Saturday, August 18, 2018

VIONGOZI WATAKIWA KUWAKUMBUSHA WAZAZI KUCHANGIA CHAKULA SHULENI NA KUNUNUA SARE ZA WATOTO WAO



Viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega Mkoani Simiyu wametakiwa kuwakumbusha wazazi na walezi kuwanunulia watoto wao sare za shule na kuchangia chakula mashuleni ili watoto wao waweze kusoma kwa utuivu na umakini wanapokuwa shuleni  na  kuzuia utoro .

Rai hiyo imetolewa na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2018, Ndg. Charles Kabeho wakati wa makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru baina ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga na Mkuu wa Wilaya ya Busega, Mhe. Tano Mwera yaliyofanyika katika Kijiji cha Mkula wilayani humo.

Kabeho amesema Serikali ya awamu ya tano imefuta ada na michango mbalimbali iliyokuwa kero kwa wananchi ili kila mtoto wa Kitanzania apate haki ya Elimu kuanzia darasa la awali mpaka Kidato cha nne bila malipo , hivyo wazazi na walezi wanapaswa kuwanunulia watoto wao sare za shule pamoja na mahitaji yao mengine ya shule ikiwa ni pamoja na daftari na kalamu.

“ Kwa sasa wazazi hamlipi tena ada wala michango  wajibu wenu ni kununua sare za shule na kununua mahitaji mengine kama kalamu, daftari na mabegi ,Serikali inaendelea kuhamasisha mtimize wajibu wenu, lakini pia namuomba Mkurugenzi awaeleze Walimu wakuu sare za Halmashauri yake ni zipi ili nao wawakumbushe wazazi kwanunulia watoto wao sare hizo” alisema.

Aidha, Kabeho amesema ni vema  wazazi  na walezi wakachangia chakula shuleni ili kuwafanya wanafunzi waweze kusoma kwa utuivu na umakini wanapokuwa shuleni  na  kuzuia utoro .

“Tunaomba pia mtimize wajibu wenu kuchangia chakula shuleni kwa sababu unapotoa chakula shuleni tunapunguza utoro , tunaongeza umakini na ufuatiliaji kwa wanafunzi pale wanapofundishwa, wanafunzi wengi wao wanatoroka pale wanapohisi njaa na wakiondoka baadhi yao hawarudi” alisema Kabeho.

Katika hatua nyingine Mwenge wa Uhuru ukiwa Wilayani Busega na kupitia miradi saba yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 900 katika sekta mbalimbali ikiwemo Afya, Elimu na Viwanda.

Akizungumza mara baada ya kufungua vyumba vitatu vya madarasa na matundu matano ya vyoo katika Shule ya Sekondari Nasa, Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2018, Ndg. Charles Kabeho ameipongeza Serikali kwa kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya elimu ambayo itasaidia kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia.

Akizungumza na Wananchi baada ya kufungua Wodi ya wazazi katika Kituo cha Afya cha Nasa Kabeho amewashukuru wananchi kwa namna wanavyojitolea nguvu kazi katika ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo katika Kituo hicho cha Afya cha Nasa.

Akiwasilisha taarifa ya ujenzi wa Wodi hiyo ya wazazi, Katibu wa Afya Wilaya wa Wilaya ya Busega Huruma Temu amesema kuwa wodi hiyo katika kituo cha Afya Nassa hadi kukamilika kwake imegharimu kiasi cha shilingi Milioni 109 ikiwa ni fedha za wafadhili kutoka UNFPA.

Haruna alibainisha kuwa lengo kuu la kujenga wodi hiyo ya wazazi ni kuboresha afya ya uzazi na kupunguza idadi ya vifo vya akinamama na watoto Wilayani Busega.

