilingi   millioni 110 ili kusaidia ujenzi wa shule ya sekondari ya vipaji maalum katika Mkoa wa Simiyu.

Msaada huo ulikabidhiwa kwa Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka na  Wakurugenzi wa Taasisi hiyo wakiongozwa na Abdukadir Mohamed katika hafla iliyofanyika Uwanja wa Maonesho ya Nanenane Nyakabindi uliopo Halmashauri ya Mji wa  Bariadi.

Mohamed  amesema Taasisi yao ambayo inamiliki kampuni za Uwindaji na upigaji picha za  Kitalii,Mwiba holdings  Ltd na Tanzania Game Trackers Safaris, ambazo zimewekeza mkoani humo, zimetoa msaada huo kusaidia watoto kupata elimu, huku akibanisha kuwa huu ni mwendelezo wa misaada ya kusaidia jamii inayotolewa ili kuchangia maendeleo  ya mkoa wa Simiyu.

"Tunachoomba ni kupewa ushirikiano tufanye kazi zetu za utalii na uhifadhi ipasavyo  pasipo shida yoyote, tuko tayari kusaidia na kuchangia maendeleo katika Mkoa wa Simiyu” alisema

Mkuu wa  Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ameshukuru wawekezaji hao kwa msaada huo walioutoa ili kusaidia ujenzi wa shule maalum ya mkoa, ambapo amesema pamoja na kujenga shule hiyo mkoa huo una mpango wa kujenga shule nyingine tatu maalum.
Amesema awali mkoa ulipanga kuifanya Shule ya Sekondari Simiyu kuwa shule ya ufundi kwa kuiongezea miundombinu yote muhimu jambo ambalo lilishauriwa na Wizara ya Elimu litafutwe eneo kubwa zaidi kwa kuwa lile llionekana kuwa dogo.
Ameongeza kuwa Mkoa umezingatia ushauri wa Wizara na kutafuta eneo kubwa  lenye ukubwa  wa ekari 50 lililopo Sapiwi  wilayani Bariadi na kubainisha kuwa Wizara imeshatoa shilingi milioni 200 kwa ajili ya ujenzi wa shule hiyo na hivyo kuendelea kuifanya Simiyu Sekondari kubaki kuwa shule maalum ndani ya mkoa.
Aidha, Mtaka amebainisha kuwa wadau mbalimbali wamechangiai ujenzi wa shule hiyo maalum wakiwemo Shirika la Bima la Taifa limetoa mifuo 400 ya saruji,  Mamlaka ya Viwanja vya Ndege mifuko 400, mifuko 400 kutoka Shirika la Reli na mifuko 200 kutoka kwa Mtanzania mmoja aitwaye Reans na Mwiba Holdings Limited ambaye amekabidhi hundi ya shilingi milioni 110.
“Watu mbalimbali wanaendelea kuchangia ujenzi wa shule yetu saruji,  Shirika la Bima la Taifa limetoa mifuko 400, Mamlaka ya Viwanja vya Ndege mifuko 400, mifuko 400 kutoka Shirika la Reli na mifuko 200 kutoka kwa Mtanzania mmoja aitwaye Reans,  MWIBA Holdings Limited nao sasa hivi wanatukabidhi pia hundi ya shilingi milioni 110”
“Kulikuwa na changamoto kwa mwekezaji huyu lakini Kamati ya Ulinzi na Usalam ya Mkoa na kamati ya Siasa ya Mkoa zilienda zikakutana na Viongozi wa Friedkin/ Mwiba Holdings Ltd na ufumbuzi ukapatikana” alisisitiza.

Amesema wawekezaji hao wamekuwa na mchango mkubwa wa maendeleo  katika mkoa huo kwani hivi karibuni walitoa msaada wa mifuko 3000 ya saruji na bati 1000 kusaidia elimu.

Mchango mwingine ni kutoa ajira kwa wananchi na pia wamechangia kuongeza mapato ya Mkoa kwa kuwa jalada la Malipo la Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) limehamishiwa Mkoani Simiyu kutoka mkoani Arusha lililokuwa awali.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Meatu, Mhe. Dkt. Joseph Chilongani amesema Serikali inatambua mchango wa Taasisi hiyo katika  maendeleo  ya jamii.

Mbunge wa viti maalum (CCM) Mkoa wa Simiyu, Mhe. Esther Midimu amempongeza Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe Anthony Mtaka pamoja na wasaidizi wake kwa jitihada wanazofanya kutafuta michango ya wadau kufanikisha ujenzi wa shule hiyo na akaomba wasimamie vizuri michango hiyo ili ifanye kazi iliyokusudiwa.
Naye Mkuu wa Wilaya ya Itilima Mhe. Benson Kilangi amesema yeye pamoja na wasaidizi wa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka watafanya kila linalowezekana ili  malengo  yalikusudiwa kufanyika kwa ajili ya maendeleo ya wananchi yanafikiwa.
MWISHO


Mkurugenzi wa kampuni za Uwindaji na upigaji picha za  Kitalii,Mwiba holdings  Ltd na Tanzania Game Trackers Safaris Abdukadir Mohamed akikabidhi hundi ya shilingi milioni 110 kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa shule maalum Simiyu, wengine ni viongozi wa Mkoa wa Simiyu wakishuhudia makabidhiano hayo.
Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Dkt. Seif Shekalaghe akitoa shukrani mara baada ya makabidhiano ya hundi ya shilingi milioni 110 kati ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka na Mkurugenzi wa kampuni za Uwindaji na upigaji picha za  Kitalii,Mwiba holdings  Ltd na Tanzania Game Trackers Safaris Abdukadir Mohamed kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa Shule maalum Simiyu.

Mkuu wa Wilaya ya Itilima, Mhe. Benson Kilangi  akizungumza mara baada ya makabidhiano ya hundi ya shilingi milioni 110 kati ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka na Mkurugenzi wa kampuni za Uwindaji na upigaji picha za  Kitalii,Mwiba holdings  Ltd na Tanzania Game Trackers Safaris Abdukadir Mohamed kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa Shule maalum Simiyu.
Mkurugenzi wa kampuni za Uwindaji na upigaji picha za  Kitalii, Mwiba holdings  Ltd na Tanzania Game Trackers Safaris Abdukadir Mohamed akikabidhi hundi ya shilingi milioni 110 kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa shule maalum Simiyu, wengine ni viongozi wa Mkoa wa Simiyu wakishuhudia makabidhiano hayo.
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Simiyu(CCM) Esther Midimu  akizungumza mara baada ya makabidhiano ya hundi ya shilingi milioni 110 kati ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka na Mkurugenzi wa kampuni za Uwindaji na upigaji picha za  Kitalii,Mwiba holdings  Ltd na Tanzania Game Trackers Safaris Abdukadir Mohamed kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa Shule maalum Simiyu.
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Mhe. Gungu Silanga  akizungumza mara baada ya makabidhiano ya hundi ya shilingi milioni 110 kati ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka na Mkurugenzi wa kampuni za Uwindaji na upigaji picha za  Kitalii,Mwiba holdings  Ltd na Tanzania Game Trackers Safaris Abdukadir Mohamed kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa Shule maalum Simiyu.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!