Wednesday, August 1, 2018

DKT. MWANJELWA ATOA WITO KWA WAKULIMA KUTUMIA ZANA BORA ZA KILIMO, KULIMA KILIMO CHENYE TIJA


Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. Dkt.Mary  Mwanjelwa ametoa wito kwa wakulima kote nchini kulima kilimo chenye tija kwa kutumia zana bora za kilimo ili kuongeza uzalishaji na kupata mavuno mengi na bora.

Dkt. Mwanjelwa ameyasema hayo Agosti Mosi, mara baada ya kukagua mabanda ya maonesho ya Kilimo katika Uwanja wa Nanenane wa Kanda ya Ziwa Mashariki uliopo Nyakabindi Bariadi, katika Maonesho ya Nanenane Kitaifa yanayofanyika Kitaifa Mkoani Simiyu.

Dkt. Mwanjelwa amesema Serikali kupitia Mfuko wa pembejeo unatoa mkopo wa pembejeo kwa riba ndogo sana, hivyo akatoa wito kwa wakulima wote nchini kwenda katika Halmashuri zao na kupata utaratibu wa kuomba mikopo hiyo ili waweze kupata mikopo itakayowawezesha kununua zana bora za kilimo.

“ Nitoe wito kwa wakulima wote nchini wajitahidi sana kwenda kwenye  kulima kilimo cha kisasa kilimo chenye tija, sisi kama Serikali tuna mfuko wetu wa pembejeo unaotoa mikopo kwa riba ndogo sana, hivyo wakulima wanaweza kuomba mikopo hiyo na kwenda kununua pembejeo bora za Kilimo” alisema Dkt. Mwanjelwa.

Katika hatua nyingine Dkt. Mwanjelwa amewataka maafisa ugani kuwafuata wakulima shambani badala ya kukaa ofisini, ili kuwapa elimu ya kilimo bora na kuwawezesha wakulima  kufikia lengo la kulima kilimo chenye tija.

Naye Baraka Itemu mkulima wa Mpunga kutoka Geita  ametoa wito kwa wakulima wenzake kote nchini kuachana na matumizi ya jembe la mkono na jembe la kukokotwa na ng’ombe kwa kuwa ni teknolojia iliyopitwa na wakati na haina tija katika uzalishaji.

“ Mimi ni mkulima wa mpunga binafsi matrekta yamenisaidia sana maana  naweza kulima eneo kubwa kwa muda mfupi na nikapata mazao mengi, natoa wito kwa wenzangu wanaotumia majembe ya mkono na ya kukokotwa na ng’ombe waache waende kwenye makampuni ya matrekta wakakope,  ili waweze kuzalisha mazao kwa wingi” alisema Baraka.

Nao wauzaji wa zana bora za kilimo waliofika katika maonesho ya Nanenane Bariadi mkoani Simiyu wamesema wako tayari kushirikiana na wakulima ili kuhakikisha wanapata zana hizo, huku wakibainisha kuwa wakulima wasiokuwa na uwezo wa kununua zana hizo kwa fedha taslimu wako tayari kuwakopesha.

Maonesho ya Nananane mwaka 2018 yanafanyika Kitaifa Mkoani Simiyu, ambapo yameanza leo na yatahitimishwa Agosti 08, 2018.

MWISHO



Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Mary Mwanjelwa  akikagua mashamba darasa ya JKT katika Uwanja wa Nanenane Nyakabindi Halmashauri ya  mji wa Bariadi leo Agosti Mosi, 2018, katika maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2018, Mkoani Simiyu.



Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Mary Mwanjelwa  akikagua mashamba darasa ya JKT katika Uwanja wa Nanenane Nyakabindi Halmashauri ya  mji wa Bariadi leo Agosti Mosi, 2018, katika maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2018, Mkoani Simiyu.
  
Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe.Dkt. Mary Mwanjelwa akisalimiana  na Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini mara baada kuwasili katika Uwanja wa Nanenane wa Nyakabindi Bariadi, kwa ajili ya kujionea shughuli mbalimbali za maonesho ya Nanenane yanayofanyika Kitaifa mwaka 2018 mkoani Simiyu.



Bw. Baraka Itemu mkulima wa Mpunga kutoka Geita akizungumza na waandishi wa habari  (hawapo picha pichani) katika Uwanja wa nanenane Nyakabindi Bariadi, yanayofanyika kitaifa mwaka 2018 mkoani Simiyu.

  
Mtaalam wa kutoka Jeshi la Magereza akitoa maelezo kwa Manaibu Waziri wa Kilimo, Dkt. Mary Mwanjelwa wakati walipotembelea mabanda ya maonesho ya mifugo ya Jeshi hilo katika Uwanja wa Nanenane Nyakabindi Halmashauri ya Mji Bariadi,  katika maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2018, Mkoani Simiyu. 



Mtaalam wa Ufugaji wa Samaki kutoka JKT, Luteni Joseph  Lyakurwa(kulia) akitoa maelezo kwa   Manaibu Waziri wa Kilimo, Dkt. Mary Mwanjelwa (wa tatu kushoto)  na Mhe. Omary Mgumba (kushoto) wakati walipotembelea mashamba darasa ya JKT katika Uwanja wa Nanenane Nyakabindi Halmashauri ya Mji Bariadi,  katika maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2018, Mkoani Simiyu.


Mtaalamu wa Jeshi la Magereza akitoa maelezo ya namna ya kutengeneza mkaa kwa kutumia mabaki ya mimea kwa   Manaibu Waziri wa Kilimo, Dkt. Mary Mwanjelwa (wa tatu kulia)  na Mhe. Omary Mgumba (wa pili kulia) wakati walipotembelea mabanda ya maonesho ya Jeshi hilo katika  Uwanja wa Nanenane Nyakabindi Halmashauri ya Mji Bariadi,  katika maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2018, Mkoani Simiyu.


Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Mary Mwanjelwa akipewa maelezo kuhusu zana na mashine za kisasa  na wataalam wa JKT katika Uwanja wa Nanenane Nyakabindi Halmashauri ya Mji wa Bariadi leo Agosti Mosi, 2018, katika maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2018, Mkoani Simiyu.
Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini akiwatambulisha viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Simiyu  kwa Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa mara baada kuwasili katika Uwanja wa Nanenane wa Nyakabindi Bariadi, kwa ajili ya kujionea shughuli mbalimbali za maonesho ya Nanenane yanayofanyika Kitaifa mwaka 2018 mkoani Simiyu.





0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!