Tuesday, September 4, 2018

WANANCHI MWASUBUYA SIMIYU KUBADILI MAISHA YAO KIUCHUMI KUPITIA KILIMO CHA UMWAGILIAJI


Wananchi wa Kijiji cha Mwasubuya wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu wamesema Mradi wa Umwagiliaji wa Mwasubuya wenye ekari 514 utawasaidia kubadili maisha yao kiuchumi kwa kuwa wanatarajia kuongeza mavuno kutokana na kuanza kutumia zana za kilimo za kisasa katika uzalishaji kuanzia hatua ya kuandaa mashamba hadi kuvuna.

Wananchi hao wameyasema hayo baada ya makabidhiano ya zana za kilimo za kisasa zitakazotumika kuanzia hatua ya kuandaa mashamba mpaka kuvuna, kutoka Kampuni ya Agricom kwa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi ambayo imewadhamini wananchi walio katika mradi wa Umwagiliaji wa Mwasubuya, yaliyofanyika katika eneo la Mradi Kijiji cha Mwasubuya, Septemba 03, 2018.

Wamesema pamoja na kuongeza uzalishaji kutokana na uwepo wa maji ya uhakika ya Bwawa la Mwasubuya na matumizi ya zana bora, mradi huo ambao utajikita zaidi katika kilimo cha mpunga pia utawawezesha wananchi  na hasa vijana kujiajiri kupitia kilimo cha mboga mboga, hatimaye kukuza kipato chao na Taifa kwa ujumla.

“Tumefurahi sana kupata mradi wa umwagiliaji, hii ni ajira kwetu hasa sisi vijana wenye nguvu, nina imani tukiutumia mradi huu vizuri utatubadilisha sisi kiuchumi kwa sababu mashine za kisasa tulizoletewa tutazitumia kulima eneo kubwa kwa muda mfupi, tutatongeza mavuno na kupata hela nyingi ” alisema Daniel Ntobi Mkulima wa Mwasubuya

“Nimeupokea mradi huu kwa furaha kabisa na nina uhakika kupitia mradi huu tutalima na kupata mazao mengi hatutakuwa na njaa lakini pia mazao mengine tutauza ili tujenge nyumba nzuri, tusomeshe watoto hata kijiji chetu kitabadilika, cha msingi hapa tuutumie vizuri” alisema Monica Severine Mkulima kutoka kijiji cha Mwasubuya

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, Mhandisi. Wilbert Siogopi amesema zana za kilimo zilizokabidhiwa na Kampuni ya Agricom zitawasaidia wakulima kuongeza uzalishaji wa zao la mpunga  na hivyo kuongeza pato la kaya zao na kukuza uchumi wa Halmashauri na Taifa kwa ujumla.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema dhamira ya Serikali ni kuufanya Mradi wa Umwagiliaji Mwasubuya kuwa wa mfano ambao watu kutoka sehemu mbalimbali za dunia watakuja kujifunza, ambapo amebainisha kuwa mpunga utakaolimwa utakuwa wa aina moja,utalimwa mara mbili kwa mwaka  na hautatumia mbolea za viwandani.

Ameongeza kuwa pamoja na kilimo cha mpunga, Serikali mkoani humo imekusudia kufunga kinu cha kukoboa mpunga na kupanga madaraja ya mchele na kupitia mradi huo pia kutakuwa na ufugaji wa samaki katika Bwawa la Mwasubuya ambapo vifaranga vitawekwa na ufugaji kupitia vizimba utafanyika sambamba na kufuga samaki katika baadhi ya mashamba ya mpunga.

“Kwenye bwawa mle tutaweka vifaranga vya sangara, kambare na sato pia katika ekari zitakazolimwa ekari 10 zitatengwa ambazo mkulima atalima mpunga na kufuga samaki kwa wakati mmoja, wakati akivuna mpunga anavuna na samaki; tunataka kufunga kinu cha kukoboa mpunga na kupanga madaraja, nawaambia maisha yenu yatabadilika, hapa ni mahali tunataka kuiambia dunia Simiyu ni nini” alisema Mtaka.