MWISHO

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2018, Ndg. Charles Francis Kabeho akitoa Ujumbe wa Mwenge wa Uhuru mwaka 2018 katika Kijiji cha  Mkula wilayani Busega, wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru wilayani humo, Agosti 18, 2018.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2018, Ndg. Charles Francis Kabeho akikagua Ujenzi  wa Vyumba vitatu vya madarasa katika Shule ya Sekondari Nasa  wilayani Busega kabla ya kuvifungua, wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru  wilayani humo, Agosti 18, 2018.
 Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2018, Ndg. Charles Francis Kabeho akiweka jiwe la ufunguzi  wa  Vyumba vitatu vya madarasa katika Shule ya Sekondari Nasa  wilayani Busega , wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru  wilayani humo, Agosti 18, 2018.
Mkuu wa Wilaya ya Busega, Mhe. Tano Mwera(kulia) na Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga wakikabidhiana Mwengewa Uhuru tayari kwa ajili kuanza mbio zake wilayani Busega Agosti, 2018. 
Mkurugenzi wa Nassa Alovera Proccesors , Bw. Venance Mdunga (wa pili kulia) akitoa maelezo kwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2018, Ndg. Charles Francis Kabeho(wa pili kulia), wakati alipofika kukagua shamba lake ambalo linatoa malighafi ya kutengeneza bidhaa zitokanazo na Alovera.
Mkuu wa Wilaya ya Busega, Mhe. Tano Mwera(kushoto) akisalimiana na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2018, Ndg. Charles Francis Kabeho, mara baada ya Mwenge wa Uhuru, kufika wilayani Busega, Agosti 17, 2018. 
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2018, Ndg. Charles Francis Kabeho akiweka Jiwe la Msingi katika Kiwanda cha Kukoboa  Mpunga na kupanga madaraja  kilichopo Lamadi Bariadi, Agosti 17, 2018.
Askari wa FFU na Mkimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa Riziki Hassan Ali wakiondoka na Mwenge wa Uhuru katika Viwanja vya Shule Sekondari Nassa wilayani Busega, wakati ukiwa  katika mbio zake wilayani humo, Agosti 17, 2018
Mkuu wa Wilaya ya Busega, Mhe. Tano Mwera akipokea Mwenge wa Uhuru kutoka Kwa Mkimbiza  Mwenge Kitaifa Riziki Hassan Ali kutoka Mkoa wa Kusini Unguja, kwa ajili ya kuanza ratiba ya Mbio za Mwenge wa Uhuru wilayani humo, Agosti 18, 2018.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2018, Ndg. Charles Francis Kabeho akikagua  Wodi ya Mama na Mtoto iliyopo katika Kituo cha Afya cha Nasa wilayani Busega, wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru wilayani humo, Agosti 18, 2018.
 Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2018, Ndg. Charles Francis Kabeho akizungumza na viongozi na Wananchi mara baada ya kufungua Kituo cha Mafuta cah Masanza Kona, wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru wilayani humo, Agosti 18, 2018. 


Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2018, Ndg. Charles Francis Kabeyo(katikati) akiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Busega, Mhe. Tano Mwera na Mkurugenzi  wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega, Bw. Anderson Njiginya, wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru wilayani humo, Agosti 18, 2018.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2018, Ndg. Charles Francis Kabeho akisalimiana na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega, Mhe. Mickness Mahela, wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru wilayani humo, Agosti 18, 2018.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2018, Ndg. Charles Francis Kabeho akisalimiana na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega, Bw. Anderson Njiginya wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru wilayani humo, Agosti 18, 2018.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2018, Ndg. Charles Francis Kabeho akipewa maelezo na Mfanyakazi wa Kiwanda cha Nassa Alovera Proccesors juu ya namna wanavyotengeneza bidhaa mbalimbali na dawa zinazozalishwa   zinazozalishwa.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2018, Ndg. Charles Francis Kabeho akiangalia mchele ulikobolewa ukiwa katika hatua za mwisho kupangwa na kuwekwa  wenye madaraja, kabla ya kukiwekea kiwanda hicho jiwe la msingi, wakati Mwenge ukiwa katika Mbizo zake wilayani humo Agosti 17, 2018.  .

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!