Wednesday, August 29, 2018

RITA KUSAJILI NA KUTOA VYETI VYA KUZALIWA KWA ZAIDI YA WANAFUNZI 60,000 WILAYANI BARIADI


Wakala wa Usajili, Udhamini na Ufilisi (RITA) unatarajia kusajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa wanafunzi 60,000 wa shule za Msingi za Sekondari wilayani Bariadi mkoani Simiyu, kupitia Mpango wa Usajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wa miaka 06 hadi 18.

Hayo yamebainishwa na Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu RITA Bw. Charles Salyeem wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa Waratibu Elimu Kata na Maafisa Watendaji Kata  kuhusu Mpango wa Usajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa wanafunzi wa shule za msingi na Sekondari wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu, Agosti 28, 2018  mjini Bariadi.

Salyeem amesema mpango huo utahusisha usajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa wanafunzi wenye umri wa kuanzia miaka 06 hadi 18 kwa ushirikiano kati ya RITA na Ofisi za Wakurugenzi wa Halmashauri kupitia Idara za Elimu ambapo wanafunzi watasajiliwa na kupata vyeti vya kuzaliwa katika shule zao.

Ameongeza kuwa watoto wa umri wa miaka 06 hadi 18 ambao si wanafunzi watapata fursa ya kusajiliwa katika Ofisi za Watendaji wa Kata, huku akibainisha kuwa watapaswa kuwa na viambatisho vya msingi vinavyotakiwa kwa maelekezo watakayopewa na Watendaji wa Kata kwenye maeneo yao.

Aidha, Salyeem amesema wazazi na walezi wa watoto wenye umri huo watahitajika kuchangia gharama kwa ajili ya usajili na kupata vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wao  ili fedha zitakazopatikana  ziwezeshe kupeleka mpango huu katika maeneo mengine.

Awali akifungua mafunzo kwa Waratibu Elimu Kata kuhusu mpango huo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga amewatakaWaratibu Elimu Kata na Maafisa Watendaji Kata kuzingatia maelekezo watakayopewa na kufanya kazi kwa uadilifu wakitanguliza uzalendo na siyo maslahi binafsi.

Aidha,Kiswaga amesema cheti cha kuzaliwa ni moja ya nyaraka muhimu kwa wanafunzi wanaotoka hatua moja ya masomo kuingia nyingine hivyo akawataka viongozi na watendaji kujipanga ili kuvuka lengo la RITA la kusajili wanafunzi 60,000 kwa kuhakikisha kila fomu inayochukuliwa kwa ajili ya kuomba usajili inarudishwa na cheti cha kuzaliwa kinachukuliwa.

“RITA imejiwekea lengo la kusajili wanafunzi 60,000 kati ya zaidi ya 156,769 waliopo wilayani Bariadi, wanafunzi wasio na vyeti ni wengi, hivyo basi tujipange tuweze kuvuka lengo, tutumie viongozi kuhamasisha wazazi na kuhakikisha zoezi hili linafanikiwa” alisema.

Afisa Mtendaji wa Kata ya Ihusi, Kasimili Ngusa amesema mpango huu utawarahisishia wanafunzi wengi wa umri wa miaka 06 hadi 18 kwa kupata vyeti vya kuzaliwa shuleni walipo, tofauti na ilivyokuwa awali ambapo iliwalazimu wazazi na walezi kufuata huduma ya usajili na kupata vyeti vya kuzaliwa Ofisi za Mkuu wa Wilaya.

Naye Mratibu wa Elimu Kata ya Isanga, Sophia Kitobelo ametoa wito kwa wazazi na walezi kutumia fursa hiyo ya kusajili na kuchukua vyeti vya kuzaliwa shuleni na katika Ofisi za kata, kuhakikisha kuwa watoto wao wanapata vyeti vya kuzaliwa ambavyo ni miongoni mwa nyaraka muhimu kwa Watanzania.