Akizungumzia namna wakulima watakavyolipa deni la mkopo wa zana bora za kilimo kutoka Agricom, Mtaka amesema Halmashauri italima shamba lote ekari 514, itatoa mbegu kwa wakulima, itapanda na kuvuna na baadaye itachukua sehemu ya mavuno(gunia 10 kwa ekari)  kutoka katika matarajio ya mavuno  ya kati ya gunia 30 hadi 42 kwa ekari, ili kufidia gharama za uzalishaji na kurejesha deni.

Naye Mkurugenzi wa Kampuni ya Agricom, Bi Angelina Ngalula amesema kampuni hiyo inafanya kazi na Halmashauri na wakulima walio tayari na kubainisha kuwa imekopesha Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi mashine za kulimia, kupandia na kuvunia zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 200 ambazo kwa mujibu wa makubaliano zitalipwa baada ya mavuno.

Mradi wa Umwagiliaji wa Mwasubuya una eneo lenye ukubwa wa ekari 700 zinazofaa kwa kilimo cha umwagiliaji na umesajiliwa kwa Jina la Umoja wa Umwagiliaji Mwasubuya (UMWASU) wenye wanachama 198.
MWISHO


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akitoa maelezo kwa Mkurugenzi wa Agricom Africa, Bi. Anjelina Ngalula  juu ya aina ya kilimo cha mpunga iitwayo Shadidi kilicholimwa katika baadhi ya mashamba yaliyo katika Mradi wa Uwagiliaji wa Mwasubuya wilayani Bariadi, kabla ya makabidhiano ya zana bora za kilimo kati ya Kampuni hiyo na Wakulima walio katika Mradi huo, Septemba 03, 2018 katika Kijiji cha Mwasubuya.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na wananchi wa Mwasubuya akiwa katika Moja ya Zana ya kupandia mpunga ambayo ni miongoni mwa zana zilizokabidhiwa kwa ajili ya kuwawezesha  wakulima wa mradi wa Umwagiliaji wa Mwasubuya wilayani Bariadi, Septemba 03, 2018 katika Kijiji cha Mwasubuya.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na wananchi wa Mwasubuya akiwa katika trekta  ambalo ni miongoni mwa zana zilizokabidhiwa kwa ajili ya kuwawezesha  wakulima wa mradi wa Umwagiliaji wa Mwasubuya wilayani Bariadi kulima kilimo cha kisasa kupitia mradi huo, Septemba 03, 2018 katika Kijiji cha Mwasubuya.
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Bariadi, Eng. Wilbert Siogopi akiwaonesha baadhi ya viongozi na wananchi mfereji unaotoa maji kutoka bwawa la Mwasubuya kwenda kwenye mashamba ya Mradi wa Umwagiliaji Mwasubuya  ,  kabla ya makabidhiano ya zana bora za kilimo kati ya Kampuni hiyo na Wakulima walio katika Mradi huo, Septemba 03, 2018 katika Kijiji cha Mwasubuya.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(wa nne kushoto) akikata utepe kuashiria ufunguzi wa hafla ya  makabidhiano ya zana bora za kilimo kutoka Kampuni ya Agricom Africa kwa Wakulima wa Umwagiliaji  Mwasubuya, katika Kijiji cha Mwasubuya wilayani Bariadi, Septemba 03, 2018 katika Kijiji cha Mwasubuya.
Baadhi ya Wananchi wa Kijiji cha Mwasubuya wakishangilia jambo wakati wa hafla ya makabidhiano ya zana bora za kilimo kutoka Kampuni ya Agricom Africa kwa Wakulima wa Umwagiliaji  Mwasubuya, katika Kijiji cha Mwasubuya wilayani Bariadi, Septemba 03, 2018 katika Kijiji cha Mwasubuya.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (wa tatu kulia) na baadhi ya viongozi na wananchi  wakielekea kuangalia Bwawa na baadhi ya mashamba katika Mradi wa Umwagiliaji wa Mwasubuya, kabla ya makabidhiano ya zana bora za kilimo kutoka  Kampuni ya Agricom Africa na Wakulima walio katika Mradi huo, Septemba 03, 2018 katika Kijiji cha Mwasubuya.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka akiteta jambo na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe. Enock Yakobo , katika hafla ya makabidhiano ya zana bora za kilimo kutoka  Kampuni ya Agricom Africa na Wakulima walio katika Mradi wa Umwagiliaji , Septemba 03, 2018 katika Kijiji cha Mwasubuya.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe. Enock Yakobo, akizungumza na baadhi ya viongozi mara baada makabidhiano ya zana bora za kilimo kutoka  Kampuni ya Agricom Africa na Wakulima walio katika Mradi wa Umwagiliaji Mwasubuya , Septemba 03, 2018 katika Kijiji cha Mwasubuya.
