Sunday, September 9, 2018

SERIKALI YAWAHAKIKISHIA WANANCHI WANAOISHI MAENEO YANAYOZUNGUKA ZIWA VICTORIA KUPATA MAJI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amesema Serikali itahakikisha maeneo yote yanayozunguza Ziwa Victoria yanapata maji safi na salama ili kuwaondolea adha wananchi wa  maeneo hayo ambayo yanazungukwa na rasimali hiyo muhimu.

Rais Magufuli ameyasema hayo leo wakati akizungumza na wananchi wa kata ya Lamadi mara baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa mradi wa maji wa Lamadi wilayani Busega mkoani Simiyu, ambao umegharimu shilingi bilioni 12.8 fedha ambazo ni mkopo kutoka Benki ya Maendeleo ya Ufaransa na Benki ya Uwekezaji ya Jumuiya ya Ulaya.

“Tumeamua Serikali ya Awamu ya Tano kuanza mpango wa kuhakikisha miji yote iliyo kando kando ya Ziwa Victoria inapata maji na ndiyo maana Lamadi mmepaa maji hongereni sana; mradi huu utatoa lita milioni 3.3 kwa siku mahitaji ya maji ya hapa ni lita milioni 1.8 kwa hiyo ni maji mengi yatakuwa yanatoka kwa siku kuliko mahitaji” alisema Rais Magufuli.

Aidha, amewataka Wananchi wa Wilaya ya Busega kuutunza mradi huo na akawaonya kuwa endapo watahujumu miundombinu na kuuharibu serikali haitapeleka mradi mwingine.

Naye Waziri wa maji na Umwagiliaji, Mhe. Makame Mbarawa amesema mradi huo utakapo kamilika mwezi Mei 2018 utawahudumia zaidi ya watu laki tatu watapa maji safi na salama.

Prof. Makame Mbalawa amesema ili kuondokana na changamoto ya maji katika Mkoa wa Simiyu Serikali imekusudia kutekeleza mradi mkubwa wa Maji kutoka Ziwa Victoria utakaowanufaisha wananchi wa Wilaya ya Bariadi,Itilima na Mwanhuzi Meatu, ambao utagharimu shilingi bilioni 378.

Pamoja na kuweka Jiwe la Msingi, Mhe. Rais Magufuli pia amefungua Jengo la Wagonjwa wa nje (OPD) la Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu, Kufungua Mtandao wa barabara za lami Mjini Bariadi zilizojengwa chini ya mradi wa ULGSP na kuweka jiwe la Msingi Ujenzi wa Barabara ya Bariadi-Maswa inayojengwa kwa kiwango cha lami yenye refu wa KM 49.7.

Sepemba 09, 2018 Mhe. Rais Magufuli anaendelea na ziara mkoani Simiyu ambapo atapita na kufanya mkutano wa hadhara Lagangabilili Itilima na kuelekea Meatu.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na viongozi mbalimbali mara baada ya kuweka Jiwe la Msingi la Mradi wa Maji wa Lamadi, wakati wa ziara yake mkoani Simiyu, Septemba 08, 2018.



Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Prof. Makame Mbarawa (kulia)akimuongoza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.  Dkt. John Pombe Magufuli kwenda katika eneo ambalo aliweka Jiwe la Msingi la Mradi wa Maji wa Lamadi, wakati wa ziara yake mkoani Simiyu, Septemba 08, 2018.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe.  Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Mkoa wa Simiyu mara baada ya kufungua Mtandao wa barabara za Lami za Mjini Bariadi,  wakati wa ziara yake mkoani Simiyu, Septemba 08, 2018.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe.  Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mkurugenzi wa Shirika la Maendeleo la Ufaransa kabla ya kuweka Jiwe la Msingi la Mradi wa Maji wa Lamadi, wakati wa ziara yake mkoani Simiyu, Septemba 08, 2018.
 Kutoka kushoto Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka  na Katibu Tawala wa Mkoa, Bw. Jumanne Sagini wakiteta jambo, wakati wa ziara ya Mhe. Rais Magufuli  mkoani Simiyu, Septemba 08, 2018.  
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli akiteta jambo na Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia hapa nchini , Bi. Bella Bird mara baada ya kufungua Mtandao wa barabara za Lami za Mjini Bariadi ambazo zinajengwa kwa edha za mkopo kutoka benki hiyo chini ya mradi wa ULGSP,  wakati wa ziara yake mkoani Simiyu, Septemba 08, 2018.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto,Mhe. Ummy Mwalimu akitoa taarifa ya Ujenzi wa Jengo la Wagonjwa wa Nje la Hospitali ya Rufaa ya Mkoa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, ambaye alilifungua jengo hilo Septemba 08, 2018 akiwa katika ziara yake ya siku tatu mkoani humo.
Baadhi ya viongozi na wananchi wa mkoa wa Simiyu, wakimsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli katika Mkutano wa hadhara uliofanyika Septemba 08, 2018 kwenye Viwanja vya Shule ya Msingi Salunda Mjini Bariadi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka   akisalimiana na Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia hapa nchini , Bi. Bella Bird mara baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli kufungua Mtandao wa barabara za Lami za Mjini Bariadi ambazo zinajengwa kwa edha za mkopo kutoka benki hiyo chini ya mradi wa ULGSP,  wakati wa ziara yake mkoani Simiyu, Septemba 08, 2018.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe.  Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Mkoa wa Simiyu mara baada ya kufungua Mtandao wa barabara za Lami za Mjini Bariadi,  wakati wa ziara yake mkoani Simiyu, Septemba 08, 2018.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikata utepe kuweka Jiwe la msingi, ujenzi wa barabara ya Bariadi-Maswa yenye urefu wa KM 49.7 inayojengwa kwa kiwango cha lami , Septemba O8, 2018 wakati akiwa katika ziara yake ya siku tatu mkoani humo.


0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!