Thursday, September 20, 2018

SIMIYU YAZINDUA UPIMAJI WA MAENEO YA WAKULIMA, WAFUGAJI KWA KUTUMIA TEKNOLOJIA YA NDEGE NYUKI (DRONES)


Mkoa wa Simiyu umezindua Mpango wa kupima maeneo ya wafugaji na wakulima kwa kutumia teknolojia ya kisasa ya ndege nyuki (drones) lengo likiwa ni kuwawezesha kuyatambua maeneo yao na kupewa hati miliki na baadaye kuyawekea miundombinu muhimu ya ufugaji na kilimo na kuondokana na migogoro kati ya wakulima na wafugaji.

Zoezi hilo limezinduliwa na  Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka katika kata ya Ng’hoboko wilayani Meatu na linatekelezwa Chini ya Serikali kwa Kushirikiana na Taasisi Ya Utafiti wa Masuala ya Kiuchumi na Kijamii (ESRF).

Amesema Mkoa huo ndiyo unaoongoza kwa kilimocha pamba nchini na ni miongoni mwa mikoa yenye ng’ombe wengi nchini, kwa kuwa wakulima na wafugaji wanamiliki ardhi ni vema maeneo yao yakapimwa wakapewa hati miliki na baadaye watalaam wa ardhi wawasaidie kuandaa mpango wa matumizi bora ya ardhi.

Ameongeza kuwa wafugaji wa mkoa wa Simiyu wamekuwa wakitozwa faini katika maeneo mbalimbali hivyo ili kuondokana na kadhia hiyo maeneo yao yakipimwa na wakaweka miundombinu muhimu kama vile mabwawa, visima, majosho na maeneo ya malisho wataondokana na uchungaji wa mifugo na kwenda kwenye ufugaji wenye tija

“Tungehitaji mpime mashamba yenu yakishapimwa mtapewa hati, watalaam wa halmashauri watawatengenezea mpango wa matumizi bora ya ardhi na kuwashauri namna sahihi ya uwekeaji wa miundombinu kama majosho, mabwawa, visima ili muwe wafugaji wenye tija ambao hamtapigwa faini wala kuibiwa ng’ombe” alisema.

Kwa upande wake Mkuu wa Mfumo kutoka Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Kiuchumi na Kijamii(ESRF) Bw. John Kajiba amesema upimaji kwa kutumia teknolojia ya ndege nyuki utafanyika  kwa urahisi  na haraka zaidi na ikilinganishwa na upimaji wa watu moja kwa kwa moja.

“Uzuri wa kutumia ndege nyuki ni kwamba tutatumia muda mfupi sana kupima eneo kubwa kwa wakati mmoja mfano,  eneo ambalo lngeweza kupimwa na watu wane kwa muda wa siku nne drone(ndege nyuki) inafanya kwa muda wa siku moja” alisema.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu, Mhe. Pius Machungwa amesema upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji utawasaidia kutatua migogoro kati ya wakulima na wafugaji na kupata hati ziatazowasaidia kuchukua mikopo kwenye taasisi za kifedha na kufanya shughuli za maendeleo kupitia maeneo yao
Nao wananchi wa Meatu wanasema wameupokea mpango huo kwa mikono miwili  kwa sababu watakuwa na uhakika wa umiliki wa maeneo yao baaada ya kupewa hati ambazo pia wamesema zitawasaidia kukopa mitaji ya kufuga na kulima kisasa na kwa tija.
“ Tumeupokea mradi huu kwa mikono miwili maana tutakapopimiwa maeneo yetu tutakuwa tunakopesheka kwenye taasisi za fedha, vile vile tutakuwa tumeondokana na migogoro kati ya wakulima na wafugaji kwa sababu maeneo yetu yatakuwa na mipaka iliyo wazi na kila mmoja atakuwa na hati ya kumili eneo lake” alisema John Mchagula mfugaji kutoka Kijiji cha Ng’hoboko
MWISHO
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akijiandaa kurusha angani ndege nyuki (drone) inayotumika kupima ardhi, katika uzinduzi wa zoezi la upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji mkoani humo, ambalo limefanyika katika Kata ya Ng’hoboko wilayani Meatu,  Septemba 19, 2018.
Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Merdad Kalemani(katikati mbele) na baadhi ya viongozi wa wilaya ya Meatu na Mkoa wa Simiyu wakifurahia jambo wakati wa ziara ya Waziri huyo Septemba 20, 2018 wilayani Meatu.
Mtaalam wa kutumia Ndege nyuki(drone) akiwaonesha viongozi na wananchi namna kifaa hcho cha kisasa kinavyorushwa angani na kwenda kukusanya taarifa zinazotakiwa, katika uzinduzi wa zoezi la upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji mkoani humo, ambalo limefanyika katika Kata ya Ng’hoboko wilayani Meatu,  Septemba 19, 2018.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka/(kulia) akiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Mhe.Dkt. Joseph Chilongani, katika hafla ya  uzinduzi wa zoezi la upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji mkoani humo, ambalo limefanyika katika Kata ya Ng’hoboko wilayani Meatu,  Septemba 19, 2018.
Baadhi ya wananchi wa Wilaya ya Meatu wakiiitazama ndege nyuki(drone) kifaa cha kisasa ambacho kitatumiwa kupima maeneo makubwa, katika uzinduzi wa zoezi la upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji mkoani humo, ambalo limefanyika katika Kata ya Ng’hoboko wilayani Meatu,  Septemba 19, 2018.
Baadhi ya Viongozi wa Mkoa wa Simiyu na Wilaya ya Meatu wakifauatilia burudani kutoka katika Kikundi cha BASEKI (hawapopichani), katika uzinduzi wa zoezi la upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji mkoani humo, ambalo limefanyika katika Kata ya Ng’hoboko wilayani Meatu,  Septemba 19, 2018.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu, Bw. Fabian Manoza  akiwasilisha taarifa ya zoezi la upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji wilayani humo, katika uzinduzi wa zoezi hilo mkoani Simiyu, ambalo limefanyika katika Kata ya Ng’hoboko wilayani Meatu,  Septemba 19, 2018.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na wananchi wa Kata ya  Ng’hoboko, wakati wa   uzinduzi wa zoezi la upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji mkoani humo, ambalo limefanyika katika Kata ya Ng’hoboko wilayani Meatu,  Septemba 19, 2018.
Baadhi ya wakulima na wafugaji wa Wilaya ya Meatu Mkoani Simiyu, wakimsikiliza mkuu wa Mkoa huo wakati wa   uzinduzi wa zoezi la upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji mkoani humo, ambalo limefanyika katika Kata ya Ng’hoboko wilayani Meatu,  Septemba 19, 2018.
Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Mhe. Dkt. Joseph Chilongani  akizungumza na wananchi wa Kata ya  Ng’hoboko wakati wa   uzinduzi wa zoezi la upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji, ambalo limefanyika katika Kata ya Ng’hoboko wilayani Meatu,  Septemba 19, 2018.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Enock Yakobo akielezea utendaji kazi wa Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Anthony Mtaka wakati wa   uzinduzi wa zoezi la upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji mkoani humo, ambalo limefanyika katika Kata ya Ng’hoboko wilayani Meatu,  Septemba 19, 2018. 
 
Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Simiyu, Lumen Mathias  akielezea utendaji kazi wa Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Anthony Mtaka wakati wa   uzinduzi wa zoezi la upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji mkoani humo, ambalo limefanyika katika Kata ya Ng’hoboko wilayani Meatu,  Septemba 19, 2018.
Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe. Dkt. Seif Shekalaghe   akiwasalimia wananchi wa Kata ya  Ng’hoboko, wakati wa uzinduzi wa zoezi la upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji, ambalo limefanyika katika Kata ya Ng’hoboko wilayani Meatu,  Septemba 19, 2018.
Kutoka kushoto Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Enock Yakobo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu, Bw. Fabian Manoza,  Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Mhe. Dkt. Joseph Chilongani  na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Meatu, Mhe. Pius Machungwa,(anaonekana nyuma) wakifurahia jambo,  wakati wa uzinduzi wa zoezi la upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji, ambalo limefanyika katika Kata ya Ng’hoboko wilayani Meatu,  Septemba 19, 2018.
Mtaalam wa Ndege nyuki akiwaeleza wakulima na wafugaji na wananchi wengine juu ya namna kifaa hicho cha kisasa kinachotumika katika  zoezi la upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji, ambalo limezinduliwa katika Kata ya Ng’hoboko wilayani Meatu,  Septemba 19, 2018.
Baadhi ya Viongozi wa Mkoa wa Simiyu na Viongozi wa  Wilaya ya Meatu wakiiitazama ndege nyuki(drone) kifaa cha kisasa ambacho kitatumiwa kupima maeneo makubwa, katika uzinduzi wa zoezi la upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji mkoani humo, ambalo limefanyika katika Kata ya Ng’hoboko wilayani Meatu,  Septemba 19, 2018.

Baadhi ya Viongozi wa Mkoa wa Simiyu na Viongozi wa  Wilaya ya Meatu wakiitazama ndege nyuki(drone) kifaa cha kisasa ambacho kitatumiwa kupima maeneo makubwa, katika uzinduzi wa zoezi la upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji mkoani humo, ambalo limefanyika katika Kata ya Ng’hoboko wilayani Meatu,  Septemba 19, 2018.
Kutoka kushoto Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Enock Yakobo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu, Bw. Fabian Manoza,  Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Mhe. Dkt. Joseph Chilongani  na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Meatu, Mhe. Pius Machungwa,(anaonekana nyuma) wakifurahia jambo,  wakati wa uzinduzi wa zoezi la upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji, ambalo limefanyika katika Kata ya Ng’hoboko wilayani Meatu,  Septemba 19, 2018
Baadhi ya viongozi wa Vijiji na kata za Wilaya ya Meatu, wakitambulishwa wakati wa uzinduzi wa zoezi la upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji, ambalo limefanyika katika Kata ya Ng’hoboko wilayani humo  Septemba 19, 2018.
Mtaalamu wa Ndege nyuki akitoa maelezo ya namna kifaa hicho kinavyofanya kazi kwa  Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, wakati wa uzinduzi wa zoezi la upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji, ambalo limefanyika katika Kata ya Ng’hoboko wilayani Meatu,  Septemba 19, 2018.
Mtaalam wa kutumia Ndege nyuki(drone) akiwaonesha viongozi na wananchi namna kifaa hcho cha kisasa kinavyorushwa angani na kwenda kukusanya taarifa, katika uzinduzi wa zoezi la upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji mkoani humo, ambalo limefanyika katika Kata ya Ng’hoboko wilayani Meatu,  Septemba 19, 2018.

Kikundi cha Burudani kiitwacho BASEKI  kutoka Bariadi Mjini kikitoa burudani ya ngomba katika uzinduzi wa zoezi la upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji mkoani humo, ambalo limefanyika katika Kata ya Ng’hoboko wilayani Meatu,  Septemba 19, 2018.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!