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Bariadi, Eng. Wilbert Siogopi akitoa taarifa  ya Mradi wa Umwagiliaji wa Mwasubuya  ,  kabla ya makabidhiano ya zana bora za kilimo kati ya Kampuni ya Agricom Africa kwa Wakulima walio katika Mradi huo, Septemba 03, 2018 katika Kijiji cha Mwasubuya.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Mwasubuya wakati wa hafla ya makabidhiano ya zana bora za kilimo kutoka  Kampuni ya Agricom Africa  kwa Wakulima walio katika Mradi wa Umwagiliaji Mwasubuya,, Septemba 03, 2018 katika Kijiji cha Mwasubuya
Baadhi ya Wananchi wa Kijiji cha Mwasubuya wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, katika  hafla ya makabidhiano ya zana bora za kilimo kutoka  Kampuni ya Agricom Africa  kwa Wakulima walio katika Mradi wa Umwagiliaji Mwasubuya,, Septemba 03, 2018 katika Kijiji cha Mwasubuya.
Kutoka kulia Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe. Enock Yakobo, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka na Mkurugenzi wa Agricom Africa, Bi. Angelina Ngalula wakifurahia jambo, katika  hafla ya makabidhiano ya zana bora za kilimo kutoka  Kampuni ya Agricom Africa  kwa Wakulima walio katika Mradi wa Umwagiliaji Mwasubuya, Septemba 03, 2018 katika Kijiji cha Mwasubuya.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe. Enock Yakobo, akizungumza na baadhi ya viongozi mara baada makabidhiano ya zana bora za kilimo kutoka  Kampuni ya Agricom Africa na Wakulima walio katika Mradi wa Umwagiliaji , Septemba 03, 2018 katika Kijiji cha Mwasubuya.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akicheza wimbo maalum pamoja na wananchi  wa Kijiji cha Mwasubuya na baadhi ya viongozi wa mkoa huo katika  hafla ya makabidhiano ya zana bora za kilimo kutoka  Kampuni ya Agricom Africa  kwa Wakulima walio katika Mradi wa Umwagiliaji Mwasubuya, Septemba 03, 2018 katika Kijiji cha Mwasubuya.
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Bariadi, Mhe. Juliana Mahongo akiwa katika trekta ambalo ni moja ya zana zilizokabidhiwa na Kampuni ya Agricom Africa  kwa Wakulima walio katika Mradi wa Umwagiliaji Mwasubuya, Septemba 03, 2018 katika Kijiji cha Mwasubuya.
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Mwasubuya, wakati wa hafla ya makabidhiano ya zana bora za kilimo kutoka  Kampuni ya Agricom Africa  kwa Wakulima walio katika Mradi wa Umwagiliaji Mwasubuya,, Septemba 03, 2018 katika Kijiji cha Mwasubuya.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akitoa maelezo kwa Mkurugenzi wa Agricom Africa, Bi. Angelina Ngalula  juu ya aina ya kilimo cha mpunga iitwayo Shadidi kilicholimwa katika baadhi ya mashamba yaliyo katika Mradi wa Uwagiliaji wa Mwasubuya wilayani Bariadi, kabla ya makabidhiano ya zana bora za kilimo kati ya Kampuni hiyo na Wakulima walio katika Mradi huo, Septemba 03, 2018 katika Kijiji cha Mwasubuya.
Baadhi ya Viongozi wa Wilaya ya Bariadi na Mkoa wa Simiyu wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, katika  hafla ya makabidhiano ya zana bora za kilimo kutoka  Kampuni ya Agricom Africa  kwa Wakulima walio katika Mradi wa Umwagiliaji Mwasubuya,, Septemba 03, 2018 katika Kijiji cha Mwasubuya.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!