Mkakati huu wa Usajili wa Wanafunzi wa shule za msingi na sekondari wenye umri wa miaka 06 hadi 18 umefunguliwa rasmi katika Wilaya ya Bariadi na baadaye utaendelea katika wilaya nyingine za Mkoa wa Simiyu; hadi sasa umeanza kutekelezwa katika wilaya kumi na moja za Mikoa miwili ya Dar es Salaam, Mara na Njombe.
MWISHO

Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu RITA Bw. Charles Salyeem akitoa taarifa katika Ufunguzi wa Mafunzo ya Waratibu Elimu Kata na Maafisa Watendaji Kata  kuhusu Mpango wa Usajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa wanafunzi wa Shule za Msingi na Sekondari wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu, Agosti 28, 2018  mjini Bariadi.

Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga  akifungua mafunzo kwa Waratibu Elimu Kata na Maafisa Watendaji Kata  kuhusu Mpango wa Usajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa wanafunzi wa shule za msingi na Sekondari wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu, Agosti 28, 2018  mjini Bariadi.
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga (kulia) na Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Bw. Donatus Weginah wakiteta jambo wakati ufunguzi wa mafunzo kwa Waratibu Elimu Kata na Maafisa Watendaji Kata  kuhusu Mpango wa Usajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa wanafunzi wa shule za msingi na Sekondari wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu, Agosti 28, 2018  mjini Bariadi.
Baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Simiyu wakiwa katika ufunguzi wa mafunzo kwa Waratibu Elimu Kata na Maafisa Watendaji Kata  kuhusu Mpango wa Usajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa wanafunzi wa shule za msingi na Sekondari wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu, Agosti 28, 2018  mjini Bariadi.
Baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Simiyu wakiwa katika ufunguzi wa mafunzo kwa Waratibu Elimu Kata na Maafisa Watendaji Kata  kuhusu Mpango wa Usajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa wanafunzi wa shule za msingi na Sekondari wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu, Agosti 28, 2018  mjini Bariadi.
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, baada ya ufunguzi wa mafunzo kwa Waratibu Elimu Kata na Maafisa Watendaji Kata  kuhusu Mpango wa Usajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa wanafunzi wa shule za msingi na Sekondari wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu, Agosti 28, 2018  mjini Bariadi.


Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa Elimu Kata wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, baada ya ufunguzi wa mafunzo kwa Waratibu Elimu Kata na Maafisa Watendaji Kata  kuhusu Mpango wa Usajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa wanafunzi wa shule za msingi na Sekondari wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu, Agosti 28, 2018  mjini Bariadi.

Baadhi ya viongozi waWilaya ya Bariadi wakiwa katika ufunguzi wa mafunzo kwa Waratibu Elimu Kata na Maafisa Watendaji Kata  kuhusu Mpango wa Usajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa wanafunzi wa shule za msingi na Sekondari wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu, Agosti 28, 2018  mjini Bariadi.
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa Watendaji Kata wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, baada ya ufunguzi wa mafunzo kwa Waratibu Elimu Kata na Maafisa Watendaji Kata  kuhusu Mpango wa Usajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa wanafunzi wa shule za msingi na Sekondari wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu, Agosti 28, 2018  mjini Bariadi.
Meneja Usajili RITA , Bi. Patricia Mpuya akiwasilisha mada katika  mafunzo kwa Waratibu Elimu Kata na Maafisa Watendaji Kata  kuhusu Mpango wa Usajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa wanafunzi wa shule za msingi na Sekondari wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu, Agosti 28, 2018  mjini Bariadi.
Baadhi ya viongozi waWilaya ya Bariadi wakiwa katika ufunguzi wa mafunzo kwa Waratibu Elimu Kata na Maafisa Watendaji Kata  kuhusu Mpango wa Usajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa wanafunzi wa shule za msingi na Sekondari wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu, Agosti 28, 2018  mjini Bariadi.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!