Wednesday, September 19, 2018

SERIKALI YATENGA SHILINGI BILIONI 4.5 UJENZI WA HOSPITALI TATU ZA WILAYA SIMIYU

Serikali imetenga kiasi cha shilingi bilioni  4.5 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali tatu za Halmashauri za Wilaya ya Busega ,Bariadi na Itilima Mkoani  Simiyu  katika bajeti 2018/2019,  ili kuendelea kuboresha utoaji wa huduma za afya kwa wananchi.

Hayo yamesemwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa SIMIYU  Bw. JUMANNE SAGINI katika kikao cha wadau wa Afya kilichofanyika Mjini Bariadi, lengo likiwa kujadili mipango na shughuli mbalimbali zinazofanywa na wadau hao mkoani Simiyu.

Sagini amewaomba Wakuu wa wilaya Bariadi, Busega  na Itilima kuwa fedha hizo zitakapoletwa wazisimamie kwa ukaribu na kuhakikisha ujenzi wa hospitali hizo unakamilika kwa wakati ili wananchi wapate huduma.

Aidha, Sagini ametoa wito kwa wadau wa afya mkoani humo kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuboresha huduma za afya  kwa kuwekeza zaidi katika vipaumbele vya Mkoa huo hususani ujenzi wa Miundombinu ya afya ikiwemo Vituo vya Afya na zahanati ambavyo mahitaji yake ni makubwa kwa wananchi.

“Tuna vituo vya Afya 17 kati ya130 vinavyotakiwa na kuna juhudi zinafanywa na wadau vituo vya Afya vingine sita vinajengwa, zahanati ziko 192 mahitaji ni zahanati 279 na zinazoendelea kujengwa 107; kuna uhitaji wa vituo vya kutolea huduma na ndiyo maana tunalipigia kelele kweli suala hili” alisema Sagini.

Mratibu wa Ukimwi Mkoa wa Simiyu, Dkt. Khamis Kulemba akitoa taarifa ya maazimio ya kikao kilichopita, ameainisha mafanikio ya wadau wa afya mkoani humo kuwa wamesaidia katika ujenzi na ukarabati wa vituo vya afya, kutoa magari ya kubebea wagonjwa (ambulance) katika baadhi ya vituo vya kutolea huduma, kupunguza vifo vya mama na mtoto na kuwepo kwa ongezeko la matumizi ya huduma za uzazi wa mpango.

Naye Hererico Ernest Afisa Mradi Amref Mkoa wa Simiyu, amesema Shirika hilo linatarajia kukarabati vituo vya kutolea huduma za afya 24 kupitia Mradi wa Uzazi Uzima, ili viweze kutoa huduma stahiki kwa mama na mtoto

“ Katika wilaya ya Meatu tutakarabati vituo vitatu, Maswa vituo vitano, Itilima vituo vinne, Bariadi mjini vituo vitatu,  Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi vituo viko vinne, Busega vituo vitano, tutavikarabati lengo ni kuhakikisha vinatoa huduma bora kwa wananchi, tutahakikisha huduma ya maji inapatikana na katika baadhi ya vituo tutajenga majengo wodi za wazazi” alisema

Kwa upange wake Mratibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa  linaloshughulikia idadi ya watu duniani  (UNFPA) Mkoa Wa Simiyu, Dkt Amir Batenga amesema mfumo wa Serikali kutumia ‘Force Account’ katika ujenzi wa vituo 38 vilivyojengwa na kukarabatiwa na shirika hilo umesaidia majengo hayo kujengwa kwa gharama nafuu na ubora unaotakiwa chini ya usimamizi wa Watalaam wa Halmashauri.

Kikao cha Wadau wa Afya Mkoa wa Simiyu kiliwahusisha Viongozi na Watendaji wa Serikali ngazi ya Mkoa na Wilaya, Viongozi wa madhehebu ya Dini na Wadau hao wakiwemo AMREF, AGPAHI, CUAMM, UNFPA, Mkapa Foundation, AMERICARE, PSI, Red Cross, ICAP, INTRAHELTH, BORESHA AFYA na  MARIESTOPES 


Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini akizungumza na viongozi,, watendaji na wadau wa afya wa Mkoa huo katika kikao kilichofanyika Septemba 17, 2018 Mjini Bariadi, kwa lengo la kujadili mipango na shughuli za wadau hao mkoani humo 
Baadhi ya Viongozi, watendaji na wadau wa afya wa mkoa wa Simiyu wakimsikiliza Katibu Tawala wa Mkoa, Bw. Jumanne Sagini katika kikao kilichofanyika Septemba 17, 2018 Mjini Bariadi, kwa lengo la kujadili mipango na shughuli za wadau hao mkoani humo.
Baadhi ya Viongozi, watendaji na wadau wa afya wa mkoa wa Simiyu wakimsikiliza Katibu Tawala wa Mkoa, Bw. Jumanne Sagini katika kikao kilichofanyika Septemba 17, 2018 Mjini Bariadi, kwa lengo la kujadili mipango na shughuli za wadau hao mkoani humo.



Mratibu wa Mapambano dhidi ya UKIMWI mkoa wa Simiyu , Dkt. Khamis Kulemba akitoa taarifa katika kikao cha wadau wa afya wa Mkoa huo katika kikao kilichofanyika Septemba 17, 2018 Mjini Bariadi, kwa lengo la kujadili mipango na shughuli za wadau hao mkoani humo.
Mkuu wa Wilaya ya Itilima, Mhe. Benson Kilangi, akichangia hoja katika kikao cha viongozi, watendaji na wadau wa afya wa Mkoa huo, kilichofanyika Septemba 17, 2018 Mjini Bariadi, kwa lengo la kujadili mipango na shughuli za wadau hao mkoani humo.
Mratibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa  Linaloshughulikia idadi ya watu duniani  (UNFPA) Mkoa Wa Simiyu, Dkt Amir Batenga akiwasilisha mada katika kikao cha wadau wa afya wa Mkoa huo kilichofanyika Septemba 17, 2018 Mjini Bariadi, kwa lengo la kujadili mipango na shughuli za wadau hao mkoani humo.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Kikristo(CCT) Mkoa wa Simiyu,  Mch. Martine Nketo(kushoto) akiteta jambo na Sheikh wa Mkoa wa Simiyu, Mahamoud Kalokola katika kikao cha wadau wa afya wa mkoa huo kilichofanyika Septemba 17, 2018 Mjini Bariadi.
Mwakilishi wa Shirika lisilo la Kiserikali la ICAP akiwasilisha mada katika kikao cha wadau wa afya wa mkoa wa Simiyu kilichofanyika Septemba 17, 2018 Mjini Bariadi.
Mmoja wa wadau wa Afya Mkoani Simiyu akichangia hoja katika kikao cha viongozi, watendaji na wadau wa afya wa Mkoa huo, kilichofanyika Septemba 17, 2018 Mjini Bariadi, kwa lengo la kujadili mipango na shughuli za wadau hao mkoani humo.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini (kulia) akiongoza kikao cha viongozi, watendaji na wadau wa afya wa Mkoa huo, kilichofanyika Septemba 17, 2018 Mjini Bariadi, kwa lengo la kujadili mipango na shughuli za wadau hao mkoani humo.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!