Sunday, September 9, 2018

JPM AMUAGIZA WAZIRI WA UJENZI KUTAFUTA MKANDARASI UJENZI WA BARABARA YA LAMI MEATU SIMIYU

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amemuagiza Waziri wa Ujenzi, Mawasilianona Uchukuzi kutafuta Mkandarasi wa Ujenzi wa barabara za lami (kilomita tatu ) katika Mji wa Mwanhuzi wilayani Meatu Mkoani Simiyu.


Mhe. Rais Magufuli ameyasema hayo Septemba 09, 2018 wakati akiwahutubia wananchi katika Mkutano wa Hadhara uliofanyika katika Viwanja vya Stendi ya Mwanhuzi wilayani Itilima mkoani Simiyu, wakati akiwa katika ziara yake  mkoani humo.

Amesema wakati akiwa Waziri wa ujenzi aliahidi ujenzi wa barabara hiyo Waziri wa ujenzi Mawasiliano na uchukuzi ahakikishe anamtafuta Mkandarasi ili aanze kufanya kazi hiyo mwezi huu Septemba 2018, ili ahadi hiyo aliyoitoa kwa wananchi wa Meatu itimie.

“Wakati nilipokuja hapa nikiwa Waziri wa Ujenzi niliahidi ujenzi wa kilomita tatu za lami, nimeshaangaa sana kuona hizo kilomita hazijajengwa, nakuagiaza Waziri wa Ujenzi kabla mwezi huu haujaisha nimuone mkandarasi anaanza kufanya kazi hapa” alisema

Aidha, Mhe. Rais amewataka wananchi kushirikiana na viongozi wao katika kujiletea maendeleo huku akiwasisitiza kuacha kujichukulia sheria mkononi na badala yake wazingatie sheria za nchi.

Katika hatua nyingine Mhe. Rais Magufuli amewaagiza Wakuu wa Mikoa na Wilaya kote nchini kushirikiana na Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuweka mipango itakayowezesha wakulima na wafugaji wanafanya shughuli zao kwa amani.

Awali akitoa salamu za Mkoa Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema mkoa huo una mpango wa kutambua na kuyapima maeneo ya Wafugaji na kuyawekea miundombinu ili wafugaji waachane na ufugaji waachane na kuhama hama na wafuge kwa tija.

Kwa upande wake Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi amesema Serikali inajiandaakufanya usanifu wa awali wa Ujenzi wa barabara ya Bariadi-Itilima-Kisesa-Mwandoya-Ng’oboko-Sibiti  ili kwa baadaye ijengwe katika kiwango cha lami.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli anaendelea na ziara yake ya siku tatu mkoani Simiyu, ambapo Septemba 10 amesalimia wananchi katika maeneo mbalimbali ikiwemo Lagangabilili Itilima, Kisesa, Mwandoya, mkutano wa hadhara Mwanhuzi na kufungua majengo ya uboreshaji wa huduma za afya katika Hospitali ya Wilaya ya Meatu, kwa niaba ya vituo vingine 39.

MWISHO




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwahutubia wananchi katika Mkutano wa Hadhara uliofanyika katika Viwanja vya Stendi ya Mwanhuzi wilayani Meatu mkoani Simiyu, Septemba 09, 2018  wakati akiwa katika ziara yake  mkoani humo.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akitoka kukagua majengo ya majengo ya uboreshaji wa huduma za afya katika Hospitali ya Wilaya ya Meatu, kabla ya kufuungua kwa niaba ya vituo vingine 39, Septemba 09, 2018  wakati akiwa katika ziara yake  mkoani humo.

Wananchi wa Tarafa ya Mwandoya wilaya ya Meatu Mkoani Simiyu wakimsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli alipowasilimia, Septemba 09, 2018  wakati akiwa katika ziara yake  mkoani humo.


Baadhi ya viongozi wa Chama na Serikali wakimsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, katika Mkutano wa Hadhara uliofanyika katika Viwanja vya Stendi ya Mwanhuzi wilayani Meatu mkoani Simiyu, Septemba 09, 2018  wakati akiwa katika ziara yake  mkoani humo.



Baadhi ya viongozi wa Chama na Serikali wakimsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, katika Mkutano wa Hadhara uliofanyika katika Viwanja vya Stendi ya Mwanhuzi wilayani Meatu mkoani Simiyu, Septemba 09, 2018  wakati akiwa katika ziara yake  mkoani humo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na viongozi wa wilaya ya Meatu na Baadhi ya watumishi wa sekta ya afya mara baada ya kufungua majengo ya uboreshaji wa huduma za afya katika Hospitali ya Wilaya ya Meatu, kwa niaba ya vituo vingine 39, Septemba 09, 2018  wakati akiwa katika ziara yake  mkoani humo.
Wananchi wa Tarafa ya Mwandoya wilaya ya Meatu Mkoani Simiyu wakimsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli alipowasilimia, Septemba 09, 2018  wakati akiwa katika ziara yake  mkoani humo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo akizungumza na viongozi wa wilaya ya Meatu na Baadhi ya watumishi wa sekta ya afya, mara baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, kufungua majengo ya uboreshaji wa huduma za afya katika Hospitali ya Wilaya ya Meatu, kwa niaba ya vituo vingine 39, Septemba 09, 2018  wakati akiwa katika ziara yake  mkoani humo.
Baadhi ya viongozi wa wilaya ya Meatu na watumishi wa sekta ya afya, wakimsikiliza  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, mara baada ya kufungua yamajengo ya  uboreshaji wa huduma za afya katika Hospitali ya Wilaya ya Meatu, kwa niaba ya vituo vingine 39, Septemba 09, 2018  wakati akiwa katika ziara yake  mkoani humo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo akiteta jambo na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe. Enock Yakobo mara baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, kufungua majengo ya uboreshaji wa huduma za afya katika Hospitali ya Wilaya ya Meatu, kwa niaba ya vituo vingine 39, Septemba 09, 2018  wakati akiwa katika ziara yake  mkoani humo.




Naibu Waziri wa Madini,   Mhe. Stanslaus Nyongo akizungumza na wananchi katika Mkutano wa Hadhara uliofanyika katika Viwanja vya Stendi ya Mwanhuzi wilayani Meatu mkoani Simiyu, Septemba 09, 2018  wakati akiwa katika ziara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli mkoani humo.
Wananchi wa Mji wa Mwanhuzi wilaya ya Meatu Mkoani Simiyu wakimsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli katika Mkutano wa hadhara , Septemba 09, 2018  wakati akiwa katika ziara yake  mkoani humo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli(kulia) akifuatilia jambo katika mkutano wake na viongozi wa wilaya ya Meatu na Baadhi ya watumishi wa sekta ya afya, mara baada ya kufungua majengo ya uboreshaji wa huduma za afya katika Hospitali ya Wilaya ya Meatu, kwa niaba ya vituo vingine 39, Septemba 09, 2018  wakati akiwa katika ziara yake  mkoani Simiyu, (kushoto ) Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Anthony Mtaka ( katikati) Mkurugenzi Mkazi wa UNFPA hapa nchini Bi. Jacqueline Mahon.



Wananchi wa Mji wa Mwanhuzi wilaya ya Meatu Mkoani Simiyu wakimsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli katika Mkutano wa hadhara , Septemba 09, 2018  wakati akiwa katika ziara yake  mkoani humo.

Wananchi wa Mji wa Mwanhuzi wilaya ya Meatu Mkoani Simiyu wakimsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli katika Mkutano wa hadhara , Septemba 09, 2018  wakati akiwa katika ziara yake  mkoani humo.


0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!